Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

SALA KWA MT. YOSEFU KWA WASIO NA AJIRA WAPATE AJIRA

Featured Image

Ee Mt. Yosefu, tunakuomba kwa ajili ya wale asio na ajira, kwa ajili ya wale wanaotaka kujipatia kipato chao na kulisha familia zao.
Wewe u Msimamizi wa wafanyakazi, tujalie kwamba pasiwepo kati yetu mtu asiye na ajira, na kwamba wale wote ambao wako tayari kufanya kazi waweze kuelekeza nguvu zao na uwezo wao katika kuwatumikia wanadamu wenzao na kujipatia kipato halali.


Wewe u Msimamizi wa familia, usiwaache wale wenye watoto wa kuwatunza na kuwalea wakose namna ya kufanya hivyo. Uwahurumie ndugu zetu waliokosa ajira na kugubikwa na umasikini kwa sababu ya magonjwa au mipango mibaya ya kijamii. Wasaidie viongozi wetu wa kisiasa na walioshika usukani katika nyanja mbalimbali za kiuzalishaji wavumbue suluhu mpya na za haki za jambo hili. Utujalie ili kila mmoja wetu apate kujipatia kipato halali na kufurahia fursa ya kushiriki kadri ya uwezo wake, katika maisha bora zaidi kwa wote. Utujalie ili wote tushiriki pamoja katika raslimali alizotujalia Mungu, na pia utujalie tuwe tayari daima kuwasaidia wale walio wahitaji kuliko sisi.
Amina.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Elijah Mutua (Guest) on February 4, 2017

Neema ya Mungu inatosha kwako

Ruth Mtangi (Guest) on January 8, 2017

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Nancy Akumu (Guest) on December 20, 2016

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Agnes Njeri (Guest) on December 9, 2016

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Alice Jebet (Guest) on November 11, 2016

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Dorothy Nkya (Guest) on October 14, 2016

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Agnes Lowassa (Guest) on September 12, 2016

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Muslima (Guest) on July 14, 2016

πŸ™πŸ™πŸ™

Janet Mbithe (Guest) on July 11, 2016

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Hellen Nduta (Guest) on May 21, 2016

πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose

Jackson Makori (Guest) on April 24, 2016

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Dorothy Mwakalindile (Guest) on March 18, 2016

Neema na amani iwe nawe.

Francis Njeru (Guest) on February 14, 2016

πŸ™β€οΈ Mungu akubariki

Christopher Oloo (Guest) on January 25, 2016

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

Andrew Mchome (Guest) on November 16, 2015

Mwamini Bwana; anajua njia

Ann Awino (Guest) on September 30, 2015

πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu

David Musyoka (Guest) on September 2, 2015

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Carol Nyakio (Guest) on July 6, 2015

πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha

Isaac Kiptoo (Guest) on July 5, 2015

Rehema hushinda hukumu

Rose Waithera (Guest) on June 23, 2015

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Robert Ndunguru (Guest) on June 12, 2015

Tumaini ni nanga ya roho

Emily Chepngeno (Guest) on June 4, 2015

Sifa kwa Bwana!

Edwin Ndambuki (Guest) on April 28, 2015

Imani inaweza kusogeza milima

Related Posts

SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI

SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI

Mama Mtakatifu, Mama wa Mungu na Malkia wa Mashahidi, leo nakuchagua Wewe uwe mfano wangu, mkinga... Read More

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

Ee Yesu Mfungwa wa Upendo wa Mungu,/ ninapofikiri Upendo wako na jinsi ulivyojitolea kwa ajili ya... Read More

AMRI ZA KANISA

AMRI ZA KANISA

1. HUDHURIA MISA TAKATIFU DOMINIKA NA SIKUKUU ZILZOAMRIWA

2. FUNGA SIKU YA JUMATANO YA MAJI... Read More

ATUKUZWE BABA

ATUKUZWE BABA

Atukuzwe Baba
na Mwana
na Roho Mtakatifu
Kama mwanzo
na sasa,
na siku zo... Read More

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU II

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU II

Yesu, Mungu wangu mpenzi,/ upo hapa katika Altare mbele yangu;/ na mimi napiga magoti mbele yako.... Read More

ROSARI YA BIKIRA MARIA MAMA WA MSAADA WA DAIMA

ROSARI YA BIKIRA MARIA MAMA WA MSAADA WA DAIMA

Namna ya kusali Rozari kwa Bikira Maria Mama wa Msaada wa Daima

(Tumia rosari ya kawaida... Read More

SALA YA UHAI KWA MT. YOSEFU

SALA YA UHAI KWA MT. YOSEFU

(Sala hii inafaa sana kwa ajili ya kutetea uhai wa watoto wachanga wakiwa tumboni mwa mama za... Read More

SALA KWA MALAIKA WAKO MLINZI

SALA KWA MALAIKA WAKO MLINZI

Malaika wa Mungu Mlinzi wangu mpenzi,
Ambaye upendo wake unanifanya niwepo hapa,
Uwe na... Read More

ROZARI YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

ROZARI YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Tumia tasbihi ya kawaida yenye chembe ndogo 53.

Kwenye Msalaba Sali:

... Read More
SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu, utulinde katika vita, uwe kinga yetu katika maovu na maoteo ya sh... Read More

Sala za kuheshimu Damu Takatifu ya Yesu

Sala za kuheshimu Damu Takatifu ya Yesu

Tusali kila siku sala hizi, angalau kwa mwezi wa saba (Julai) kila mwaka, mwezi wa kuhesh... Read More

Malkia wa Mbingu

Malkia wa Mbingu

Malkia wa mbingu, furahi, aleluya. Kwani uliyestahili kumchukua, Aleluya. Amefufuka alivyosema, A... Read More