Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Wosia mzuri wa baba kwa mwanae

Featured Image

Mwanangu, mimi baba yako nimeishi miaka mingi kuliko wewe ndio maana unaniita baba. Ni kweli sijasoma kama wewe ulivyosoma Ila mambo niliyokutana nayo tangu nimezaliwa ni elimu tosha ambayo wewe huna. Sasa nataka nikupe Elimu hiyo ili ukijumlisha na elimu yako ya darasani ujue namna nzuri ya kuishi katika dunia hii iliyojaa mishangazo mingi.


Maisha ni jumla ya mambo yote unayoyatenda kila siku. Namaanisha kila unalolifanya Leo linaathiri maisha yako ya kesho kwa hali chanya au hali hasi. Na kama ni hali hasi ni kwa ukubwa gani halikadharika kama ni hali chanya ni kwa kiwango gani. Mwanangu kila jambo unalolifanya Leo huamua ni mlango gani Unaweza ingia Kesho lakini pia mlango upi huwezi ingia Kesho. Ndio maana ni muhimu kuijua Kesho yako ukiwa Leo.


Mwanangu ili ufanikiwe ni lazima ujue kuishi na watu vizuri. Na mimi sikushauri kabisa kwamba uwe na marafiki wengi. Kuwa na marafiki wengi ni moja ya eneo unaweza jitengenezea mtego mbaya wa kukuangamiza kesho yako. Mwenye hekima mmoja aliwahi kusema ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe. Mwanangu kwa kusema hivyo simaanishi uwe na maadui,hapana. Ila marafiki zako watakusaidia mlango unaotaka kuingia Kesho uingie kwa urahisi au kwa ugumu au usiingie kabisa na wakati mwingine Unaweza kuingia na wakahusika kukutoa kwa aibu kubwa. Ndio maana ni muhimu Kuwa na marafiki ila Kuwa nao wachache chagua kwa makini mno. Sio lazima kila akufaaye kwa dhiki ndiye awe rafiki. Kuna watu wanakufaa kwa dhiki Leo ila Kesho wakutumikishe Kuwa makini sana.


Mwanangu, kuwa makini sana na mahusiano yako ya kimapenzi maana yanagusa hisia zako na mtu unayehusiana naye moja kwa moja. Hivyo basi kuwa makini maana mahusiano hayo yanaweza kukufanya Kesho ukamkosesha raha utakayekuwa naye kama sio huyo uliyenaye leo ndie ukajaaliwa Kuwa naye Kesho. Mwanangu, Unaweza kuniona mshamba sababu ulimwengu wenu unaonekana kama haujali sana haya mambo ila tafadhari zingatia utakapofika Kesho utaelewa sana hiki ninachokuambia.


Mwanangu, jichunge sana na mambo unayoyafanya Leo na uwe muungwana na kupenda haki. Tamaa isikupeleke ukafanya mambo mabaya ambayo yatakulazimisha kutunza siri moyoni mwako hata kama utafika ile Kesho yako. Jiepushe kabisa na mambo mabaya ya siri ya nafsi. Hakuna utumwa mbaya kama utumwa ndani ya nafsi yako mwenyewe maana kila ukikumbuka nafsi itakusuta na kukukosesha raha ya kweli. Hivyo kubali na kuridhika na ulivyo kama huwezi kujiongeza kwa njia halali na za haki. Ni heri uwe masikini mwenye uhuru ndani kuliko uwe tajiri na maarufu mwenye siri mbaya ndani ya Moyo wako. Mwanangu tafadhari uwe makini sana.


Mwanangu, siwezi sahau kukwambia kuhusu Mungu. Maisha ya uchaji wa Mungu yatakuepusha na mengi. Hapa naomba unielewe kwamba usijifanye unamcha Mungu bali mche Mungu. Sio kwasababu unashida ya kufanikiwa ndio umche Mungu, hapana! Bali umche Mungu sababu ni Mungu na yeye ndiye anaijua Kesho yako vizuri kuliko wewe mwenyewe. Ukimshirikisha mambo yako na ukawa mwaminifu kwake hakika hatakuacha kamwe.


Mwanangu, usiku umeenda nenda kalale sasa ila usije ukapenda na kutamani waovu kwa uovu wao na wakakushawishi ujiunge nao. Tafadhari usikubali.


#Kizazi Ganzi#


JIFUNZE KUJIFUNZA


Mwl Makwaya
Kuwa Ni Kufanya.






Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE




Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke





Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.





[products columns="2" ids="30827"]


AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya Kukuza Nguvu ya Uhusiano wa Ndugu katika Familia yako

Jinsi ya Kukuza Nguvu ya Uhusiano wa Ndugu katika Familia yako

Asante kwa kuchagua kusoma makala yetu kuhusu jinsi ya kukuza nguvu ya uhusiano wa ndugu katika f... Read More

Jinsi ya Kuunganisha Kizazi: Kuweka Mipango na Kujenga Ushirikiano katika Familia

Jinsi ya Kuunganisha Kizazi: Kuweka Mipango na Kujenga Ushirikiano katika Familia

Kuunganisha kizazi ni muhimu sana katika familia. Ni jambo linalofanya familia iwe na nguvu na ku... Read More

Kuunda Muda na Nafasi ya Ubunifu katika Mahusiano yako

Kuunda Muda na Nafasi ya Ubunifu katika Mahusiano yako

Mahusiano ni muhimu sana katika maisha ya binadamu. Kuunda muda na nafasi ya ubunifu katika mahus... Read More

Njia za Kupunguza Mazoea ya Ubaguzi katika Mahusiano: Kujenga Usawa na Ushirikiano

Njia za Kupunguza Mazoea ya Ubaguzi katika Mahusiano: Kujenga Usawa na Ushirikiano

Mahusiano yoyote yanahitaji usawa na ushirikiano kati ya wapenzi. Hata hivyo, wakati mwingine huw... Read More

Jinsi ya kutambua Mahitaji ya Mawasiliano ya mke wako

Jinsi ya kutambua Mahitaji ya Mawasiliano ya mke wako

Kutambua mahitaji ya mawasiliano ya mke wako ni muhimu katika kudumisha uhusiano wenye afya na furah... Read More
Kuhamasisha Heshima na Uwiano katika Mahusiano ya Familia

Kuhamasisha Heshima na Uwiano katika Mahusiano ya Familia

Mahusiano ya familia ni muhimu sana katika maisha yetu ya kila siku. Kuwa na heshima na uwiano ka... Read More

Jinsi ya Kuelewa na kushughulikia tofauti za kiimani na mafundisho ya kidini na mpenzi wako

Jinsi ya Kuelewa na kushughulikia tofauti za kiimani na mafundisho ya kidini na mpenzi wako

Kama unapenda mtu wa imani tofauti na wewe, hapa kuna maoni kadhaa ambayo yanaweza kukusaidia kue... Read More

Jinsi ya Kuimarisha mawasiliano ya kimapenzi na mpenzi wako

Jinsi ya Kuimarisha mawasiliano ya kimapenzi na mpenzi wako

Kuimarisha mawasiliano ya kimapenzi na mpenzi wako ni muhimu kwa kuendeleza uhusiano wenye afya na k... Read More
Kuunda Uhusiano wenye Furaha na Chanya na Marafiki wa Mwenzi wako

Kuunda Uhusiano wenye Furaha na Chanya na Marafiki wa Mwenzi wako

Kuunda uhusiano wenye furaha na chanya na marafiki wa mwenzi wako ni muhimu sana katika kudumisha... Read More

Kukabiliana na Mazoea ya Kutowajibika katika Familia: Kuweka Nafasi ya Ushiriki na Ushirikiano

Kukabiliana na Mazoea ya Kutowajibika katika Familia: Kuweka Nafasi ya Ushiriki na Ushirikiano

Mazoea ya kutowajibika katika familia ni kitu ambacho kinaweza kusababisha migogoro kati ya wanaf... Read More

Jinsi ya Kujenga Furaha na Amani katika Ndoa na mke wako

Jinsi ya Kujenga Furaha na Amani katika Ndoa na mke wako

Kujenga furaha na amani katika ndoa na mke wako ni muhimu sana kwa ustawi wa uhusiano wenu. Hapa kun... Read More
Je, watu wanapenda kujaribu nafasi mpya za ngono/kufanya mapenzi?

Je, watu wanapenda kujaribu nafasi mpya za ngono/kufanya mapenzi?

  1. Je, watu wanapenda kujaribu nafasi mpya za ngono/kufanya mapenzi?

Hivi karibu... Read More