Nikitafuta rafiki kwa nia ya kuoana (mchumba), je ni sifa gani niangalie kwa msichana/mvulana?
Date: April 17, 2022
Author: SW - Melkisedeck Shine
Kuchagua mchumba ni moja ya maamuzi ambayo kijana anahitaji kuyafanya kwa uangalifu mkubwa sana. Kwa sababu huyo ndiye atakayekuwa mwenzi wake wa maisha. Katika kuchagua mchumba kila mtu ana mawazo yake kuhusiana na kilicho muhimu kuzingatiwa. Mara nyingi mhemuko una nguvu zaidi kuliko uamuzi wa kimantiki
Hata hivyo, vifuatavyo ni kati ya vigezo ambavyo vinaweza kuangaliwa:
• Chagua mtu anayekuheshimu wewe na wengine; Chagua mtu unayemwamini;
• Chagua mtu ambaye unaweza kuongea, kujadiliana, na kuhojiana naye kwa uwazi bila kugombana;
• Chagua mtu mwenye umri unaokaribiana na wa kwako;
• Chagua mtu anayependelea vile unavyopendelea;
• Chagua mtu ambaye ataelewa matatizo yako na yuko tayari kukusaidia kuyatatua; na
• Chagua mtu mwenye afya nzuri.
Hii inamaanisha pia kumpata mtu ambaye kabla ya kuanza kujaamiana naye, atakuwa tayari kwenda kupima kwa hiari kujua hali yake ya VVU na pia kuwa tayari kutumia kinga kwa maana ya kondomu hadi hapo mtakapojua hali zenu.
Wafahamishe wazazi wako mtu uliyemchagua kama mchumba na mtambulishe kwao i ili wamfahamu na yeye awafahamu wazazi wako. Wakati huohuo na wewe jaribu kuwafahamu wazazi wake. Usifanye uchumba wa haraka. Pata muda wa kutosha kumwelewa rafiki yako.
Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.
Related Posts
Je, watu wanapendelea ngono/kufanya mapenzi ya mvutano au ngono/kufanya mapenzi ya kupumzika? Hil...
Read More
Ukitaka kuelewa jinsi mimba i inavyopatikana, lazima uelewe mzunguko wa hedhi wa mwanamke. Baada ...
Read More
Kifungu cha 14 cha Katiba ya Tanzania kinaeleza kwa ufasaha
kuwa: “Kila mtu ana haki ya ku...
Read More
Hakuna uchunguzi wa kisayansi ambao umeonyesha faida
yoyote inayopatikana kwa kuua Albino.Read More
Kama umeamua kutojamiiana kabla ya ndoa, huo ni uamuzi mzuri na ni haki yako. Kutojamiiana kabla ...
Read More
Watu ambao wanaonekana tofauti na wengine (ama kwa misingi
ya kabila, rangi, dini, kimo au h...
Read More
Watu wengi huwaona Albino kama watu tofauti na watu wengine
na kuwakwepa, wanaweza hata kuba...
Read More
Jinsi ya Kusimamia Uchungu wa Kupendwa na Msichana
Kupendwa na msichana ni jambo la kufura...
Read More
Inakuwaje mtoto anakuwa wa kike au wa kiume?
Mwili wa mwanaume unatengeneza aina mbili za...
Read More
Jinsi ya Kuonyesha Utambulisho Wako kwa Msichana
Kuonyesha utambulisho wako kwa msichana n...
Read More
Ukweli ni kwamba hakuna madhara yoyote ya kiafya ukikaa muda mrefu bila kujamii ana. Hakuna madha...
Read More
Inawezekana kwa msichana mdogo kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanaume mwenye umri mkubwa. Hata...
Read More
No comments yet. Be the first to share your thoughts!