Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMS💌💕
AckyShine

Jinsi ya kupika pizza ya mboga mboga na cheese

Featured Image

MAHITAJI

1 kilo unga wa ngano
240 ml maji ya vugu vugu
2 olive oil kijiko kikubwa cha chakula
2 asali kijiko kidogo cha chai
1 chumvi kijiko kidogo cha chai
1 hamira ya chenga kijiko kidogo cha chai

JINSI YA KUPIKA

Chukua bakuli weka maji ya uvugu vugu, amira ya chenga, asali na chumvi kisha koroga ichanganyike vizuri acha itulie kwa dakika 10.
Kisha chukua olive oil na unga wa ngao mimina kidogo kidogo changanya mpaka ichanganyike safi kabisa kisha anza kukanda kama mchanganyiko wa chapati au maandazi.
Baada ya mchanganyiko wako kua mgumu safi kabisa funika bakuli lako na mfuko wa plastiki au cling film kwa muda wa saa 1 katika joto la chumba na mchanganyiko wako utaumuka baada ya muda huo. kisha ukandamize mchanganyiko huo wa unga na kua flati kama mwanzo.
Kata mafungu matano hadi saba ya ujazo sawa inategemea na ukubwa wa piza unaopenda we mlaji kisha sukuma umbo la duara.
Tengeneza mchuzi mzito wa nyanya kisha weka juu ya kitako cha piza na kuitandaza vizuri kwenye pizza yako kama unavyopaka siagi kwenye mkate. Usisahau kuweka chumvi na sukari kidogo katika mchuzi wa nyanya ili kukata uchachu.
Katakata nyanya, kitunguu, pili pili hoho, na bilinganya na kuziweka juu ya pizza yako kwa mpangilio ukitanguliza biringanya, ikifuatiwa na pili pili hoho, kitunguu maji na nyanya.
Kisha chukua mozarella cheese ikwaruze katika mkato mdogo rahisi kuyeyuka kwa kutumia kwaruzo la karoti linafaa.
kisha chukua mkwaruzo wa mozarella cheese na unyunyizie juu ya hizo mboga.
Weka pizza yako kwenye sahani ya bati au pizza pan ili isaidie kuiva upande wa chini.
Weka pizza yako kwenye oven ambayo imeshawashwa na ina joto 400 - 450 F. Choma kwa dakika 20 hadi 25 iwe kaukau na rangi ya kahawia pia cheese itakua imyeyuka na kusambaa vizuri juu ya pizaa.

NB: Unaweza weka mchanganyiko wa nyama yeyote ile kama salami, nyama ya ngombe, nyama ya kuku au samaki kwa kufata maelekezo sawa sawa na hii piza ya mboga, tofauti yake itakua huweki mboga unaweka nyama.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Mapishi ya Muhogo Na Mbatata Za Nazi Kwa Nyama Ngombe

Mapishi ya Muhogo Na Mbatata Za Nazi Kwa Nyama Ngombe

Vipimo - Mahitaji Ya Nyama

Nyama ya n’gombe ya mifupa - 3 lb

Tangawizi mbichi il... Read More

Vidokezo 10 vya Vitafunio visivyo na Karanga

Vidokezo 10 vya Vitafunio visivyo na Karanga

Vidokezo 10 vya Vitafunio visivyo na Karanga 🥜🚫

Kama unapenda kufurahia vitafunio na... Read More

Mapishi ya Chapati za maji za vitunguu

Mapishi ya Chapati za maji za vitunguu

Mahitaji

Unga wa ngano (plain flour) 1/4
Kitunguu kikubwa (chopped/slice onion) 1Read More

Jinsi ya kutengeneza Mkate wa mayai

Jinsi ya kutengeneza Mkate wa mayai

Mahitaji

Slice za mkate 6
Mayai 3
Chumvi
Olive oil

Matayarisho

... Read More
Jinsi ya kutengeneza Fagi Ya Kumumunyuka Mdomoni

Jinsi ya kutengeneza Fagi Ya Kumumunyuka Mdomoni

VIAMBAUPISHI

Maziwa mazito matamu (condensed milk) - 2 vibati

Sukari - 1 kikombeRead More

Jinsi ya kuandaa Vileja Vya Tambi

Jinsi ya kuandaa Vileja Vya Tambi

MAHITAJI

Tambi (vermiceli Roasted) Mifuko 2

Siagi - 4 Vijiko vya supu

Maziwa ... Read More

Mapishi ya Mchemsho wa ndizi na nyama

Mapishi ya Mchemsho wa ndizi na nyama

Mahitaji

Ndizi mbichi 6
Nyama ya ng'ombe (nusu kilo)
Viazi mviringo 2
Kitu... Read More

Jinsi ya kutengeneza Nangatai

Jinsi ya kutengeneza Nangatai

MAHITAJI

Unga wa ngano - 2 - 2 ¼ Vikombe

Siagi - 1 ½ Kikombe

Sukari - 1 Kik... Read More

Mapishi mazuri ya Wali Wa Kukaanga Kwa Kidari Cha Kuku

Mapishi mazuri ya Wali Wa Kukaanga Kwa Kidari Cha Kuku

Vipimo vya Wali:

Mchele - 3 vikombe

*Maji ya kupikia - 5 vikombe

*Kidonge cha s... Read More

Jinsi ya kutengeneza Biriani Ya Nyama Ya Ng'ombe

Jinsi ya kutengeneza Biriani Ya Nyama Ya Ng'ombe

Mahitaji

Nyama - 2 Ratili (LB)

Chumvi - kiasi

Mafuta - 1 Kikombe

Samli ... Read More

Mapishi ya Maharage

Mapishi ya Maharage

Mahitaji

Maharage (beans 2 vikombe vya chai)
Nazi (coconut milk kiasi)
Vitunguu... Read More

Mapishi ya Biriani Ya Tuna

Mapishi ya Biriani Ya Tuna

MAHITAJI

Mchele Basmati - Mugs 2 ½

Vitunguu (Vikubwa kiasi) - 3

Tuna - Vibat... Read More