Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
☰
AckyShine

Mapishi ya Wali Wa Kukaanga Kwa Nyama Mbuzi Ilichomwa Ya Sosi Ya Ukwaju

Featured Image

Vipimo Vya Wali

Mchele Basmati - 4 vikombe

Vitunguu vya majani (Spring onions) - 5 miche

Pilipili mboga nyekundu (capsicum) - 1

Pilipili mboga manjano (capscimu) - 1

Nyanya kubwa - 1

Supu ya kidonge - 2

Siagi - 2 vijiko vya supu

Chumvi - kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha mchele kisha roweka kiasi masaa matatu takriban.
Katakata vitunguu majani, mapilipili boga, nyanya vipande kiasi.
Weka siagi katika sufuria ya kupikia, weka katika moto iyayuke.
Tia vitunguu majani, mapilipili boga, nyanya, kaanga kidogo tu.
Tia mchele kaanga kidogo, kisha tia maji kiasi ya kuivisha mchele.
Tia supu ya kidogo au supu yoyote, funika wali upikike moto. mdogodogo.

Vipimo Vya Nyama Mbuzi Na Sosi Ya Ukwaju

Nyama mbuzi mapande makubwa kiasi - 7/8 vipande

Kitunguu saumu(thomu/galic) kilosagwa - 1 kijiko cha supu

Pilipili mbichi ilosagwa - 1 kijiko cha supu

Ukwaju mzito ulokamuliwa - 1 kikombe cha chai

Jiyra/cummin/bizari pilau - 1 kijiko cha chai

Nyanya kopo - 2 vijiko vya supu

Siki - 2 vijiko vya supu

Mafuta - Β½ kikombe cha chai

Chumvi - kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Changanya vitu vyote pamoja katika kibakuli kidogo.
Weka nyama katika bakuli kubwa kisha tia mchanganyiko wa sosi, ubakishe sosi kiasi pembeni.
Roweka kwa muda wa masaa 3 – 5
Panga nyama katika bakuli au treya ya kuchomea katika oven.
Pika (bake) kwa moto wa kiasi kwa muda wa saa takriban.
Karibu na kuiva, epua, zidisha kuichangaya na sosi ilobaki.
Rudisha katika jiko uendelee kuipika muda kidogo tu.
Epua ikiwa tayari, weka juu ya wali uliopakuwa kisha mwagia sosi ya nyanya pilipili (chilii tomato sauce) ukipenda.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Mapishi ya Pasta za cream na uyoga

Mapishi ya Pasta za cream na uyoga

Mahitaji

Pasta (2 na 1/2 vikombe vya chai)
Uyoga (mashroom 2 vikombe vya chai)
... Read More

Jinsi ya kupika Biskuti Za Tende

Jinsi ya kupika Biskuti Za Tende

Viamba upishi

Unga 4 Vikombe vya chai Sukari ya laini (icing sugar) 1 Kikombe cha chai Ba... Read More
Mapishi ya choroko

Mapishi ya choroko

Mahitaji

Choroko kikombe 1 na nusu
Nazi kopo 1
Kitunguu kikubwa 1
Nyanya 1... Read More

Mapishi ya Ugali Mchuzi Wa Samaki Nguru Wa Nazi Na Bamia Za Kukaanga

Mapishi ya Ugali Mchuzi Wa Samaki Nguru Wa Nazi Na Bamia Za Kukaanga

Vipimo Vya Ugali:

Unga wa mahindi/sembe - 4

Maji - 6 takriban

Namna Ya Kutay... Read More

Jinsi ya kupika Wali Wa Karoti Na Nyama

Jinsi ya kupika Wali Wa Karoti Na Nyama

Viambaupishi: Wali

Mchele 3 Magi

Mafuta 1/4 kikombe

Karoti unakata refu refu ... Read More

Mapishi ya Biskuti Za Mtindi/Yoghurt

Mapishi ya Biskuti Za Mtindi/Yoghurt

MAHITAJI

Chenga za biskuti - 3 gilasi

Mtindi (yogurt) - 1 Kopo (750g)

Maziwa ... Read More

Mapishi ya Pilau Ya Sosi Ya Soya Na Mboga

Mapishi ya Pilau Ya Sosi Ya Soya Na Mboga

Viambaupishi

Kuku (mkate mkate vipande) 1

Mchele wa Basmati (rowanisha) 3 magi

<... Read More
Mapishi ya visheti vitamu

Mapishi ya visheti vitamu

VIAMBAUPISHI

Unga - Vikombe 2

Samli au shortening ya mboga - 2 Vijiko vya supu

<... Read More
Mapishi ya Ndizi Mbichi Za Nyama Ng'ombe

Mapishi ya Ndizi Mbichi Za Nyama Ng'ombe

Vipimo

Ndizi mbichi - 10

Nyama - kilo 1

Nazi ya kopo - 1

Chumvi - 1 Kij... Read More

Mapishi ya Biriani Ya Samaki Nguru, Njegere Na Snuwbar (UAE)

Mapishi ya Biriani Ya Samaki Nguru, Njegere Na Snuwbar (UAE)

Mahitaji

Mchele wa basmati - 4 cups

Samaki nguru (king fish) - 7 vipande au zaidiRead More

Mapishi mazuri ya Uji wa ulezi

Mapishi mazuri ya Uji wa ulezi

Mahitaji

Unga wa ulezi (millet flour vijiko 3 vya chakula)
Maziwa fresh (milk 1/2 ki... Read More

Mapishi ya Biriani Nyepesi Kupika Ya Samaki

Mapishi ya Biriani Nyepesi Kupika Ya Samaki

Vipimo

Mchele wa pishori (basmati) - 4

Vitunguu katakata - 3

Nyanya (tungule)... Read More