Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
AckyShine

Mapishi ya Biriani Ya Kuku Wa Kuchoma Wa Tanduri

Featured Image

Mahitaji

Mchele - 4 vikombe

Kuku - 1

Vitunguu - 3

Nyanya/tungule - 4

Zabibu kavu - ½ kikombe

Tangawizi na kitunguu (thomu/galic) - 2 vijiko cha supu

Pilipili mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha supu

Mtindi (yoghurt) - 2 kijiko cha supu

Masala ya tanduri - 2 vijiko vya supu

Pilipili manga - 1 kijiko cha chai

Hiliki - ½ kijiko cha chai

Mdalasini - kijiti kimoja

Ndimu - 3 vijiko vya supu

Chumvi - kiasi

Zaafarani (saffron) - 1 kijiko cha chai

Mafuta - ½ kikombe

Namna Ya Kutayarisha Kuku:

Baada ya kumsafisha kuku, mkate vipande vikubwa vikubwa kiasi upendavyo, muoshe mchuje atoke maji.
Katika bakuli, tia tangawizi, kitunguu thomu ilosagawa, pilipili mbichi ilosagwa, chumvi, ndimu, mtindi, masala ya tanduri na uchanganye vizuri, kisha mtie kuku na uchanganye tena na acha arowanike kwa muda wa kiasi saa au zaidi.
Panga kuku katika sinia ya kuchoma ndani ya oveni. Kisha mchome (grill) hadi awive, mtoe acha kando. Mwagia juu yake masala yatakayobakia katika sinia baada ya kumchoma.

Namna Ya Kutayarisha Masala Ya Nyanya:

Weka mafuta katika karai, tia vitunguu ulivyokatakata, kaanga hadi vianze kugeuka rangi.
Tia nyanya ulizokatakata, tia pilipili manga, hiliki, mdalasini, chumvi, na zabibu. Kaanga kidogo tu yakiwa tayari.

Namna Ya Kutayarisha Wali:

Osha na roweka mchele wa basmati.
Roweka zaafarani kwa maji ya moto kiasi robo kikombe weka kando.
Chemsha maji, tia chumvi, kisha tia mchele uive nusu kiini.
Mwaga maji uchuje mchele kisha rudisha katika sufuria au sinia ya foil. Nyunyizia zaafarini, na rudisha katika moto upike hadi uive kamili.
Epua, kisha pakua wali katika sahani au chombo upendacho, mwagia juu yake masala ya nyanya. Kisha weka vipande vya kuku ulivyochoma, biriani ikiwa tayari

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Mapishi ya Viazi vitamu na kachumbari

Mapishi ya Viazi vitamu na kachumbari

Mahitaji

Viazi utamu 3
Nyanya 2 kubwa
Kitunguu
Tango
Limao
Chumv... Read More

Jinsi ya kupika Mkate wa sinia

Jinsi ya kupika Mkate wa sinia

Mahitaji

Unga wa mchele (rice flour 2 vikombe vya chai)
Sukari (sugar 3/4 ya kikombe... Read More

Mapishi ya Biskuti Za Mayai

Mapishi ya Biskuti Za Mayai

VIAMBAUPISHI

Unga 3 Vikombe

Sukari ya unga (icing sugar) 1 Kikombe

Siagi 250 ... Read More

Bisikuti Za Kokoa (Cocoa Biscuits)

Bisikuti Za Kokoa (Cocoa Biscuits)

Viambaupishi

Siagi 100gm

Unga wa kaukau (cocoa powder) 2 Vijiko vya supu

Mazi... Read More

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Chumvi

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Chumvi

VIAMBAUPISHI

Unga - 3 Vikombe vya chai

Siagi - 250 gms

Baking powder - 3 Viji... Read More

Mapishi ya Wali Wa Kichina Wa Kamba Na Kuku

Mapishi ya Wali Wa Kichina Wa Kamba Na Kuku

MAHITAJI

Mchele wa pishori (basmati) - 4

Nyama ya kuku bila mafupa - 1 Lb

Kam... Read More

Vidokezo vya kukusaidia ule mboga za majani zaidi

Vidokezo vya kukusaidia ule mboga za majani zaidi

Ulaji wa mboga za majani ni muhimu kwa sababu zina vitamini na madini mengi na viwango vidogo vy... Read More

MAANA YA MANENO YANAYOTUMIKA KATIKA MASUALA YA LISHE

MAANA YA MANENO YANAYOTUMIKA KATIKA MASUALA YA LISHE

1. Chakula

ni kitu chochote kinacholiwa au kunywewa na kuupatia mwili virutubishi mbalimb... Read More

Jinsi ya kutengeneza Pilau Ya Kuku

Jinsi ya kutengeneza Pilau Ya Kuku

Mahitaji

Mchele wa basmati - 3 vikombe

Kuku - ½

Viazi - 4

Vitunguu - 2... Read More

Jinsi ya kuandaa Vileja Vya Karanga

Jinsi ya kuandaa Vileja Vya Karanga

MAHITAJI

Mayai 5

Sukari 450gm (1 lb)

Unga wa Ngano 1 kg

Siagi 450gm (... Read More

Mapishi ya Wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Samaki Na Rojo La Bilingani Na Viazi/Mbatata

Mapishi ya Wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Samaki Na Rojo La Bilingani Na Viazi/Mbatata

Wali Wa Nazi

Mpunga - 4 vikombe

Tui la nazi - 6 vikombe

Chumvi - Kiasi

Read More
Mapishi ya Pilau Ya Nyama Na Mtindi

Mapishi ya Pilau Ya Nyama Na Mtindi

MAHITAJI

Nyama iliyokatwa vipande - 1 Ratili(LB)

Mchele Basmati - 2 Magi

Chum... Read More