Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Mapishi ya Wali, Mchuzi Wa Nazi Wa Samaki Nguru

Featured Image

Mahitaji

Mchele - 3 vikombe

Samaki Nguru (king fish) - 5 vipande

Vitunguu - 2

Nyanya/tungule - 4

Mafuta - 3 vijiko vya supu

Tui la nazi zito - 2 vikombe

Pilipili mbichi - 5-7

Kitunguu saumu(thomu/galic) - 7-9 chembe

Kotmiri - 1 msongo (bunch)

Bizari ya samaki - 1 kijiko cha chai

Ndimu - 2-3

Chumvi - kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha samaki, kata vipande kiasi weka kando.
Katakata kitunguu na nyanya vipande vidogo vidogo sana (crush) .
Katakata kotmiri weka kando.
Saga pamoja, pilipili mbichi, kitunguu thomu, ndimu na chumvi.
Changanya pamoja na bizari ya samaki kisha paka katika vipande vya samaki acha kidogo vikolee.
Weka mafuta katika sufuria au karai, kaanga vitunguu kidogo tu kisha tia nyanya/tungule endelea kukaanga hadi vilainike na kupondeka.
Tia kikombe kimoja na nusu cha tui la nazi, kisha tia vipande vya samaki na masala yake, acha mchuzi uchemke samaki aive. Ongeza chumvi, ndimu, pilipili ikihitajika.
Ongezea tui lilobakia acha motoni kwa daika chache tu.
Epua mwagia kotmiri mchuzi ukiwa tayari.

Pika wali wa maji/mweupe kama kawaida utolee na mchuzi.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya kupika Pilau ya Nyama ya Kusaga Na Mboga Mchanganyiko

Jinsi ya kupika Pilau ya Nyama ya Kusaga Na Mboga Mchanganyiko

Mahitaji

Mchele - 2 Mugs

Viazi - 3

Nyama ya Kusaga - 1 Pound

Mboga mcha... Read More

Jinsi ya kupika Biskuti Za Kopa Za Kunyunyuziwa Sukari Za Rangi

Jinsi ya kupika Biskuti Za Kopa Za Kunyunyuziwa Sukari Za Rangi

MAHITAJI

Unga vikombe 2 ΒΌ

Siagi 250g

Sukari kukaribia kikombe Β½ (au takriba... Read More

Mapishi mazuri ya Wali Wa Kukaanga Kwa Kidari Cha Kuku

Mapishi mazuri ya Wali Wa Kukaanga Kwa Kidari Cha Kuku

Vipimo vya Wali:

Mchele - 3 vikombe

*Maji ya kupikia - 5 vikombe

*Kidonge cha s... Read More

Mapishi ya Maini ya kuku

Mapishi ya Maini ya kuku

Mahitaji

Maini ya kuku 1/2 kilo
Vitunguu vikubwa 2
Hoho 1
Pilipil 1
L... Read More

Jinsi ya Kupika skonzi

Jinsi ya Kupika skonzi

Mahitaji

Unga wa ngano (self risen flour 2 vikombe vya chai)
Sukari (sugar 1/2 kijik... Read More

Mapishi ya Biriani Ya Kuku Wa Kuchoma (Grilled)

Mapishi ya Biriani Ya Kuku Wa Kuchoma (Grilled)

Mahitaji

Mchele wa Basmati /Pishori - 4 vikombe

Kuku

Vitunguu - 3

Nyany... Read More

Mapishi ya Dagaa wa nazi, nyanya chungu na bamia

Mapishi ya Dagaa wa nazi, nyanya chungu na bamia

Mahitaji

Dagaa waliokaushwa (dried anchovy 2 kikombe cha chai)
Bamia (okra 5)
N... Read More

Mapishi ya Maharage na spinach

Mapishi ya Maharage na spinach

Mahitaji

Maharage yaliyochemshwa kiasi
Spinach zilizokatwa kiasi
Vitunguu maji ... Read More

Mapishi ya Viazi, samaki na asparagus

Mapishi ya Viazi, samaki na asparagus

Mahitaji

Viazi (potato 1/2 kilo)
Samaki (fish 2)
Asparagus 8
Kitunguu kili... Read More

Mapishi ya Pilau Ya Nyama Na Mtindi

Mapishi ya Pilau Ya Nyama Na Mtindi

MAHITAJI

Nyama iliyokatwa vipande - 1 Ratili(LB)

Mchele Basmati - 2 Magi

Chum... Read More

Mapishi ya chipsi

Mapishi ya chipsi

Mahitaji

Viazi (potato) 1/2 kilo
Mafuta ya kukaangia (veg oil)
Chumvi

Ma... Read More

Mapishi ya Bokoboko La Kuku

Mapishi ya Bokoboko La Kuku

Mahitaji

Ngano nzima (shayiri) - 3 Vikombe

Kuku - Β½ (3 LB takriban)

Thomu na... Read More