Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
☰
AckyShine

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

Featured Image

Ee Bwana Yesu Kristo. Mkombozi wetu, kwa mapendo na tamaa yako ya kutaka kulinda vema Kanisa lako, ukachagua Mapadri wawe Wachungaji na Viongozi wa roho za watu. Nakuomba sana; ubariki nia na bidii inayowapasa Mapadri wote katika kazi zao. Uwaongezee Utakatifu.

Uwatie moyo mzuri wenye mapendo makubwa kwako na roho za watu. Hivyo wakiisha kupata wenyewe Utakatifu, waweze kuwaongoza vizuri watu walio chini ya ulinzi wao, katika njia ya Utakatifu na furaha ya milele. Uwajalie neema zote za hali ya Upadri. Uwajalie ili waonyeshe kila siku ya maisha yao mfano wa kila fadhila ya mapendo na ya uaminifu katika Kanisa, kwa Baba Mtakatifu na kwa Maaskofu.

Yesu mpendelevu, uangalie kwa mapendo kazi na mateso ya Mapadri wako; ubariki na ustawishe mafundisho yao; wanapowafundisha watoto, wanapowahubiria watu, wanapowatuliza wakosefu watubu na wanapowasaidia wagonjwa na wale wanaokaribia mauti, Ee Yesu uwe pamoja nao. Uwakinge na hatari zote za roho na za mwili.

Mwokozi Yesu, ulijalie Kanisa liwe na Mapadri wengi walio Watakatifu. Uwajalie watoto na vijana wengi wasikie wito wa Upadri, uwatie furaha na Utakatifu na roho za Mapadri waliokufa uzijalie punziko la amani.

Kwa mimi mwenyewe Ee Yesu mpendelevu, naomba unijalie roho ya imani na utii mnyenyekevu ili niwaheshimu Mapadri kama Mawakili wa Mungu. Niwatii katika njia zote za wokovu wa roho yangu. Amina.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Faith Kariuki (Guest) on August 20, 2017

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Nancy Kabura (Guest) on August 16, 2017

πŸ™πŸ™πŸ™

Elizabeth Mtei (Guest) on July 17, 2017

πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka

Sarah Achieng (Guest) on June 22, 2017

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Peter Mwambui (Guest) on June 12, 2017

πŸ™β€οΈ Mungu akubariki

Grace Majaliwa (Guest) on May 23, 2017

Neema ya Mungu inatosha kwako

Lucy Mushi (Guest) on March 29, 2017

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Anna Sumari (Guest) on December 31, 2016

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Peter Mwambui (Guest) on November 5, 2016

πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha

James Malima (Guest) on October 31, 2016

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Irene Akoth (Guest) on August 5, 2016

πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku

James Malima (Guest) on July 24, 2016

Baraka kwako na familia yako.

Joyce Nkya (Guest) on July 5, 2016

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Grace Mushi (Guest) on May 17, 2016

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Grace Njuguna (Guest) on May 9, 2016

πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu

Christopher Oloo (Guest) on February 17, 2016

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Mary Kendi (Guest) on January 6, 2016

Tumaini ni nanga ya roho

John Lissu (Guest) on January 6, 2016

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Agnes Lowassa (Guest) on November 14, 2015

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Sharon Kibiru (Guest) on September 4, 2015

πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai

Anna Mahiga (Guest) on July 11, 2015

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Irene Makena (Guest) on June 28, 2015

πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu

Joseph Njoroge (Guest) on June 7, 2015

Rehema hushinda hukumu

Related Posts

Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania

Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania

Anza Novena hii tarehe 19 Agosti ili kumalizia tarehe 27 Agosti na kush... Read More

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU I

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU I

Utukuzwe ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Uliagua kifo chako./ Katika karamu ya mwisho ulitumia mkate... Read More

AMRI ZA KANISA

AMRI ZA KANISA

1. HUDHURIA MISA TAKATIFU DOMINIKA NA SIKUKUU ZILZOAMRIWA

2. FUNGA SIKU YA JUMATANO YA MAJI... Read More

Sala ya Usiku kabla ya kulala

Sala ya Usiku kabla ya kulala

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

SALA YA KUSHUKURU

Tunakus... Read More

SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU

SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU

Sali Atukuzwe 7 kwa heshima ya Malaika 7 wateule ujipatie neema ya kuepa dhambi mbaya saba na kut... Read More

Sala fupi ya Asubuhi

Sala fupi ya Asubuhi

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, milele na milele, Amina... Read More

Sala kwa wenye kuzimia

Sala kwa wenye kuzimia

Ee Yesu mwenye huruma, mpenda roho za watu, nakuomba kwa ajili ya kuzimia kwa Moyo wako Mtakatifu... Read More

SALA YA MATUMAINI

SALA YA MATUMAINI

Mungu wangu,

natumaini kwako nitapewa kwa njia ya Yesu Kristu,

neema zako duniani na ... Read More

Matendo ya Rozari Takatifu: Mchanganuo kwa siku zote za Saba za Juma

Matendo ya Rozari Takatifu: Mchanganuo kwa siku zote za Saba za Juma

MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)

Read More