Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
AckyShine

Dalili, athari, kinga na tiba ya ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB)

Featured Image
Kifua kikuu ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea vya bacteria na kuenezwa kwa njia ya hewa. Mtu mwenye maambukizi ya kifua kifua kikuu akikohoa, kupiga chafya au kutema mate ovyo husambaza vijidudu hewa, huweza kumwabukiza mtu mwingine kama atakuwa hajaanza kutumia dozi ya kifua kikuu.

Dalili za kifua kikuu.



  1. Kukohoa kwa muda wa wiki mbili au zaidi

  2. Maumivu ya kifua

  3. Homa za usiku

  4. Kutoka jasho kwa wingi usiku

  5. Kupungua uzito

  6. Kukohoa damu

  7. Kukosa hamu ya chakula na mwili kuwa dhaifu


Athari za kifua kikuu.



  1. Ugonjwa huweza kuenea kwenye viungo vingine vya mwili.

  2. Watu wengine hupoteza maisha iwapo hawatapata tiba sahihi mapema.

  3. Watu wengine huambukizwa ugonjwa katika muda mfupi.

  4. Wagonjwa wa kifua kikuu hawazezi kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendelea.

  5. Matibabu ya kifua kikuu huchua muda mrefu na ni gharama kubwa.


Kinga za ugonjwa wa kifua kikuu.


Ugonjwa huu unakingwa kwa chanjo ya kifua kikuu kwa kitaalamu (BCG) ambayo hutolewa mara tu mtoto anapozaliwa.
Ili kupunguza uwezekano wa kupata kifua kikuu zingatia yafuatayo;


  1. Kujenga na kuishi kwenye nyumba zinazoruhusu mzunguko kwa hewa ya kutosha (ziwe na madirisha makubwa ya kutosha)

  2. Epuka kukaa kwenye msongamano wa watu wengi

  3. Watoto wanyonyeshwe maziwa ya mama pekee kwa miezi sita na umlikiza kwa vyakula vyenye virutubisho ili kumjengea kinga imara

  4. Kula vyakula vyenye lishe bora

  5. Kutotema mate na makohozi ovyo ili kuziua usambaaji wa bacteria wasababishao Kifua kikuu.


Ratiba ya chanjo.


Chanjo ya kifua kikuu hutolewa baada ya mtoto kuzaliwa au anapofika kliniki kwa mara ya kwanza
Iwapo kovu kwa mtoto halijajitokeza chanjo irudiwe katika kipindi cha miezi 3.

Tiba ya kifua kikuu (TB)


Ugonjwa wa kifua kikuu unatibika. Matibabu yake huchukua muda mrefu wa miezi 6 hadi 8 na ni ya gharama kubwa.

Inashauriwa mgonjwa awahi matibabu mapema kwenye vituo vya kutolewa huduma za kinga.

Ugonjwa wa kifua kikuu ni hatari, hata hivyo unakingwa kwa chanjo.

Mzazi au mlezi hakikisha kila mtoto anapozaliwa anapata chanjo ya kuzuia kifua kuu

“Kumbuka chanjo ya kifua kikuu (BCG) Itamkinga mtoto dhidi ya ugonjwa wa kifua kikuu”.
AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Tatizo la maumivu wakati na baada ya kufanya mapenzi

Tatizo la maumivu wakati na baada ya kufanya mapenzi

Wakati wa kufanya tendo la ndoa wapo baadhi ya watu hupatwa na maumivu wakati au baada ya kushiriki ... Read More
Vyakula vinavyofaa kuliwa katika kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani

Vyakula vinavyofaa kuliwa katika kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani

Vyakula vinavyofaa kuliwa wakati huu wa mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni vingi, leo tutaan... Read More

Namna ya kujitibu chunusi kwa kutumia dawa ya meno au dawa ya mswaki

Namna ya kujitibu chunusi kwa kutumia dawa ya meno au dawa ya mswaki

Dawa ya mswaki au dawa ya meno ni dawa nyingine ya asili unayoweza kutumia kujitibu chunusi. Hii... Read More

Mambo ya kuzingatia kuhusu ugonjwa wa Kaswende

Mambo ya kuzingatia kuhusu ugonjwa wa Kaswende

Kaswende husababishwa na bakteria aitwaye Treponema pallidum , ambaye pia huitwa spirochetes kutokan... Read More
Sababu na madhara ya tatizo la kukosa choo

Sababu na madhara ya tatizo la kukosa choo

Tatizo la kukosa choo (constipation) ni tatizo ambalo limekuwa likiwakumba watu wengi sana katika du... Read More
Vyakula vinavyosaidia kuongeza kinga ya mwili

Vyakula vinavyosaidia kuongeza kinga ya mwili

Watu wengi tumekuwa tukijali kazi zetu za kila siku bila kujali hali ya afya zetu matokeo yake ku... Read More

Ushauri kuhusu mwili wako

Ushauri kuhusu mwili wako

Nimekutana na hiki kitabu japo nimekipitia juu juu nikaona nisiwe mchoyo Wa kukushirikisha wewe u... Read More

Umuhimu wa kula fenesi kiafya

Umuhimu wa kula fenesi kiafya

Fenesi ni miongoni mwa matunda ya msimu yenye umbo la kipekee huku likiwa na ladha tamu isiyomith... Read More

Tiba kwa kutumia maji

Tiba kwa kutumia maji

⭕Tiba kwa kutumia maji⭕
💧💧💧💧💧💧💧💧💧

Hamuwezi kuamini! mar... Read More

Vyakula 7 vya kuepuka kula ili uwe na afya nzuri

Vyakula 7 vya kuepuka kula ili uwe na afya nzuri

Inasemwa kuwa “wewe ni kile unachokula” kwa kumaanisha kuwa mwonekano wetu na afya ya mwili n... Read More

Faida za kula uyoga kiafya

Faida za kula uyoga kiafya

Uyoga una vitamini na aina nyingi na madini. Virutubisho vilivyothibitishwa kuwemo kwenye uyoga n... Read More

Njia bora za kumfanya mtu aache kuvuta sigara

Njia bora za kumfanya mtu aache kuvuta sigara

Ni kazi ngumu kidogo kuacha uvutaji wa sigara. Uvutaji ni tishio kwa maisha yetu. Yawezekana hufa... Read More