Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
☰
AckyShine

Magonjwa ya zinaa na dalili zake

Featured Image
Kuna magonjwa mengi tofauti ya zinaa, lakini yale ambayo yameenea sana ni kisonono, kaswende, klamdia, kankroidi, utando mweupe , Virusi vya UKIMWI na UKIMWI. Shida kubwa ya magonjwa mengi ya zinaa ni kwamba dalili zake hazionekani kwa urahisi na kama yasipotibiwa kikamilifu yanaweza kuleta madhara makubwa. Maelezo kuhusu magonjwa ya zinaa yaliyoenea sana ni kama yafuatayo:

Kisonono:


Huchukua muda wa siku 1 hadi 14 tangu kuambukizwa mpaka kuonyesha dalili za kuumwa. Kwa wanawake dalili za kisonono ni maumivu chini ya tumbo ambayo yanaweza kuambatana na homa na kutokwa uchafu ukeni. Wapo wanawake wengine ambao hawaoni dalili zozote. Kwa wanaume dalili ni kutokwa na usaha uumeni na kupata maumivu wakati wa kukojoa. Athari yake kwa mwanamke ni kuziba mirija ya kupitisha mayai na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi, na vilevile ugumba. Kwa mtoto aliye tumboni mwa mama mjamzito kisonono cha mama yake kinaweza kusababisha upofu. Kwa mwanaume athari yake ni kuziba mirija ya kupitisha mkojo.
The ListPages module does not work recursively.

Kaswende:


Dalili ya kaswende kwa mwanamke ni vidonda sehemu za siri hasa kwenye mashavu ya uke na sehemu ya njia ya haja kubwa, pamoja na sundosundo sehemu ya siri. Kwa mwanaume dalili ni vidonda. Mara nyingi kimoja kwenye kichwa cha uume, kwenye kishina cha uume na kuzunguka njia ya haja kubwa. Pia mwanaume anaweza kupata sundosundo sehemu za siri. Ugonjwa huu husababisha matatizo ya moyo, na kuharibu ubongo na kuzaa watoto walemavu.

Klamdia:


Dalili yake kwa mwanamke mara nyingi siyo rahisi kuonekana. Kwa mwanaume dalili ni kupata maumivu wakati wa kukojoa, na kukojoa mara kwa mara. Athari kwa mwanamke ni kuziba kwa mirija ya kupitisha mayai na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi. Mimba hizi kuhatarisha maisha ya mama na kuleta ugumba vinaweza kutokea. Kwa mwanaume athari ni kuziba mirija ya kupitisha mbegu na utasa.
The ListPages module does not work recursively.

Kankroidi:


Dalili yake ni vidonda sehemu za siri vinavyokuwa na maumivu makali, maumivu wakati mkojo unapopita kwenye vidonda na kuvimba tezi sehemu za siri. Tezi huweza kupasuka na kutoa uchafu na maumivu makali.

Utando mweupe:


Dalili kwa mwanamke ni kutokwa na uchafu ukeni (kama maziwa yaliyoganda), kuwashwa na kuwa na michubuko sehemu za siri. Kwa mwanaume ni kuwashwa sehemu za siri na kusikia maumivu wakati wa kukojoa. Athari ni maumivu wakati wa kujamiiana.
The ListPages module does not work recursively.

Virusi vya UKIMWI:


Katika hatua ya mwanzo baada ya kuambukizwa hakuna dalili maalum. Hatua hii inaweza kuchukua mpaka miaka kumi. Lakini mara mtu anapoanza kuugua UKIMWI dalili zinakuwa nyingi. Pamoja na kupungua kinga ya mwili, kupungua uzito na kuumwa mara kwa mara. Matokeo ya kuugua UKIMWI baada ya muda fulani ni kifo.
AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya Kujikinga na Maambukizi ya Kisonono na Kaswende

Jinsi ya Kujikinga na Maambukizi ya Kisonono na Kaswende

Jinsi ya Kujikinga na Maambukizi ya Kisonono na Kaswende 🌟

Karibu sana kwenye makala hi... Read More

Jinsi ya Kujikinga na Mimba Pasipo Kuharibu Afya ya Mwili

Jinsi ya Kujikinga na Mimba Pasipo Kuharibu Afya ya Mwili

Jinsi ya Kujikinga na Mimba Pasipo Kuharibu Afya ya Mwili

Leo tutajadili jinsi ya kujiking... Read More

Nifanyeje Kuelewa Hatari na Faida za Ngono kabla ya Kuanza?

Nifanyeje Kuelewa Hatari na Faida za Ngono kabla ya Kuanza?

Nifanyeje Kuelewa Hatari na Faida za Ngono kabla ya Kuanza? 🌍πŸ’₯😊

Karibu kijana! Le... Read More

Je, watu wanaamini nini katika kuongeza mchezo wa hisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, watu wanaamini nini katika kuongeza mchezo wa hisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, watu wanaamini nini katika kuongeza mchezo wa hisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi? Kufanya ... Read More

Vidokezo vya Kuepuka Mazungumzo ya Kuchosha na Msichana

Vidokezo vya Kuepuka Mazungumzo ya Kuchosha na Msichana

Mazungumzo ni sehemu muhimu katika uhusiano wowote wa kimapenzi. Lakini kuna wakati mazungumzo ya... Read More

Njia za Kuzuia Mimba

Njia za Kuzuia Mimba

Njia za uzazi wa mpango zinatofautiana sana na zinaweza kugawanywa katika makundi mengi:

Vizuizi... Read More

Kulambana sehemu za siri ni salama kiafya? Je, tendo hili ni la kawaida?

Kulambana sehemu za siri ni salama kiafya? Je, tendo hili ni la kawaida?

Si rahisi kusema ni kitendo kipi kilicho cha kawaida na kisicho cha kawaida. Kulamba ni jambo linalo... Read More
Je, nini kitatokea iwapo mwanamke atatumia dawa za kulevya wakati wa ujauzito?

Je, nini kitatokea iwapo mwanamke atatumia dawa za kulevya wakati wa ujauzito?

Kama mama mjamzito atatumia dawa za kulevya basi humuathiri mtoto moja kwa moja. Mtoto aliye tumb... Read More

Kwa nini nao watu wanaishi kwenye ndoa wanapata maambukizi ya virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Kwa nini nao watu wanaishi kwenye ndoa wanapata maambukizi ya virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Kuna sababu kuu mbili i kwa wana ndoa kupata maambukizi i ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI.
Kw... Read More

Wakati wa makuzi/ kubalehe/ kuvunja ungo, ni mabadiliko gani yanatokea kwenye miili ya wasichana?

Wakati wa makuzi/ kubalehe/ kuvunja ungo, ni mabadiliko gani yanatokea kwenye miili ya wasichana?

Balehe ni kipindi cha mpito kati ya utoto na utu uzima, ambapo watoto wa ki... Read More

Je, Ni Lazima Kufanya Ngono Kwa Sababu ya Marafiki au Shinikizo za Kisiasa?

Je, Ni Lazima Kufanya Ngono Kwa Sababu ya Marafiki au Shinikizo za Kisiasa?

Je, ni lazima kufanya ngono kwa sababu ya marafiki au shinikizo za kisiasa? πŸ€”

Ndugu vij... Read More

Madhara ya dawa za kulevya yanadumu kwa muda gani?

Madhara ya dawa za kulevya yanadumu kwa muda gani?

Ni vigumu sana kujibu swali hili kwa sababu muda wa madhara hutegemea sababu mbalimbali kama vile... Read More