Eti kwa nini Watu hawapostigi hii? Hata selfie sijaonaga
Updated at: 2024-05-25 16:59:02 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vijana mkiwa mnaendesha magari mna post mukiwa mpo beach mna post mkiwa kwenye masherehe mna post Lakin mkiwa mmeenda kwa mganga siwaoni kupost mitunguli na vibuyu vya mganga unakuwa je wa zee tena. 😀😀😀😀
Updated at: 2024-05-25 17:54:01 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Usije ukaenda kwa mganga, mwenzako yamenikuta, yani masharti niliyopewa, acha tu, yalikua hivi:-
1.Jasho la nyoka. 2.Manyoya ya mende. 3.Sisimizi Shoga. 4.Mbwa mjane. 5.Kuku aliye single. 6.Samaki mwenye miaka miwili bila kuoga 7.Mti wenye ujauzito. 8.Mbavu za Nzi. 9.Nywele za Kiroboto. 10.Mwanya wa Mbu. Duuh..!! mwanangu kwa hali hii mbona itakula kwako. Wengine wanasemaga IGA UFE! Rizik anagawa Mungu tu shetan simuelew!
Je, hii ni kweli kwa wale wasichana wasiojibu meseji WhatsApp!!!?
Updated at: 2024-05-25 16:56:10 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Ukiona hivyo ujue ndio hivi
Mwanaume mwenzangu ukiona unamtext msg msichana WhatsApp kaisoma hajajibu, umetuma ya pili kasoma hajajibu, ukatuma ya tatu hajajibu mmmmmh😨😨 hapo ujue mwenzio kaangalia kwenye profile yako, kakagua picha weee mwishoni akajisemea tu "Huyu.mkaka hapana kwa kweli"🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Angalia alichokifanya huyu mtu baada ya kuokota wallet ya thamani
Updated at: 2024-05-25 17:15:08 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Jamaa aliokota wallet, alipofika nyumbani akapiga simu kwenye radio station "naitwa Juma nimepiga simu kutangaza kuwa nimeokota wallet ndani ina laki7, ATM card na karatasi yenye PIN ya ATM card na kijimfuko cha dhahabu" Mtangazaji akasema, kwa hiyo ungependa kumrudishia mwenyewe kama anakusikiliza? Jamaa akajibu; hapana, ninaomba kumuombea dedication wimbo wa R.Kelly usemao "U SAVED ME" umfikie popote alipo!!
Haya ndiyo madhara ya kutowapeleka watoto kanisani ⛪
Updated at: 2024-05-25 17:08:53 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
MTOTO aliibiwa yeboyebo KANISANI akawa analia sana kwa uchungu mpaka MCHUNGAJI akamwambia usilie mwachie MUNGU. MTOTO akajibu Mungu hazimtoshi zile yebo ni ndogo! Usicheke,
Huu ni Mtihani Tuwapeleke Watoto KANISANI Wamjue MUNGU.
Updated at: 2024-05-25 17:07:17 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Jana usiku kuna Jirani yangu..kanitumia text "mambo vipi?"…halafu tunakaa nae mtaa mmoja nikaona nikimjibu ni uharibifu wa hela nikaenda kumgongea mlango saa 7 usiku. Alipofungua nikamjibu "shwari"halafu nikarudi nyumbani kulala zangu..