Jifunze kujikagua, jifunze kujiuliza je hapa ndipo napotakiwa kuwa? Usifurahie tu kwamba upo hapo kwa muda mrefu yamkini unaona panakufaa and you are settled lakini ukweli ni kwamba sio pako na haukutengenezwa kuwa hapo. Hata kama tai ataonekana kwenye banda la kuku lakini ukweli ni kwamba tai kaumbiwa kuwa angani tofauti na kuku aishie bandani. Jiulize hapo ulipo ni pako??
Updated at: 2024-05-23 16:07:18 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Jifunze kujikagua, jifunze kujiuliza je hapa ndipo napotakiwa kuwa? Usifurahie tu kwamba upo hapo kwa muda mrefu yamkini unaona panakufaa and you are settled lakini ukweli ni kwamba sio pako na haukutengenezwa kuwa hapo. Hata kama tai ataonekana kwenye banda la kuku lakini ukweli ni kwamba tai kaumbiwa kuwa angani tofauti na kuku aishie bandani. Jiulize hapo ulipo ni pako??
Na ndio maana kwenye maisha, mafanikio ya leo ni matokeo ya tulichojifunza kutoka kwa waliopita, baada ya wao kukosea mahali nasi tukaboresha, na kwa hakika vizazi vijavyo navyo vitaendelea kurekebisha pale tunapokosea sisi na hii yote ndiyo huleta ladha ya maisha. Ukipitia Changamoto mwenyewe na ukapambana kujikwamua mwenyewe, utapata somo litakalokufunza zaidi kuliko kusimuliwa changamoto walizopiti wengine.
Maisha ni Maamuzi, aliyekula Sahani mbili za wali mchana ili usiku asile tena, anaweza kuwa sawa na aliyeamua kutokula Mchana ili usiku ale sahani mbili za wali, japo hawa hawawezi kuwa sawa sawia na aliyeamua kula sahani moja ya wali mchana na moja ya wali usiku, Ijapokua mwisho wa siku wote wamekula sahani Mbili za wali kwa siku. Jumapili Njema kwenu nyote.
Kukosa hela sio tatizo bali ndio kigezo ya kutafuta hela
Ukimonyesha mtu fursa akakwambia hana hela mwambie hiyo ndio sababu ya wewe kumonyesha fursa ili awe na hela tukumbuke kuwa hela haitokani na helahela inatokana na fursa
Updated at: 2024-05-23 16:07:19 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Ukimonyesha mtu fursa akakwambia hana hela mwambie hiyo ndio sababu ya wewe kumonyesha fursa ili awe na hela tukumbuke kuwa hela haitokani na helahela inatokana na fursa
Nijukumu la mtu asiye na hela kutafuta njia ya kuwa na hela watu wengi tunachelewa kufanikiwa kwa kutojua majukumu yetu ili kupambana na UMASIKINI mwombe Mwenyezi MUNGU kwa imani yako akufungue akili…
Kuna tofauti kubwa sana kati ya mtu anayejenga GHOROFA na yule anayejenga Nyumba ya KAWAIDA.
Anayejenga Ghorofa anatakiwa achimbe msingi Mrefu kwenda chini kabla hajaanza kuinua Ghorofa yake juu. Hivyo wakati huyu mwingine anapokuwa anajenga Nyumba ya kawaida atakapokuwa tayari anakaribia hata kuezeka, unaweza kukuta yule anayejenga Ghorofa bado yuko kwenye Msingi. Ila siku akianza kuinua Ghorofa lake, kila mtu atashangaa urefu wa juu atakaoenda nao.
Updated at: 2024-05-23 16:07:17 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kuna tofauti kubwa sana kati ya mtu anayejenga GHOROFA na yule anayejenga Nyumba ya KAWAIDA.
Anayejenga Ghorofa anatakiwa achimbe msingi Mrefu kwenda chini kabla hajaanza kuinua Ghorofa yake juu. Hivyo wakati huyu mwingine anapokuwa anajenga Nyumba ya kawaida atakapokuwa tayari anakaribia hata kuezeka, unaweza kukuta yule anayejenga Ghorofa bado yuko kwenye Msingi. Ila siku akianza kuinua Ghorofa lake, kila mtu atashangaa urefu wa juu atakaoenda nao.
Kwenye maisha ndivyo ilivyo- "If want to go so high, you need to go so deep" (Kama unataka kwenda juu sana ni lazima ukubali kwenda chini sana). Ni lazima ufanye kitu cha tofauti kitakochokujengea Future imara.
Ukweli ni kuwa Watu wengi wanaokuzunguka wanajenga maisha ambayo ni kama Nyumba ya kawaida. Na wewe kama unataka kujenga maisha yanayofanana na Ghorofa, Ni lazima ukubali kuonekana unachelewa kwenye baadhi ya mambo.
Hii inamaanisha nini?… Hii inamaanisha kuwa utalazimika kufanya vitu vya TOFAUTI na kuwa TAYARI kusubiri. Utatakiwa Kuwekeza wakati wengine wanaenda kununua nguo mpya waendane na Fashion, Utatakiwa Kusoma vitabu wakati wengine wanaangalia movie na kupiga stories, Utatakiwa Uanzishe Biashara yako wakati wenzako wamesharidhika na mshahara wanaopata n.k
Unachofanya kuanzia unapoamka hadi unapoenda kulala kitajulisha kama unajenga Maisha GHOROFA ama Maisha KAWAIDA.
Ukijiona unapoteza muda hovyo, ukiingia Facebook/instagram ni kusoma umbea tu, Unalalamika unasema utafanya na hakuna unachofanya, ujue unajenga Maisha ya KAWAIDA tena ni kama Nyumba ya UDONGO.
Ukitaka kujenga maisha GHOROFA; 1. _Jifunze kitu kipya leo._ 2. _Chukua hatua kuelekea Ndoto yako._ 3. _Usiwe mtu wa kulalamika bali tafuta suluhisho kwa kila changamoto._
Je, LEO utajiunga na wanaojenga Maisha GHOROFA ama wale wanaojenga Maisha ya KAWAIDA?
FURSA HAIJI MARA MBILI: Jinsi unavyoweza kupata faida au hasara ukitumia Nafasi au fursa uliyonayo
Kwenye maisha fursa moja tu inatosha kabisa kubadilisha hali yako ya sasa na kukuweka kwenye kiwango kingine kabisa cha mafanikio.Kuna watu wengi sana ambao waliwahi kufikiria kuwa maisha yao yatachukua miaka mingi sana kabla hayajabadilika na kwa mshangao wao walipoanza kufanya vitu sahihi wakakutana na mabadiliko makubwa sana katika maisha yao kwa kupitia fursa moja tu.
Updated at: 2024-05-23 16:07:29 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kwenye maisha fursa moja tu inatosha kabisa kubadilisha hali yako ya sasa na kukuweka kwenye kiwango kingine kabisa cha mafanikio.Kuna watu wengi sana ambao waliwahi kufikiria kuwa maisha yao yatachukua miaka mingi sana kabla hayajabadilika na kwa mshangao wao walipoanza kufanya vitu sahihi wakakutana na mabadiliko makubwa sana katika maisha yao kwa kupitia fursa moja tu.
Kufanikiwa kwenye maisha ni matokeo ya kujua mambo sahihi ya kuyafanya.Ni kama ilivyo wakati unapotaka kufungua mlango uliofungwa,unachohitaji ni ufunguo sahihi wa kutumia na sio vinginevyo. Ili ufanikiwe lazima uwe mtu mwenye bidii na ambaye unawathamini watu bila kujali hali zao za sasa.Ili kutoka hapo ulipo na kwenda kule unakotaka unahitaji watu wa kukuunganisha na fursa mpya,kukuonyesha njia nzuri ya kufanya mambo,wa kukurekebisha na watu ambao unaweza kujifunza kwao.
Kuna baadhi ya LEVEL huwezi kufika…Kuna MAFANIKIO huwezi kuyafikia…Kuna HELA huwezi kuzipata…Kama umezungukwa na watu BASIC… Kuanzia asubuhi mpaka jioni wanaongelea WATU TU..Fulani kamegwa na yule..halafu yule naniliu saivi anatembea na yule ex wa nanii…Asubuhi mpaka jioni DISCUSSING PEOPLE…Hawa ndio watu BASIC…Hata siku 1 hawatakupa Ushauri kuhusu HOW TO REACH SOMEWHERE…NEVER
Updated at: 2024-05-23 16:07:23 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kuna baadhi ya LEVEL huwezi kufika…Kuna MAFANIKIO huwezi kuyafikia…Kuna HELA huwezi kuzipata…Kama umezungukwa na watu BASIC… Kuanzia asubuhi mpaka jioni wanaongelea WATU TU..Fulani kamegwa na yule..halafu yule naniliu saivi anatembea na yule ex wa nanii…Asubuhi mpaka jioni DISCUSSING PEOPLE…Hawa ndio watu BASIC…Hata siku 1 hawatakupa Ushauri kuhusu HOW TO REACH SOMEWHERE…NEVER
Na ukionekana unaanza kufanya vitu EPIC watakugeuka kwamba UNARINGA.. UNAJISIKIA.. UMEWATENGA…UNAJIDAI UNA HELA…and lots of bullshit… Pengine ulipaswa kuwa mbaaalii kibiashara lakini HUWEZI coz umezungukwa n Mbaazi tupu…BASIC PEOPLE…Ukiwaambia umesikia Kiwanja kinauzwa Kigamboni wanakwambia Kigamboni watu wanatapeliwa kuna mradi wa Joji Bushi…Ukiwambia unataka kujiunga Forever Living wanakwambia UNALIWA HELA…Ukiwaambia kuna SACCOSS wanatoa mikopo unataka uchukue ujenge wanakwambia INTEREST ZAKE UTASHINDWA na kujenga sio mchezo shosti..Unaamini unaacha!…Nataka kufanya Kitu flani WANAKUKATISHA TAMAA Unahitaji kuzungukwa na watu wenye POSITIVE ENERGY ambao ukiwambia unataka kwenda Mbinguni kwa kupitia Mkuranga wanakuchangia Nauli…Niliposema naacha kazi watu ohh utakula nini..utaishije…Mji Mgumu huu..Wenzio wanatafuta kazi we unaacha utalosti…WHO SAID??Nadunda kama kawa..NEGATIVE PEOPLE WILL BRING U DOWN….Ukitaka Kupaa kaa karibu na ndege…We unataka kupaa unakuwa rafiki wa Nyangumi…UNAZAMISHWA SASA HIVI!! Tangu nianze kukaa na watu Positive I have changed a lot…Nikiwaza jambo wanauliza HOW DO WE ACHIEVE THIS na sio FULANI ALIWAHIFANYA HII AKAFELI.. Ikikusaidia Chukua.. KILL ALL NEGATIVE PEOPLE AROUND YOU kama unataka kufikia Malengo Makubwa, I will be ur Lawyer at the Court na mwambie Hakimu nilikutuma mimi! TIME TO DELETE ALL BASIC PEOPLE who wait of option😜😜😉😉
Kauli 10 za mtu ambaye unatakiwa umuepuke maishani
Kauli 10 za mtu asiye na malengo wala uthubutu 1)Sina mtaji 2)Sina Connection 3)Nitaanza rasmi kesho 4)Mimi ni wa hivihivi tu
Updated at: 2024-05-23 16:06:59 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kauli 10 za mtu asiye na malengo wala uthubutu 1)Sina mtaji 2)Sina Connection 3)Nitaanza rasmi kesho 4)Mimi ni wa hivihivi tu
5)Mifumo mibovu ya Serikali ndiyo inayonirudisha nyuma 6) Mke/mme/ndugu zangu Ndiyo walioniangusha/kunitenda/kikwazo 7)Kupata ni majaliwa 8)Usilazimishe mambo 9)Kuna watu special siyo mimi. 10)Sina bahati
KAA MBALI NA HUYO MTU. NI HATARI KWA NDOTO ZAKO!!!!
Hakuna mtu duniani ambaye hajawahi kukutana na hali ya kukataliwa. Yaani kukataliwa katika hali yoyote ile. Waweza kuwa umekataliwa katika kupata ajira, umekataliwa katika mahusiano, umekataliwa kupata nafasi ya kusoma, umekataliwa kupata mtaji wa biashara, umekataliwa tuu..umekataliwa.
Updated at: 2024-05-23 16:07:06 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Hakuna mtu duniani ambaye hajawahi kukutana na hali ya kukataliwa. Yaani kukataliwa katika hali yoyote ile. Waweza kuwa umekataliwa katika kupata ajira, umekataliwa katika mahusiano, umekataliwa kupata nafasi ya kusoma, umekataliwa kupata mtaji wa biashara, umekataliwa tuu..umekataliwa.
—-= Unaweza kuwa umekataliwa katika ajira moja kumbe kuna ajira nyingine tena yenye maslahi zaidi inakusubiri.
—-= Umekataliwa na mteja mmoja na kumbe kuna wateja wengi wanakusubiri.
—-= Umekataliwa katika chuo kimoja mwaka huu kumbe mwakani kuna nafasi yako inakusubiri.
——= Umekataliwa na mpenzi ulioamini kabisa atakua wako wa maisha kumbe aliye wako haswaa anakusubiri ufike.
Watu wengi kinachowarudisha nyuma, "ni kuacha kuboresha fikra zao ili kuwa watatuzi wa matatizo_(problem solvers)_ ila wameamua kuwa walalamikaji tu kila siku, ili tuendelee ni lazima tujikite katika kutafuta majibu ya matatizo yanayotuzunguka." Yaani, mara zote jiulize " *sasa nifanye nini? Na sio kwa nini mimi?"*
Mtaalamu mmoja aliwahi kusema " _Life is 10% of what happens to you and 90% of how you respond to it_". Yaani _yale yanayokutokea maishani yanachangia asilimia kumi tu kuboresha au kuharibu maisha yako na asilimia 90 ya maisha yako ni jinsi wewe unavyoyachukulia maisha hayo_. Kwa nini ukate tamaa baada ya kukataliwa. Yape maisha yako maana sana thamani ya juu kabisa ili kukataliwa kwako iwe ni kukupa nguvu ya kufanya vizuri zaidi. Tambua utakacho na unachoweza kukifanya. Jifunze vizuri na ubobee ili kuuhakikishia ulimwengu kwamba wewe sio mzigo ila ni sehemu ya wenye majibu ya matatizo yanayotuzunguka.
Kukataliwa, ni mtaji. Kila jambo lina wakati wake.
Hii ndio sababu kwa nini huwezi kufanikiwa kibiashara
HUWEZI KUFANIKIWA KIBIASHARA KAMA UNAPENDA KUJIHURUMIA HURUMIA! 💥Mama mmoja Mzungu alitembelea mlima Kilimanjaro miaka iliyopita. Alikuwa amepanga kupanda mlima Kilimanjaro mpaka kileleni, yaani Kibo na Mawenzi, ili hatimaye apewe cheti cha kupanda mlima mrefu Afrika.
Updated at: 2024-05-23 16:07:12 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
HUWEZI KUFANIKIWA KIBIASHARA KAMA UNAPENDA KUJIHURUMIA HURUMIA! 💥Mama mmoja Mzungu alitembelea mlima Kilimanjaro miaka iliyopita. Alikuwa amepanga kupanda mlima Kilimanjaro mpaka kileleni, yaani Kibo na Mawenzi, ili hatimaye apewe cheti cha kupanda mlima mrefu Afrika.
💥Lakini kwa bahati mbaya akiwa amefika katikati ya mlima alizidiwa kiafya na hatimaye akashushwa mlimani akiwa amezirai hadi hospitalini.
💥Siku ya tatu alipozinduka hospitalini huku marafiki zake wakimpa pole, aliwajibu kuwa “Mlima Kilimanjaro hauwezi kuongezeka urefu, lakini mimi mwanadamu nina uwezo wa kuongeza maarifa, nguvu na mbinu za kupanda milima wowote duniani. Kwa hiyo nitarudi tena wakati mwingine mpaka nipande mlima Kilimanjaro hadi kileleni, ingawa nimepata changamoto wakati huu.”.
💥Alivyorudi kwao Marekani, alianza kufanya mazoezi tena ya kukimbia na kupanda vichuguu na vilima kwa muda wa mwaka mzima, na kisha mwaka uliofuata alirudi tena Tanzania, akapanda mlima Kilimanjaro mpaka kilele cha Kibo na mawenzi, na hatimaye akapewa cheti cha kupanda mlima Kilimanjaro!.
💥Je huyo mzungu angeamua kusubiri mlima Kilimanjaro upungue urefu ndipo aje Tanzania kuupanda, jambo hilo lingewezekana?
💥Je unataka maisha yawe rahisi ndipo uyamudu? Je unataka viwanja vishuke bei ndiyo ujenge nyumba yako? Je unataka ada za shule ziwe chini ndipo usome? Je unataka gharama za hospitali ziwe chini ndipo utibiwe? Je unataka mahari iwe chini ndipo uoe? Je unataka vitabu vya mafunzo ya biashara viwe bei chee ndiyo ununue? Unataka mshahara wako uwe mkubwa ndipo ufanikiwe? Je unataka shetani auwawe ndiyo umche Mungu? Je unataka dunia irudi nyuma, ndipo uweze kuyamudu maisha? Je, unataka urudi tumboni mwa mama yako ili uwe unakula na kulala bure? Ebo!🙊
💥Kama nia yako ni kufanikiwa hutakiwi kujionea huruma, nenda kwa wakati na ujitoe hadi kieleweke.
Kila la kheri na pia nakutakia MAFANIKIO makubwa sana wewe na kizazi chako! Siri ya utajiri ni ubahil asikudang'anye mtu tumia hela ikuzoee hakuna aliyezaliw kuwa maskin!
Ili kutoka hapo ULIPO uweze kwenda HATUA inayofuata kuna SWALI muhimu sana unahitaji kujiuliza. Watu ambao huwa wanashindwa kupiga hatua katika maisha yao ni kwa sababu huwa wanajiuliza kinyume cha swali hili. Swali hili ndilo wanalojiuliza watu wote waliofanikiwa:
Swali: "Hivi kwa sasa nina nini ambacho naweza kuanza kukitumia kama mtaji wa kwanza kuanza kufanya ninachotaka"?
Updated at: 2024-05-23 16:07:18 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Ili kutoka hapo ULIPO uweze kwenda HATUA inayofuata kuna SWALI muhimu sana unahitaji kujiuliza. Watu ambao huwa wanashindwa kupiga hatua katika maisha yao ni kwa sababu huwa wanajiuliza kinyume cha swali hili. Swali hili ndilo wanalojiuliza watu wote waliofanikiwa:
Swali: "Hivi kwa sasa nina nini ambacho naweza kuanza kukitumia kama mtaji wa kwanza kuanza kufanya ninachotaka"?
Siku moja wakati nasoma biblia niliona Mungu alipotaka kumtumia Mussa kuokoa wana wa Israel akamuuliza-
“Una nini mkononi mwako”-
Mussa akajibu kwa kudharau alichonacho kuwa “Nina fimbo kavu tu ya kuchungia mifugo”.
Ndipo Mungu alianza kumuonyesha miujiza kutumia fimbo ambayo siku zote alikuwa nayo na kujidharau ndiyo ambayo ikatumika kwenda kuokoa wana wa Israel.
Watu wengi sana wanashindwa kuanza kwa sababu huwa wanajiuliza-
"Hivi ninakosa nini ili niweze kuanza" badala ya 'Hivi nina nini cha kuanzia'.
Cha kuanzia sio lazima iwe pesa-Inawezekana ni uwezo wa kufanya jambo fulani la kipekee,inawezekana ni mahusiano mazuri uliyonayo na watu fulani(mtandao wako),inawezekana ni uzoefu ulionao,inawezekana ni kipaji n.k Leo unapoanza siku yako naomba ijiulize-
“Nina nini mkononi mwangu ambacho naweza kutumia katika hatua ya kwanza”?.
Kumbuka hakuna mtu ambaye hana kitu kabisa-KITAFUTE HADI UKIPATE NA ANZA KUKITUMIA KUCHUKUA HATUA.
Share ili wengine wajifunze…..uwe na Jumatatu njema……..
MALIGHAFI ZINAZO HITAJIKA WAKATI WA UTENGENEZAJI WA MISHUMAA.
1. Paraffin Wax 2. Utambi 3. Mould ( Umbo ) 4. Stearine au mixture 5. Rangi 6. Jiko la mafuta ya taa au mkaa. 7. Sufuria. 8. Boric acid.
Updated at: 2024-05-23 16:07:00 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MALIGHAFI ZINAZO HITAJIKA WAKATI WA UTENGENEZAJI WA MISHUMAA.
1. Paraffin Wax 2. Utambi 3. Mould ( Umbo ) 4. Stearine au mixture 5. Rangi 6. Jiko la mafuta ya taa au mkaa. 7. Sufuria. 8. Boric acid.
VIDOKEZO MUHIMU :
1. Paraffin Wax :
Hii inatokana na nta na sega ya nyuki iliyo changanywa na mafuta ya taa. Ina rangi nyeupe na katika utengenezaji wa mishumaa ina ubora kuliko bee wax.
* Bee Wax : Inatokana na masega ya nyuki yaliyo changanywa na mafuta ya petroli na diesel na rangi yake ni ya njano.
2. STEARINE
Hii dawa maalumu inayo fanya mishumaa iungane ama ishikamane.
3. BORIC ACID :
Hii ni maalumu kwa ajili ya kuufanya utambi usiishe mapema na uwake bila kutoa moshi.
4. RANGI :
Rangi nzuri zinazo tumika katika utengenezaji mishumaa ni rangi za chakula na nyingi huwa ni za maji.
JINSI YA KUTENGENEZA
Andaa mould ( umbo lako ) utakalo litumia baada ya kuyeyusha ( paraffin wax ) na kuchanganya na michanganyo yote.
Kwa Mfano : ( Kipimo cha stearine )
1. Wax kilo moja - Stearine vijiko vinne vya chakula. 2. Wax nusu kilo - Stearine vijiko vinne vya chakula 3. Wax robo kilo - Stearine kijiko cha chakula.
Baada ya mould ( umbo ) kuwa tayari , chemsha wax mpaka iyeyuke na itoe kwenye vyombo ambavyo umetayarisha na usubiri ikauke ili uanze kutoa mishumaa.