Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Kwa nini wasichana wakiingia utu uzima damu zinaanza kutoka kwenye uke?

Featured Image
Kutoka damu (hedhi) kwa mara ya kwanza kunaitwa kuvunja ungo na hii ni dalili ya mtoto wa kike kuingia utu uzima,0 yaani kuwa mwanamke. Wasichana wanavunja ungo kati ya umri wa miaka 8 na umri wa miaka 18. Lakini, kuvunja ungo haina maana kwamba unahitaji kuanza kujamii ana. Kwa sababu ukijamii ana kuna hatari ya kupata mimba!

Mwanzoni siku za hedhi zinaweza kuwa na mabadiliko sana. Ni baada ya muda ndipo msichana anaanza kwenda mwezini mara moja kila mwezi. Kwa wanawake wengi ni kila baada ya siku 28, hata hivyo, wengine huweza kupata hedhi chini au zaidi ya siku hizo. Idadi ya siku katika mzunguko wa hedhi ni siku 21 hadi 35.Ukitaka kuelewa kabisa maana ya kutoka damu za mwezi, lazima nieleze kuhusu mzunguko wa hedhi. Siku ya kwanza ya damu huhesabiwa kama siku ya kwanza ya mzunguko. Baada ya damu kutoka, yai moja linaanza kukua ndani ya kokwa.

Na vilevile utando ndani ya mfuko wa uzazi huanza kujengeka ili ukaribishe mimba. Kati ya siku 11 au 14 yai hupevuka ndani ya kokwa na halafu husafiri kwenye mirija ya kupitishia mayai hadi kwenye mfuko wa uzazi. Mwanamke anapata mimba kama yai likirutubishwa na mbegu ya kiume ndani ya mirija ya kupitisha mayai, i ina maana, kwamba atakuwa amejamii ana kipindi cha siku chache kabla ya yai kupevuka au siku yai linapopevuka. Kama yai halikurutubishwa, basi hufa na hutangulia kutoka kama ute, pia utando kwenye mfuko wa uzazi na kuta za uzazi hubomoka na kutoka kama damu. Hii ndiyo hedhi yenyewe.

Endapo msichana amejamiiana na mvulana na yai likarutubushwa, hataona hedhi na aelewe kwamba kuna uwezekano kwamba mimba imetungwa.

Mzunguko wa hedhi kwa baadhi ya wasichana hauna mpangilio mwanzoni, hivyo endapo hupati hedhi inayolingana kila mwezi usijali.

Katika hali ya kawaida usipopata hedhi na hukujamiiana na mvulana, basi inawezekana ni mabadiliko tu ya mwili. Hali hii ikiendelea au ukiwa na wasiwasi unashauriwa kumuona mtaalamu wa afya
AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Nifanyeje kuepuka vishawishi vya kujamiiana kutoka kwa watu wengine, hasa wakubwa?

Nifanyeje kuepuka vishawishi vya kujamiiana kutoka kwa watu wengine, hasa wakubwa?

Vijana wengi wanajikuta wanatumbukia katika matatizo mazito kama kupata mimba mapema, utoaji wa m... Read More

Njia za Kujenga Uhusiano Imara na Msichana

Njia za Kujenga Uhusiano Imara na Msichana

Kujenga uhusiano na msichana ni jambo muhimu katika maisha ya kimapenzi. Uhusiano unapokuwa imara... Read More

Je, kuna umuhimu kuweka mazingira ya kimapenzi kabla ya kufanya ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu kuweka mazingira ya kimapenzi kabla ya kufanya ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu wa kuweka mazingira ya kimapenzi kabla ya kufanya ngono au kufanya mapenzi? Ndio... Read More

Je, ni kweli kwamba kuvuta bangi kunaongeza akili na uwezo wa kufikiri?

Je, ni kweli kwamba kuvuta bangi kunaongeza akili na uwezo wa kufikiri?

Hapana, hii si kweli! Vijana wanaoamini kwamba wana uwezo wa kufikiri baada ya kuvuta bangi kwa s... Read More

Kumaliza ashiki au hamu ya kufanya mapenzi

Kumaliza ashiki au hamu ya kufanya mapenzi

Kwa vijana mara nyingine siyo rahisi kufahamu afanye nini mara anapopata ashiki (hamu) ya kutaka ... Read More

Jinsi ya Kuanza Mazungumzo na Msichana Unayempenda

Jinsi ya Kuanza Mazungumzo na Msichana Unayempenda

Kuanza mazungumzo na msichana unayempenda inaweza kuwa vigumu, lakini pia inaweza kuwa jambo la k... Read More

Kwa nini Albino tunaonekana kama mzigo katika familia zetu?

Kwa nini Albino tunaonekana kama mzigo katika familia zetu?

Watu wanaohitaji kupewa uangalizi maalumu wanaweza
kuonekana ni mzigo kwa kuwa wanaweza waka... Read More

Je, watu huchanganyikiwa baada ya matumizi ya dawa za kulevya?

Je, watu huchanganyikiwa baada ya matumizi ya dawa za kulevya?

Kuna i imani potofu kwamba wote wenye matatizo ya akili wamekuwa hivyo kutokana na matumizi ya da... Read More

Jinsi ya Kuvutia Wasichana: Vidokezo vya Kuchumbiana na Wasichana

Jinsi ya Kuvutia Wasichana: Vidokezo vya Kuchumbiana na Wasichana

Jambo rafiki yangu! Katika maisha ya kila siku, tunakutana na wasichana wengi ambao tunapenda kuw... Read More

Je, watu wanapendelea ngono/kufanya mapenzi ya kawaida au ngono/kufanya mapenzi yenye michezo ya kubahatisha?

Je, watu wanapendelea ngono/kufanya mapenzi ya kawaida au ngono/kufanya mapenzi yenye michezo ya kubahatisha?

Je, unajua kwamba wengi wetu tunapenda kufanya mapenzi ya kawaida? Na pia unajua kwamba kuna wale... Read More

Kwa nini uume unasimama mara nyingine wakati wa kuamka asubuhi?

Kwa nini uume unasimama mara nyingine wakati wa kuamka asubuhi?

Ni kweli kwamba mara nyingi hali hii huwatokea wavulana na wanaume. Ndani ya uume kuna mishipa mingi... Read More
Sababu za ukeketaji

Sababu za ukeketaji

Hakuna hata mmoja anayejua hasa kwa nini, na lini desturi
imeanza. Jamii inatoa maelezo tofa... Read More