Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
AckyShine

MAPISHI YA LADU

Featured Image

VIAMBAUPISHI

Unga - 6 vikombe

Samli - ½kikombe

Baking Powder - ½kijiko cha chai

Maziwa- 1 kikombe

Maji -Kisia kiasi kama unga bado mzito

VIAMBAUPISHI VYA SHIRA

Sukari - 5 vikombe

Maji - 2 1/2 vikombe

Vanilla - 2 vijiko vya chai

Rangi ya orange - 1 kijiko cha chai

Iliki ya unga - 1 Kijiko cha chai

MAANDALIZI

Changanya unga wa dengu, samli, baking powder pamoja na maziwa katika mashine ya keki (cake mixer).
Ukisha changanya angalia kama mchanganyiko wako umekua mwepesi kidogo kuliko wa keki, kama bado mzito basi ongeza maji kiasi.
Kisha weka mafuta kiasi kwenye karai,weka na samli kikombe kimoja, weka kwenye moto wa kiasi.
Mafuta yakisha pata moto, chukua kijiko kikubwa cha matundu chota mchanganyiko wako na kijiko cha kawaida tia kwenye kijiko cha matundu. Hakikisha kijiko cha matundu kiwe juu ya karai ili mchanganyiko wako uchuruzike ndani ya mafuta yalio pata moto.
Pika ndani ya mafuta mpaka iwive, ila usiache ikawa brown.
Toa mchanganyiko ulowiva tia ndani ya shira uliyo pika. Hakikisha shira iwe imepoa kabla ya kutia mchanganyiko huo.
Endelea kupika mchanganyiko wako mpaka uishe, kila ukitoa katika mafuta hakikisha unatia ndani ya shira.
Ukishamaliza wote kanda huo mchanganyiko ulokua ndani ya shira mpaka uone shira yote imekauka (yaani iwe imeingia ndani ya mchanganyiko).
Tupia zabibu kavu na lozi zilizo katwa, changanya na mkono.
Wacha mchanganyiko katika bakuli, funika na foil mpaka siku ya pili.
Siku ya pili chukua mchanganyiko kiasi katika mkono tengeneza mviringo (round).

MAANDALIZI YA SHIRA

Katika sufuria, tia sukari, maji, iliki, vanilla na rangi.
weka kwenye moto wacha ichemke mpaka itowe povu (bubbles) juu.
Kisha toa povu, wacha shira kwenye moto kama dakika 3.
Hakikisha shira yako iwe inanata kiasi kwenye vidole, lakini iwe nyepesi kidogo kuliko shira ya kaimati.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Cornflakes

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Cornflakes

MAHITAJI

Unga - 1 Kikombe

Sukari ya kusaga - 3/4 Kikombe

Siagi - 125 gms

<... Read More
Mapishi ya samaki aina ya salmon

Mapishi ya samaki aina ya salmon

Wakati mwingine mtu unakuwa umechoka na usingependa kupoteza muda jikoni, so mlo wa chapchap unak... Read More

Mapishi ya Samaki wa kupaka

Mapishi ya Samaki wa kupaka

Mahitaji

Samaki (Tilapia 2)
Nyanya ya kopo (Tomato tin 1)
Kitunguu (Onion 1)Read More

Mapishi ya wali mtamu Wa Nazi Kwa Maharage Na Samaki Nguru Wa Kukaanga

Mapishi ya wali mtamu Wa Nazi Kwa Maharage Na Samaki Nguru Wa Kukaanga

Vipimo

Wali:

Mchele mpunga - 4 Vikombe

Tui la nazi - 6 vikombe

Chumvi... Read More

Jinsi ya kupika Wali Wa Karoti Na Nyama

Jinsi ya kupika Wali Wa Karoti Na Nyama

Viambaupishi: Wali

Mchele 3 Magi

Mafuta 1/4 kikombe

Karoti unakata refu refu ... Read More

Mapishi mazuri ya Uji wa ulezi

Mapishi mazuri ya Uji wa ulezi

Mahitaji

Unga wa ulezi (millet flour vijiko 3 vya chakula)
Maziwa fresh (milk 1/2 ki... Read More

Mapishi ya Pilau Ya Nyama ya Kusaga, Adesi Za Brauni Na Zabibu

Mapishi ya Pilau Ya Nyama ya Kusaga, Adesi Za Brauni Na Zabibu

Mahitaji

Mchele wa Par boiled au basmati - 5 vikombe

Nyama kondoo/mbuzi ya kusaga -... Read More

Mapishi ya Biriani Ya Tuna

Mapishi ya Biriani Ya Tuna

MAHITAJI

Mchele Basmati - Mugs 2 ½

Vitunguu (Vikubwa kiasi) - 3

Tuna - Vibat... Read More

Mapishi ya Ndizi za nazi na utumbo

Mapishi ya Ndizi za nazi na utumbo

Mahitaji

Ndizi mshale 10
Utumbo wa ng'ombe 1/2 kilo
Nazi ya kopo 1
Nyanya ... Read More

Mapishi ya Wali Wa Kichina Wa Kamba Na Kuku

Mapishi ya Wali Wa Kichina Wa Kamba Na Kuku

MAHITAJI

Mchele wa pishori (basmati) - 4

Nyama ya kuku bila mafupa - 1 Lb

Kam... Read More

Mapishi ya Haliym Ya Nyama Mbuzi -Bokoboko La Pakistan

Mapishi ya Haliym Ya Nyama Mbuzi -Bokoboko La Pakistan

Mahitaji

Nyama ya mbuzi au ng’ombe ya mafupa - 2 LB

Mchanganyiko wa dengu (hadesi... Read More

Jinsi ya kutengeneza Slesi Za Chokoleti Na Karameli

Jinsi ya kutengeneza Slesi Za Chokoleti Na Karameli

VIAMBAUPISHI

Unga - 1 Magi (vikombe vya chai)

Sukari ya browni - ½ Magi

Siag... Read More