Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
☰
AckyShine

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

Featured Image

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji mwema
Kwa ajili ya makardinali na maaskofu wakuu; Uwape moyo wa kichungaji ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wa majimbo; Uwajaze na Roho wako ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre watawa; Wakamilishe katika wito wao ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre walioko hatarini; Uwaokoe ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wenye udhaifu; Uwatie nguvu ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wenye hofu; Uwape amani ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre waliokata tamaa; Uwavuvie upya ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wakaao upweke; Uwasindikize ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wamisionari; Uwalinde ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wanaohubiri; Uwaangazie ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre na watawa waliokufa; Uwafikishe kwenye utukufu wako ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wote; Wajalie hekima na ufahamu wako ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wote; Uwajalie elimu na shauri lako
Kwa ajili ya mapadre wako; wajalie wakuheshimu na wakuogope
Kwa ajili ya mapadre wote; Wajalie subira na upendo
Kwa ajili ya mapadre wote; wajalie utii na upole
Kwa ajili ya mapadre wote; uwajalie hamu kuu ya kuokoa roho za watu
Kwa ajili ya mapadre wote; wape fadhila za imani, matumaini na mapendo
Kwa ajili ya mapadre wote; Wajalie upendo mkuu kwa Ekaristi
Tunakuomba uwajalie mapadre wote; Waheshimu uhai na hadhi ya mtu ee Bwana
Tunakuomba uwajalie mapadre wote nguvu na bidii katika kazi zao ee Bwana
Tunakuomba uwajalie mapadre wote amani katika mahangaiko yao ee Bwana
Tunakuomba uwajalie mapadre wote upendo mkuu kwa Utatu Mtakatifu ee Bwana
Tunakuomba uwajalie mapadre wote upendo mkuu kwa Bikira Maria ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wawe mwanga wa Kristo ee Bwana
Uwajalie mapadre wote, wawe chumvi kwa ulimwengu ee Bwana
Uwajalie mapadre wote, wajizoeze kujitoa sadaka na kujinyima ee Bwana
Uwajalie mapadre wote, wawe watakatifu kimwili, kiakili na kiroho ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wawe watu wa sala ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wawe kioo cha imani kwako ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wajali sana wongofu wetu ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wawe waaminifu kwa wito wao wa kikuhani ee Bwana
Uwajalie mapadre wote, ili mikono yao ibariki na kuponya ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wawake moto wa mapendo yako ee Bwana
Uwajalie mapadre wote hatua zao zote ziwe kwa ajili ya utukufu wa Mungu ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wajazwe na Roho Mtakatifu na uwajalie karama zake kwa wingi ee Bwana.





Tuombe.
Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, usikie sala tunazokutolea kwa ajili ya mapadre wetu. Uwajalie wafahamu waziwazi kazi uliyowaitia kuifanya, uwape neema zote wanazohitaji ili waitikie wito wako kwa ushujaa, kwa upendo, na majitoleo yenye udumifu katika mapenzi yako matakatifu. Amina.


AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Lucy Mushi (Guest) on September 21, 2017

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

David Kawawa (Guest) on August 16, 2017

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Lydia Mzindakaya (Guest) on May 22, 2017

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Grace Njuguna (Guest) on February 19, 2017

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Vincent Mwangangi (Guest) on January 17, 2017

Mwamini katika mpango wake.

Raphael Okoth (Guest) on December 8, 2016

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Esther Nyambura (Guest) on October 31, 2016

Imani inaweza kusogeza milima

Anna Malela (Guest) on April 21, 2016

Dumu katika Bwana.

Francis Mtangi (Guest) on April 5, 2016

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Jane Malecela (Guest) on January 24, 2016

πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu

Frank Sokoine (Guest) on December 24, 2015

πŸ™βœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe

Betty Akinyi (Guest) on December 8, 2015

πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe

Stephen Kikwete (Guest) on December 2, 2015

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Joyce Mussa (Guest) on November 17, 2015

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Mary Mrope (Guest) on October 11, 2015

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

David Nyerere (Guest) on September 28, 2015

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Francis Mtangi (Guest) on August 28, 2015

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

Janet Mbithe (Guest) on August 1, 2015

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Lucy Mushi (Guest) on July 5, 2015

Rehema zake hudumu milele

Thomas Mwakalindile (Guest) on June 27, 2015

πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo

Joseph Kawawa (Guest) on June 26, 2015

Katika imani, yote yanawezekana

Charles Mboje (Guest) on May 4, 2015

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Stephen Kangethe (Guest) on April 23, 2015

πŸ™πŸ™πŸ™

Related Posts

Kanuni ya imani

Kanuni ya imani

Nasadiki kwa Mungu, Baba Mwenyezi,/ mwumba mbingu na dunia./ Na kwa Yesu Kristu, Mwanaye wa pekee... Read More

SALA KWA MT. YOSEFU KWA AJILI YA KULIOMBEA KANISA LA MAHUJAJI

SALA KWA MT. YOSEFU KWA AJILI YA KULIOMBEA KANISA LA MAHUJAJI

Ee Mtukufu Mt. Yosefu, ulichaguliwa na Mungu kuwa Baba Mlishi wa Yesu, mchumba safi kabisa wa Mar... Read More

SALA YA KUMWOMBA MTAKATIFU TERESIA WA MTOTO YESU

SALA YA KUMWOMBA MTAKATIFU TERESIA WA MTOTO YESU

Ee Mtakatifu Teresia wa mtoto Yesu, ulistahili kuitwa Msimamizi wa misioni katoliki za dunia yote... Read More

Novena ya Noeli

Novena ya Noeli

Novena ya Noeli (maarufu kama novena ya Mt. Andrea)

Husaliwa kuanzia tar 30 Nov hadi usiku ... Read More

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

Ee Yesu Mfungwa wa Upendo wa Mungu,/ ninapofikiri Upendo wako na jinsi ulivyojitolea kwa ajili ya... Read More

SALA YA UHAI KWA MT. YOSEFU

SALA YA UHAI KWA MT. YOSEFU

(Sala hii inafaa sana kwa ajili ya kutetea uhai wa watoto wachanga wakiwa tumboni mwa mama za... Read More

Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema

Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema

Read More

SALA KWA MTAKATIFU YUDA TADEI

SALA KWA MTAKATIFU YUDA TADEI

Mtakatifu Yuda Tadei,/ Mtume Mtakatifu,/ mtumishi mwaminifu na rafiki wa Yes... Read More

SALA KWA MALAIKA WAKO MLINZI

SALA KWA MALAIKA WAKO MLINZI

Malaika wa Mungu Mlinzi wangu mpenzi,
Ambaye upendo wake unanifanya niwepo hapa,
Uwe na... Read More

SALA YA MTU ALIYEKABILIWA NA MATATIZO MBALIMBALI

SALA YA MTU ALIYEKABILIWA NA MATATIZO MBALIMBALI

Ewe Mtakatifu Yuda Tadei,/ mtume mtukufu na shahidi wa Kristo,/ umesifika pote kwa wepesi wako wa... Read More

Kuweka nia njema

Kuweka nia njema

Kumheshimu Mungu wangu, Namtolea roho yangu, Nifanye kazi nipumzike, Amri zake tu nishike, Wazo n... Read More

Sala ya Malaika wa Bwana

Sala ya Malaika wa Bwana

Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria, naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Salamu M... Read More