Inawezekana msichana akapata mimba kabla ya kuvunja ungo?
Updated at: 2024-05-25 16:23:55 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Msichana anaweza kupata mimba kabla ya kuvunja ungo, yaani kabla ya kuona hedhi kwa mara ya kwanza. Kwa uhakika utajiuliza kwa nini. Kabla ya kuona hedhi, yai ndani ya kokwa linapevuka na kusafiri kutoka kwenye kokwa mpaka tumbo la uzazi. Hedhi yenyewe ni dalili kwamba lile yai pevu halikurutubishwa na kwa hiyo linatoka pamoja na utando wa tumbo la uzazi kupitia ukeni. Kuna maana kwamba hata kama msichana hajavunja ungo, i inawezekana kwamba ndani ya tumbo lake yai limeshaanza kupevuka. Lile yai linaweza kurutubishwa na msichana anaweza kupata mimba, hata kama hajaona hedhi yake kwa mara ya kwanza.
Updated at: 2024-05-25 16:24:05 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Haki za binadamu ni haki zinazohusiana na mambo ya msingi na
asili ya uhuru na heshima ya ubinadamu ambapo watu wote wamepewa
haki ya kupata heshima kama
binadamu. Mara mtu azaliwapo
mume au mke hupata
haki hizi. Haki hizi
zinatambuliwa kimataifa
na zina usawa kwa watu
wote. Nchi mbalimbali
zimetia saini na kuidhinisha
haki hizi za kimataifa
na kufanya ni sehemu
ya sheria zao
pamoja na kuweka sera
zinazolinda haki hizi.
Haki za uzazi zina misingi yake katika haki za binadamu na pia
zinahusiana na haki za mtu mmojammoja.
Kupata habari juu ya ujinsia na mada zinazohusu afya
ya uzazi.
Mwanamke au mwanaume kuamua kwa uhuru na
kuwajibika, kama unataka kujamiaana lini na nani.
Uhuru wa maamuzi.
Kuamua kwa hiari na kuwajibika juu ya idadi na muda wa
kupishana katika kupata watoto.
Kupata huduma za afya ya uzazi kwa urahisi.
Haki za kufanya maamuzi kuhusu afya ya uzazi, kwa
uhuru, bila kunyanyaswa, kulazimishwa, bila kutumia
nguvu pamoja na maamuzi nani wa kufunga naye ndoa.
Kujilinda kutokana na mila zenye madhara kama vile
ukeketaji wa wanawake.
Haki hizi zimerekebishwa tangu mkutano uliofanyika Cairo mwaka
19941.
Je, ni madhara gani atapata mama mjamzito endapo atajamiiana na mwenzi wake?
Updated at: 2024-05-25 16:22:24 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kama kati ya mwanamke na mwanaume hakuna mwenye magonjwa ya zinaa, hakuna madhara yoyote kwa mwanamke mwenye mimba kujamii ana na mwenzi wake. Mfuko wa mimba hufunga kabisa na kifuko kinamzunguka mtoto vizuri, na hivyo hakuna uwezekano wowote wa mbegu za kiume kupenya na kumfikia mtoto. Inashauriwa lakini wakati wa kujamii ana na mwanamke mjamzito tumbo lisigandamizwe sana. Wanawake wengine hawana hamu kubwa ya kujamii ana hasa mwishoni mwa ujauzito, na mwanaume anashauriwa kuheshimu hisia hizi za mwanamke. Kama mwanaume atakuwa ameambukizwa magonjwa ya zinaa wakati wa kujamii ana, hii i ii inaweza kuwa hatari sana kwa mwanamke na pia kwa mtoto tumboni. Wakijamii ana mume na mke wakati wa ujauzito, lazima wawe na uhakika kwamba hamna mwenye magonjwa ya zinaa au watumie kondomu kwa ajili ya kinga. Iwapo watakuwa na wasiwasi wowote, wamwone daktari kwa uchunguzi.
Updated at: 2024-05-25 16:24:03 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kuna aina nyingi za unyanyasaji wa jinsia na unaweza kutokea
kwa wote wanaume na wanawake. Kwa kawaida unajulikana
kama matumizi ya makusudi ya kutumia nguvu na uwezo na
kutishia au kwa hali halisi kinyume cha mtu au kikundi au
jamii ambapo matokeo yake yanaweza kuleta jeraha au kifo,
kuumia kisaikilojia, kutokukua au kudumaa.7 Chini ya sheria za
Tanzania8 unyanyasaji wa kijinsia ni pamoja na maneno, sauti
ishara au maonyesho ya sehemu za mwili kwa makusudi kinyume
na matakwa ya mtu.
Hakuna mtu anayeruhusiwa kujamiiana nawe bila ya ridhaa yako,
maana hii itakuwa ni ubakaji. Kumlazimisha mtu kujamiiana nawe kwa
kubadilishana na zawadi au kumpa kazi ni unyanyasaji wa kijinsia.
Kadhalika hakuna mtu anayeruhusiwa kushika viungo vya siri vya
uzazi, au kukupiga busu bila ya ridhaa yako. Tendo la ukeketaji ni
aina nyingine ya ukatili wa kijinsia.
Aina nyingine za unyanyasaji wa kijinsia ni pamoja na kumwita
mtu majina, kumlazimisha mtu kuvua nguo mbele za watu au
kumlazimisha mtu kujamiiana na mtu mwingine. Fikiria kwamba
unyanyasaji wa kijinsia ni tendo baya kwa haki za binadamu
na unasababisha maumivu kwa wahusika. Tukumbuke kwamba
uhusiano wa kimapenzi na watu waliokaribu nasi kwa mfano baba,
mama, kaka, dada, babu au bibi ni aina nyingine ya unyanyasaji
wa jinsia. Inajulikana kama kujamiiana kwa maharimu “incest“
na inakatazwa kisheria.
Updated at: 2024-05-25 16:22:06 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Uhusiano mzuri na wazazi ni muhimu sana siyo katika masuala ya uchaguzi wa mchumba tu, bali katika masuala yote ya msingi maishani. Kwa hiyo, hatua ya kwanza ni kujaribu kuelewana nao.
Mara nyingi vijana hufikiri wazazi hawaelewi maisha ya vijana wa kisasa. Mara nyingine hufikiri kwamba mila na desturi zinamzuia kijana kufanya uamuzi ambao unafaa. Pia wengine hufikiri kwamba tofauti ya malengo kati ya vijana na wazazi huleta mgongano.
Hali kama hii ikijitokeza, ni vizuri kuwasiliana na wazazi kwa nia ya kuelewana. Usisahau kwamba wazazi wakati wote wanajaribu kujena maisha bora ya baadaye ya watoto wao. Unapowasiliana na wazazi jaribu kuwaeleza kwa heshima na upole kwa nini hukubaliani na mawazo yao na kwa nini unaona uamuzi wako unafaa. Inawezekana kwa kufanya hivi unaweza kupata ridhaa ya wazazi wako.
Kama hujawahi kuzungumza na wazazi wako kwa karibu, mara nyingi i i inakuwa vigumu kuanzisha mazungumzo. Jaribu kuanza kwa mazungumzo rahisi. Tafuta muda mzuri wa kuanzisha mazungumzo. Usianzishe mazungumzo na wazazi wakati wamechoka au wakati wametingwa na kazi nyingi; hawatakusikiliza. Jaribu kuwa wazi na mkweli, na waonyeshe wazazi wako kwamba unayajali mawazo yao. Kwa kufanya hivyo wazazi wako wanaweza kukuamini na kuafikiana na wewe katika maswali mazito zaidi. Vilevile onyesha kwamba unawaheshimu. Inachukua muda mrefu kufanikisha mawasiliano mazuri na wazazi, lakini ni vema kuyaanzisha mapema kwa ajili ya kufanikisha lengo la mawasiliano mazuri na wazazi.
Updated at: 2024-05-25 16:24:12 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Albino ni binadamu kama alivyo binadamu mwingine na ana haki sawa za kuishi na kufaidi kuwepo kwake hapa duniani kama ilivyo kwa binadamu wengine. Kuua Albino kwa sababu yoyote ile ni jambo baya sana ambalo linakemewa na serikali, dini zote, na kila mwanadamu mwenye akili timamu na maadili ya utu na watetea haki za binadamu. Kitendo hiki vilevile kinapingana na haki za binadamu kwa hiyo wavunjaji wa haki hizi wanashtakiwa kisheria.
Je, kuna matatizo yoyote kama mdomo wa msichana utagusana na shahawa?
Updated at: 2024-05-25 16:22:08 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kama mpenzi wako hatakuwa na maambukizi ya magonjwa ya zinaa hakuna madhara ya kiafya. kama shahawa i itagusana na mdomo wa msichana. Lakini, wasichana wengi hawapendi kupokea shahawa mdomoni na wanasikia kukerwa kufanya hivyo.
Wapenzi wajadiliane kati yao na kuamua kama tendo la kumwaga mbegu mdomoni wanalipenda au hawalipendi. Huu ni msingi mmojawapo wa kuonyesha kujaliana.
Hata hivyo, kama mwanaume ameambukizwa na magonjwa ya zinaa ni rahisi sana kwa mwanamke kuambukizwa magonjwa hayo wakati anapokea majimaji na shahawa mdomoni. Kwa hiyo, kutumia kondomu katika mtindo huu ni salama zaidi.
Madhara yanayotokea kwa unyanyasaji wa jinsia kwa mtu
Updated at: 2024-05-25 16:24:00 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Unyanyasaji wa ujinsia una matatizo mabaya ya kimwili na yanayochukua muda mrefu kwa mwathiriwa kupona. Unyanyasaji wa jinsia mara nyingi humuumiza mwathiriwa, matendo ya ubakaji, majaribio ya ubakaji, unyanyasaji wa kijinsia kwa mtoto, na ukeketaji kwa wanawake yanamhusu moja kwa moja mwili wa mwathiriwa. Mwathiriwa anaweza kupata maumivu makali wakati wa kitendo, viungo vyake vya uzazi akiwa mwanamume au mwanamke kuna uwezekano ukapata majeraha wakati wa ubakaji. Zaidi ya hayo mbakaji anaweza kumuumiza mwathiriwa katika sehemu nyingie za mwili. Na jambo baya zaidi ukatili wa kijinsia wakati mwingine unaweza kusababisha ulemavu wa maisha na mara nyingine hata kifo cha mwathiriwa. Ubakaji unaweza kusababisha mimba, na uenezaji wa magonjwa hatari kama Virusi vya Ukimwi. Watoto wanadhuriwa zaidi na vitendo vya ukatili wa ujinsia katika miili yao kwa sababu ukubwa wa viungo vyao vya sehemu za siri ni vidogo kuliko vile vya watu wazima. Athari za kisaikolojia kwa mwathiriwa pia ni hatari sana. Uonevu wa ujinsia kwa mwathirika unaweza kusababisha kuchanganyikiwa na kupata kiwewe na hali ya hatari sana inayoweza kusababisha mtu akapata kichaa katika miezi ya kwanza. Baada ya uonevu wa ujinsia na hata baada ya miaka, mwathiriwa bado atakuwa na kumbukumbu ya maumivu aliyopata na hivyo kukumbuka katika akili yake. Waathiriwa wengi wa ubakaji wana matatizo ya kutokuwa na uhusiano mzuri wa kujamiiana, kwani kila mara atahusisha kujamiiana na alipobakwa. Ndiyo maana waathiriwa wa ubakaji wanahitaji msaada, uelewa na uvumilivu toka kwa wazazi wao, wenzi wao na marafiki.
Je, nikila na mtu mwenye Virusi vya UKIMWI, nitaambukizwa na virusi vya UKIMWI na UKIMWI?
Updated at: 2024-05-25 16:22:28 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Hapana, ukila na mtu mwenyemaambukizi ya Virusi vya UKIMWI huwezi kuambukizwa Virusi vya UKIMWI wala UKIMWI, isipokuwa pale ambapo wote wawili mna vidonda mdomoni na mnachangia kijiko kimoja. Lakini uwezekano huu ni mdogo sana, kiasi tunachoweza kusema kwamba huwezi kuambukizwa Virusi vya UKIMWI na UKIMWI ukila sahani moja na mtu aliyeambukizwa na virusi. Lakini, kufuatana na kanuni za afya, ni vizuri zaidi kila mtu atumie vifaa vyake na baada ya kuvitumia avioshe kikamilifu.
Updated at: 2024-05-25 16:22:05 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Lengo kuu la kujamiiana ni kutafuta watoto. Lakini si sababu pekee. Sababu hizo ni pamoja na;
kupata starehe,
kujiburudisha,
kupoteza mawazo,
kujenga na kudumisha uhusiano na hisia za kupendana,
kuhitajiana,
Hata hivyo ni muhimu sana kuzingatia uzazi wa mpango. Ili kuleta raha katika tendo la kujamiiana na kuzuia mimba isiyotakiwa na kuzaa mtoto ambaye mtashindwa kumlea ni lazima kutumia uzazi wa mpango.
Tumia njia za kupanga uzazi kama hamtaki kupata mimba! Au kwa usalama zaidi tumia kondomu ambayo ni kinga ya mimba na maambukizi mengine yanayosababishwa na ngono.