Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
☰
AckyShine

SALA YA KUOMBEA FAMILIA

Featured Image

Ewe Mungu Mwenyezi, sisi kama familia tunakushukuru kwa zawadi ya Mama Kanisa Katoliki ambaye siku zote hutupatia malezi bora kwa ajili ya wokovu wetu. Kanisa halichoki kutuhimiza tutafakari na kuishi utakatifu wa familia ya Nazareti ya Yesu, Maria na Yosefu. Familia hii iliishi upendo uliojengwa kwa fadhila za imani, uaminifu, utii, uvumilivu na upole hata wakawa watakatifu. Tunapoadhimisha mwaka wa Familia, tunaiweka mbele yetu familia ya Nazareti iwe dira, baraka na mfano kwa familia zetu.

Tunakushukuru Baba kwa ajili ya familia zote zinazojitahidi kuishi fadhila hizo za Familia takatifu na tunakuomba uzidi kuwaimarisha wanandoa ili tupate kwao mifano mingi na bora ya kuigwa. Ee Bwana, tunaomba Roho Mtakatifu atuangazie tuweze: kutambua familia kuwa Kanisa la nyumbani na shule ya imani na upendo; kuimarisha familia kwa sala, sakramenti na tunu za kiinjili na kushirikiana kwa heshima katika familia kwa usitawi wa roho na wa mwili kwa wanafamilia wote.

Tunaziombea familia zetu na Jumuiya Ndogondogo za Kikristo ziwe bustani bora na salama za kuchipusha na kulea miito mitakatifu ya Ndoa, Utawa na Upadre. Tunawaombea vijana na watoto wetu Uchaji wa Mungu ili wawe na bidii ya kujitunza kwa kushika amri za Mungu na kuishi fadhila za kiinjili, wawe na roho ya kimisionari yaani walipende Kanisa na kuwa na moyo wa kueneza ufalme wako kwa matendo ya imani. Baba wa huruma, tunakukabidhi familia zenye misukosuko ya mafarakano, ulevi, ubinafsi, uregevu-dini, uvivu, ushirikina, hofu, magonjwa sugu na mengineyo yenye kuleta huzuni; kwa hisani yako uwape neema, mwanga na nguvu za kuanza maisha mapya yenye amani, waweze kufurahia upatanisho na uponyi wa pendo lako la kibaba kati yao.

Tunaomba toba na msamaha kwa ukatili, manyanyaso na hata mauaji katika familia zetu na uwaponye wote waliojeruhiwa kwa maneno, matendo na makwazo ya aina yeyote. Aidha tunakuomba uwe kitulizo na faraja kwa wagonjwa na wazee, pia tegemeo la yatima na wajane. Wenye matatizo ya kiafya au ya kijamii wasikate tamaa bali waunganishe hali zao na msalaba wa Mwanao na kukutumaini wewe Mweza yote. Jamii iwajibike nao kwa kuzijali haki zao na kuwapa misaada wanayohitaji.

Tunakuomba ubariki miradi na kazi zetu ili familia zipate usitawi na maendeleo; na utujalie hekima ya kukushukuru kwa maisha ya haki, amani na ukarimu na mwisho tukaimbe sifa zako pamoja na familia Takatifu ya Yesu, Maria na Yosefuna jeshi lote la mbinguni. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.

Baba yetu… …..Salamu Maria….…Atukuzwe Baba………

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Anthony Kariuki (Guest) on September 12, 2017

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Joseph Kawawa (Guest) on September 4, 2017

πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe

Nancy Kabura (Guest) on July 12, 2017

πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie

Chris Okello (Guest) on March 29, 2017

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Joseph Kitine (Guest) on March 21, 2017

πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu

Benjamin Masanja (Guest) on March 14, 2017

Mwamini Bwana; anajua njia

Janet Sumari (Guest) on January 10, 2017

πŸ™β€οΈ Mungu akubariki

Simon Kiprono (Guest) on December 30, 2016

πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani

Janet Mwikali (Guest) on July 26, 2016

Rehema zake hudumu milele

Grace Mushi (Guest) on July 11, 2016

πŸ™πŸ™πŸ™

James Kawawa (Guest) on May 7, 2016

Sifa kwa Bwana!

Charles Mboje (Guest) on March 3, 2016

Imani inaweza kusogeza milima

Joseph Kitine (Guest) on October 19, 2015

πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose

Grace Majaliwa (Guest) on October 3, 2015

πŸ™βœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe

Ann Awino (Guest) on October 2, 2015

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Nuru (Guest) on September 8, 2015

πŸ™πŸ™πŸ™

David Musyoka (Guest) on August 15, 2015

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Grace Mushi (Guest) on July 22, 2015

πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu

Grace Minja (Guest) on June 17, 2015

Baraka kwako na familia yako.

Elizabeth Malima (Guest) on June 10, 2015

πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai

Alex Nyamweya (Guest) on May 18, 2015

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Elizabeth Malima (Guest) on May 16, 2015

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Joseph Mallya (Guest) on April 3, 2015

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Related Posts

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji ... Read More

SALA KWA MT. YOSEFU KWA WASIO NA AJIRA WAPATE AJIRA

SALA KWA MT. YOSEFU KWA WASIO NA AJIRA WAPATE AJIRA

Ee Mt. Yosefu, tunakuomba kwa ajili ya wale asio na ajira, kwa ajili ya wale wanaotaka kujipatia ... Read More

SALA KWA MTAKATIFU YUDA TADEI

SALA KWA MTAKATIFU YUDA TADEI

Mtakatifu Yuda Tadei,/ Mtume Mtakatifu,/ mtumishi mwaminifu na rafiki wa Yes... Read More

Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema

Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema

Read More

Sala ya Kuombea Hali njema ya hewa na mvua

Sala ya Kuombea Hali njema ya hewa na mvua

Ee Mungu Mwenyezi wa milele, mpaji wa mema yote, unayetusamehe na kutulinda. Utujalie sisi tunaok... Read More

SALA YA UHAI KWA MT. YOSEFU

SALA YA UHAI KWA MT. YOSEFU

(Sala hii inafaa sana kwa ajili ya kutetea uhai wa watoto wachanga wakiwa tumboni mwa mama za... Read More

ROZARI, MATENDO NA LITANI YA MAMA BIKIRA MARIA

ROZARI, MATENDO NA LITANI YA MAMA BIKIRA MARIA

Read More
SALAMU MARIA

SALAMU MARIA

Salamu Maria
Umejaa neema
Bwana yu nawe
Umebarikiwa kuliko wanawake wote
Na Y... Read More

Sala kwa wenye kuzimia

Sala kwa wenye kuzimia

Ee Yesu mwenye huruma, mpenda roho za watu, nakuomba kwa ajili ya kuzimia kwa Moyo wako Mtakatifu... Read More

Sala ya Malaika wa Bwana

Sala ya Malaika wa Bwana

Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria, naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Salamu M... Read More

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo na mafungu 7 yaani mateso 7 yenye Salamu Maria... Read More

SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE

SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE

Nakusikitikia sana Mama Mtakatifu Maria kwa sababu ya ukiwa wako mkuu. Uchungu wako ulikuwa mkubw... Read More