Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
AckyShine

Jinsi ya kupika Mseto Kwa Mchuzi Wa Samaki Wa Nazi

Featured Image

Vipimo vya mseto

Tanbihi: Kiasi ya vipimo inategemea wingi wa watu, unaweza kupunguza au kuongeza. Hiki ni kiasi cha watu 6 takriban.

Chooko - 3 Vikombe

Mchele - 2 Vikombe

Samli - 2 vijiko Vya supu

Chumvi - kiasi

NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA

Safisha na kosha chooko utoe taka taka zote.
Osha mchele kisha roweka pamoja na chooko kwa muda wa saa au zaidi.
Pika chooko na mchele ukiongeza maji inapohitajika, tia chumvi, funika pika moto mdogo mdogo huku unakoroga kwa mwiko kila baada ya muda huku unaponda ponda.
Karibu na kuwiva na kupondeka tia samli endelea kupika hadi karibu na kukauka. Epua.

Samaki

Vipande vya samaki (nguru) - 6 – 7 (4LB)

Kitunguu saumu na tangawizi iliyosagwa - 2 vijiko vya supu

Pilipili ya unga nyekundu - 1 kijiko cha supu

Pilipili mbichi iliyosagwa ukipenda - 1 kijiko cha chai

Bizari ya samaki - 1 kijiko cha chai

Chumvi - kiasi

Ndimu - kiasi

Mafuta ya kukaangia - kiasi

Namna Ya Kutaysha Na Kupika

Changanya thomu/tangawizi, pilipili, bizari, chumvi pamoja na ndimu iwe masala nzito.
Paka vipande vya nguru kwa masala hayo weka akolee dakika kumi hivi.
Kaanga vipande vya nguru katika mafuta madogo kwenye kikaango (fyring pan) uweke upande.

Mchuzi Wa Nazi

Vitunguu maji – katakata vidogodogo - 4

Nyanya zilizosagwa (crushed) - 3- 4

Nyanya kopo - 1 kijiko cha chai

Mafuta - 3 vijiko vya supu

Bizari ya mchuzi - 1 kijiko cha chai

Bamia zilizokatwa ndogo ndogo - 2 vikombe

Chumvi - kiasi

Ndimu - 2 vijiko vya supu

Tui la nazi - 3 Vikombe au 800 ml

Namna Ya Kupika

Katika karai au sufuria, tia mafuta ukaange vitunguu hadi vianze kugeuka rangi.
Tia nyanya zilizosagwa, nyanya kopo, uendelee kukaanga, kisha tia bizari, chumvi.
Tia nazi na mwisho tia bamia uache ziwive kidogo tu.
Tia vipande vya samaki vilivyokwisha kaangwa.
Tayari kuliwa na mseto upendavyo.

Vidokezo:

Bizari nzuri kutumia ni ya 'Simba Mbili' inaleta ladha nzuri katika mchuzi.
Ni bora kupika mchuzi kwanza kabla ya mseto kwani mseto ukikaa kwa muda unazidi kukauka.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Vitafunio vya Afya kwa Kutosheleza Hamu Zako

Vitafunio vya Afya kwa Kutosheleza Hamu Zako

Vitafunio vya Afya kwa Kutosheleza Hamu Zako 🍇🍎🥕

Hakuna jambo bora zaidi kama kuf... Read More

Namna ya kupika Vitumbua

Namna ya kupika Vitumbua

Vitumbua ni aina ya vitafunwa vya chai ambavyo hutengenezwa kwa kutumia unga wa mchele. Kiasili v... Read More

Jinsi ya kupika mkate wa sembe

Jinsi ya kupika mkate wa sembe

Mahitaji:

Unga sembe glass 1
Unga ngano glass 1
Sukari glass 1 (unaweza kupungu... Read More

Jinsi ya kupika mboga ya majani ya mashona nguo

Jinsi ya kupika mboga ya majani ya mashona nguo

Viamba upishi

Mashonanguo mkono 1
Tui la nazi kikombe 1
Karanga zilizosagwa kik... Read More

Jinsi ya kutengeneza Visheti Vyeupe Na Vya Kaukau

Jinsi ya kutengeneza Visheti Vyeupe Na Vya Kaukau

VIAMBAUPISHI

Unga - 4 Vikombe vya chai

Siagi - 1 Kikombe cha chai

Hiliki ½ K... Read More

Jinsi ya kupika Pilau ya Mpunga Na Nyama Ya Ng’ombe

Jinsi ya kupika Pilau ya Mpunga Na Nyama Ya Ng’ombe

Mahitaji

Mpunga - 4 vikombe

Nyama - 1 kilo moja

Kitunguu maji - 3

Mbata... Read More

Jinsi ya kupika Magimbi Kwa Nyama Ya Ng’ombe

Jinsi ya kupika Magimbi Kwa Nyama Ya Ng’ombe

Vipimo

Majimbi (Eddoes) kiasi 6 au 7

Nyama ng’ombe ½ kilos

Tangawizi ilosa... Read More

Jinsi ya kupika Wali Wa Sosi Ya Tuna

Jinsi ya kupika Wali Wa Sosi Ya Tuna

Viambaupishi

Sosi Ya tuna

Tuna (samaki/jodari) 2 Vikopo

Vitunguu (kata kata) ... Read More

Jinsi ya Kupika skonzi

Jinsi ya Kupika skonzi

Mahitaji

Unga wa ngano (self risen flour 2 vikombe vya chai)
Sukari (sugar 1/2 kijik... Read More

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Tende

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Tende

MAHITAJI

Unga - 4 Vikombe vya chai
Sukari ya laini (icing sugar) - 1 Kikombe cha cha... Read More

Mapishi ya Mseto wa choroko

Mapishi ya Mseto wa choroko

Mahitaji

Mchele 2 vikombe vya chai
Choroko kikombe 1 na 1/2
Nazi kopo 1
Sw... Read More

Jinsi ya kupika Vileja

Jinsi ya kupika Vileja

VIPIMO

Unga wa mchele 500g

Samli 250g

Sukari 250g

Hiliki iliyosagwa 1/2 k... Read More