Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
☰
AckyShine

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

Featured Image

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji mwema
Kwa ajili ya makardinali na maaskofu wakuu; Uwape moyo wa kichungaji ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wa majimbo; Uwajaze na Roho wako ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre watawa; Wakamilishe katika wito wao ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre walioko hatarini; Uwaokoe ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wenye udhaifu; Uwatie nguvu ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wenye hofu; Uwape amani ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre waliokata tamaa; Uwavuvie upya ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wakaao upweke; Uwasindikize ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wamisionari; Uwalinde ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wanaohubiri; Uwaangazie ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre na watawa waliokufa; Uwafikishe kwenye utukufu wako ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wote; Wajalie hekima na ufahamu wako ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wote; Uwajalie elimu na shauri lako
Kwa ajili ya mapadre wako; wajalie wakuheshimu na wakuogope
Kwa ajili ya mapadre wote; Wajalie subira na upendo
Kwa ajili ya mapadre wote; wajalie utii na upole
Kwa ajili ya mapadre wote; uwajalie hamu kuu ya kuokoa roho za watu
Kwa ajili ya mapadre wote; wape fadhila za imani, matumaini na mapendo
Kwa ajili ya mapadre wote; Wajalie upendo mkuu kwa Ekaristi
Tunakuomba uwajalie mapadre wote; Waheshimu uhai na hadhi ya mtu ee Bwana
Tunakuomba uwajalie mapadre wote nguvu na bidii katika kazi zao ee Bwana
Tunakuomba uwajalie mapadre wote amani katika mahangaiko yao ee Bwana
Tunakuomba uwajalie mapadre wote upendo mkuu kwa Utatu Mtakatifu ee Bwana
Tunakuomba uwajalie mapadre wote upendo mkuu kwa Bikira Maria ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wawe mwanga wa Kristo ee Bwana
Uwajalie mapadre wote, wawe chumvi kwa ulimwengu ee Bwana
Uwajalie mapadre wote, wajizoeze kujitoa sadaka na kujinyima ee Bwana
Uwajalie mapadre wote, wawe watakatifu kimwili, kiakili na kiroho ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wawe watu wa sala ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wawe kioo cha imani kwako ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wajali sana wongofu wetu ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wawe waaminifu kwa wito wao wa kikuhani ee Bwana
Uwajalie mapadre wote, ili mikono yao ibariki na kuponya ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wawake moto wa mapendo yako ee Bwana
Uwajalie mapadre wote hatua zao zote ziwe kwa ajili ya utukufu wa Mungu ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wajazwe na Roho Mtakatifu na uwajalie karama zake kwa wingi ee Bwana.





Tuombe.
Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, usikie sala tunazokutolea kwa ajili ya mapadre wetu. Uwajalie wafahamu waziwazi kazi uliyowaitia kuifanya, uwape neema zote wanazohitaji ili waitikie wito wako kwa ushujaa, kwa upendo, na majitoleo yenye udumifu katika mapenzi yako matakatifu. Amina.


AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Lucy Mushi (Guest) on September 21, 2017

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

David Kawawa (Guest) on August 16, 2017

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Lydia Mzindakaya (Guest) on May 22, 2017

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Grace Njuguna (Guest) on February 19, 2017

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Vincent Mwangangi (Guest) on January 17, 2017

Mwamini katika mpango wake.

Raphael Okoth (Guest) on December 8, 2016

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Esther Nyambura (Guest) on October 31, 2016

Imani inaweza kusogeza milima

Anna Malela (Guest) on April 21, 2016

Dumu katika Bwana.

Francis Mtangi (Guest) on April 5, 2016

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Jane Malecela (Guest) on January 24, 2016

πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu

Frank Sokoine (Guest) on December 24, 2015

πŸ™βœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe

Betty Akinyi (Guest) on December 8, 2015

πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe

Stephen Kikwete (Guest) on December 2, 2015

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Joyce Mussa (Guest) on November 17, 2015

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Mary Mrope (Guest) on October 11, 2015

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

David Nyerere (Guest) on September 28, 2015

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Francis Mtangi (Guest) on August 28, 2015

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

Janet Mbithe (Guest) on August 1, 2015

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Lucy Mushi (Guest) on July 5, 2015

Rehema zake hudumu milele

Thomas Mwakalindile (Guest) on June 27, 2015

πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo

Joseph Kawawa (Guest) on June 26, 2015

Katika imani, yote yanawezekana

Charles Mboje (Guest) on May 4, 2015

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Stephen Kangethe (Guest) on April 23, 2015

πŸ™πŸ™πŸ™

Related Posts

Sala ya kuomba Kifo chema

Sala ya kuomba Kifo chema

Enyi Yesu na Maria na Yosefu,

nawatolea Moyo, na roho, na uzima wangu.

Enyi Yesu na M... Read More

SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

Ee Yesu Kristu,/ Bwana wangu na Mungu wangu/ ambaye ninasadiki kuwa upo hapa/ katika Sakramenti T... Read More

Kuweka nia njema

Kuweka nia njema

Kumheshimu Mungu wangu, Namtolea roho yangu, Nifanye kazi nipumzike, Amri zake tu nishike, Wazo n... Read More

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

Ee Bwana Yesu Kristo. Mkombozi wetu, kwa mapendo na tamaa yako ya kutaka kulinda vema Kanisa lako... Read More

Sala kwa Mtakatifu Yosefu

Sala kwa Mtakatifu Yosefu

Ee Yosef mwenye heri, tunakimbilia kwako, katika masumbuko yetu, na kishaomba shime ya Mchumba wa... Read More

SALA YA MAPENDO

SALA YA MAPENDO

Mungu wangu,

nakupenda zaidi ya cho chote,

kwani ndiwe mwema,

ndiwe mwenye kupe... Read More

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU I

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU I

Utukuzwe ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Uliagua kifo chako./ Katika karamu ya mwisho ulitumia mkate... Read More

Sala ya Usiku kabla ya kulala

Sala ya Usiku kabla ya kulala

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

SALA YA KUSHUKURU

Tunakus... Read More

Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema

Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema

Read More

SALA YA MATUMAINI

SALA YA MATUMAINI

Mungu wangu,

natumaini kwako nitapewa kwa njia ya Yesu Kristu,

neema zako duniani na ... Read More

SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI

SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI

Mama Mtakatifu, Mama wa Mungu na Malkia wa Mashahidi, leo nakuchagua Wewe uwe mfano wangu, mkinga... Read More

LITANIA YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

LITANIA YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie ... Read More