Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
☰
AckyShine

Njia za Kuzuia Mimba

Featured Image
Njia za uzazi wa mpango zinatofautiana sana na zinaweza kugawanywa katika makundi mengi:

Vizuizi


(hizi huzuia mbegu kulifikia yai): Kuna mpira wa kiume (kondomu ya kiume), yaani mfuko wa mpira uliozibwa upande moja. Unavishwa kwenye uume uliosimama kabla ya kuingia ukeni. Pia kuna mpira wa kike (kondomu ya kike), yaani mpira unaoingizwa ukeni kabla ya kujamiiana.

Vidonge vya kuzuia mimba:


Lazima mwanamke anywe vidonge hivi kila siku hata kama hajamiiani.

Njia nyingine za kuzuia mimba kwa muda mrefu


. Njia hizi hazihitaji maandalizi maalum, ili kuzuia mimba, kabla ya kujamiiana na pia mwanamke hahitaji kukumbuka kufanya chochote kila siku. Kati ya njia hizi ni pamoja na sindano anazopewa mwanamke kila baada ya miezi mitatu. Pili, kuna vipandikizi, yaani vijiti vyembamba vya plastiki vinavyowekwa kwenye sehemu ya juu ya mkono wa mama kwa njia ya upasuaji mdogo. Vijiti vina kichocheo kinachozuia kupevuka kwa yai. Pia, kuna kitanzi ambacho ni kitu kidogo kilichotengenezwa kwa aina maalum ya plastiki. Kwa ufupi kinaitwa IUD. Huwekwa kwa utaalamu ndani ya mfuko wa uzazi. Sindano, vipandikizi na vitanzi lazima viwekwe na mtaalamu mwenye ujuzi kwenye kituo cha afya chenye vifaa vya kutosha. Kwa vile dawa za kuzuia mimba kwa muda mrefu zinaingiliana na mzunguko wa kawaida wa hedhi kwa kiasi, athari zake ni kubwa kuliko kutumia vidonge.

Kwa mwanaume na mwanamke kuna njia ya kudumu ya kufunga kizazi kwa njia ya upasuaji


. Kwa mwanaume mirija inayopitisha mbegu hukatwa na kufungwa, ili kuzuia mbegu zisitoke. Akijamiiana, anaweza kumwaga shahawa, lakini ndani ya shahawa hakuna mbegu. Kama mwanaume amefunga kizazi uume utadinda kama kawaida na kufikia mshindo atamwaga maji ya shahawa ambayo hayatakuwa na mbegu. Kwa mwanamke mirija ya kupitisha mayai hukatwa na kufungwa, ili kuzuia mayai kufika kwenye mfuko wa uzazi. Baada ya upasuaji huu, mama ataendelea na hedhi kama mwanzo, lakini yai halitaweza kukutana na mbegu za kiume tena.

Vilevile kuna njia nyingine mbalimbali ambazo hazina uhusiano na matumizi ya dawa au vizuizi vya mimba. Njia hizi hazina uhakika mkubwa wa kutopata mimba. Mara nyingine mama anatumia ishara mbalimbali, au tarehe kujua lini anaweza kupata mimba, ili kuepuka kujamiiana katika kipindi hicho. Kumwaga mbegu za kiume nje ya uke, au kutegemea kwamba mimba hazishiki wakati wa kunyonyesha ni njia nyingine za asili zinazotumiwa. Kumbuka kwamba njia hizi hutumika sana, lakini si njia salama sana za kuzuia mimba wala kuambukizwa na magonjwa ya zinaa.
Ni muhimu kukumbuka kwamba njia ya uzazi wa mpango inaweza kufaa kwa mtu huyu na isifae kwa mtu mwingine. Kwa hiyo, ni vizuri kila mtu aliyeamua kupanga uzazi apate ushauri kwenye kliniki kuhusu njia inayomfaa zaidi
AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Je, ni kweli kuwa ulemavu unaweza kugundulika mara tu mtoto anapozaliwa?

Je, ni kweli kuwa ulemavu unaweza kugundulika mara tu mtoto anapozaliwa?

Ni kweli kuwa daktari anaweza kufanya vipimo vya kugundua
kama mtoto aliye tumboni ni mwenye... Read More

Vijana Albino wafanye nini ili kulinda ngozi yao?

Vijana Albino wafanye nini ili kulinda ngozi yao?

Pamoja na matatizo ya kuona, ngozi ya Albino ni rahisi sana
kudhurika kwa mionzi ya jua. Hat... Read More

Inakuaje mwanaume anaonyesha dalili za magonjwa ya zinaa zaidi kuliko mwanamke?

Inakuaje mwanaume anaonyesha dalili za magonjwa ya zinaa zaidi kuliko mwanamke?

Wanaume mara nyingi huambukizwa sehemu za mrija wa mkojo. Katika sehemu hizi ni rahisi kusikia mw... Read More

Je, kuna vipimo ambavyo vinaweza kugundua hali ya kuwepo kwa ualbino wakati kichanga kikiwa bado tumboni?

Je, kuna vipimo ambavyo vinaweza kugundua hali ya kuwepo kwa ualbino wakati kichanga kikiwa bado tumboni?

Hakuna kipimo rahisi cha kuwezesha kuonyesha kama mama
mjamzito amebeba kinasaba cha ualbino... Read More

Je, uke wa mwanamke unaweza kupanuka kiasi gani?

Je, uke wa mwanamke unaweza kupanuka kiasi gani?

Wakati wa kujifungua, uke wa mwanamke mzima hupanuka kuanzia kipenyo cha sentimeta kumi mpaka kum... Read More

Jinsi ya kufanya wazazi wamkubali mchumba

Jinsi ya kufanya wazazi wamkubali mchumba

Uhusiano mzuri na wazazi ni muhimu sana siyo katika masuala ya uchaguzi wa mchumba tu, bali katika m... Read More
Kwa nini nao watu wanaishi kwenye ndoa wanapata maambukizi ya virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Kwa nini nao watu wanaishi kwenye ndoa wanapata maambukizi ya virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Kuna sababu kuu mbili i kwa wana ndoa kupata maambukizi i ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI.
Kw... Read More

Je, gongo na sigara husaidia uyeyushaji wa chakula?

Je, gongo na sigara husaidia uyeyushaji wa chakula?

Ni imani na fikra potofu kwamba, ukinywa gongo au kuvuta
sigara kwa kiasi kidogo baada ya ch... Read More

Je, Ni Vipi Kuepuka Shinikizo la Kufanya Ngono?

Je, Ni Vipi Kuepuka Shinikizo la Kufanya Ngono?

Je, ni vipi kuepuka shinikizo la kufanya ngono? Hii ni swali ambalo vijana wengi hujikuta wakijiu... Read More

Jinsi ya Kutambua Ishara za Kuwa Tayari kwa Ngono

Jinsi ya Kutambua Ishara za Kuwa Tayari kwa Ngono

Jinsi ya Kutambua Ishara za Kuwa Tayari kwa Ngono 😊

Karibu kijana, leo tutaongelea jamb... Read More

Nifanyeje Kujielewa na Kuelewa Miili Yetu kabla ya Kujihusisha na Ngono?

Nifanyeje Kujielewa na Kuelewa Miili Yetu kabla ya Kujihusisha na Ngono?

Jinsi ya Kujielewa na Kuelewa Miili Yetu kabla ya Kujihusisha na Ngono 😊😊😊

Karibu... Read More

Madhara yatokanayo na ukeketaji

Madhara yatokanayo na ukeketaji

Ukeketaji au tohara ya wanawake ni hatari sana kwa msichana anayetahiriwa. Wasichana hufa kutokana n... Read More