Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
☰
AckyShine

ROSARI YA BIKIRA MARIA MAMA WA MSAADA WA DAIMA

Featured Image

Namna ya kusali Rozari kwa Bikira Maria Mama wa Msaada wa Daima

(Tumia rosari ya kawaida)

Mwanzo, kwenye Msalaba:

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

Kwenye chembe ndogo za awali:

K: Ee Mungu utuelekezee msaada W: Ee Bwana utusaidie hima
W: Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu,
Kama mwanzo na sasa na siku zote na milele. Amina.

Maria ametusaidia,
Maria anataka kutusaidia,
Maria anaweza kutusaidia,
Maria atatusaidia.

KATIKA KILA FUNGU SALI SALA ZIFUATAZO:

Kwenye chembe kubwa:

Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu,
Kama mwanzo na sasa, na siku zote, na milele. Amina.

Maria ametusaidia,
Maria anataka kutusaidia,
Maria anaweza kutusaidia,
Maria atatusaidia.

Ee Maria Mama wa Msaada wa daima
Sikiliza maombi ya roho zetu
Unaweza kutusaidia katika mahitaji yetu
Ee Maria kwa matumaini twakuita wewe.

Kwenye chembe ndogo:

Kama unasali mwenyewe: β€œEe Maria, utusaidie! (mara kumi)
Kama mnasali zaidi ya mmoja kwa pamoja: K; Ee Maria, W: Utusaidie. (mara kumi)

MWISHO SALI SALA ZIFUATAZO:

Salamu Maria

Salamu Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe, umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu Mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu, sasa, na saa ya kufa kwetu. Amina. (mara tatu)

Tunaukimbilia

Tunaukimbilia ulinzi wako, ee Mzazi Mtakatifu wa Mungu, usitunyime tukiomba katika shida zetu, utuokoe siku zote, kila tuingiapo hatarini, ee Bikira Mtukufu na mwenye baraka,. Amina.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Agnes Lowassa (Guest) on September 20, 2017

πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha

Anna Malela (Guest) on September 6, 2017

πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu

John Malisa (Guest) on August 23, 2017

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Sarah Karani (Guest) on August 19, 2017

πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri

Anna Mahiga (Guest) on June 24, 2017

Neema na amani iwe nawe.

Richard Mulwa (Guest) on June 22, 2017

Imani inaweza kusogeza milima

Samuel Were (Guest) on March 25, 2017

πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu

Victor Sokoine (Guest) on March 16, 2017

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

John Malisa (Guest) on January 3, 2017

πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe

Edith Cherotich (Guest) on December 4, 2016

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Bernard Oduor (Guest) on December 4, 2016

πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu

Moses Kipkemboi (Guest) on September 4, 2016

πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike

Anna Mchome (Guest) on August 21, 2016

πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi

Joseph Kitine (Guest) on August 19, 2016

Nakuombea πŸ™

Peter Mbise (Guest) on May 10, 2016

πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani

Samuel Omondi (Guest) on February 26, 2016

Endelea kuwa na imani!

Alice Jebet (Guest) on January 16, 2016

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Diana Mallya (Guest) on December 31, 2015

πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua

Robert Okello (Guest) on October 8, 2015

πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu

John Lissu (Guest) on July 31, 2015

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Catherine Mkumbo (Guest) on May 29, 2015

Neema ya Mungu inatosha kwako

Joseph Njoroge (Guest) on May 9, 2015

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Sarah Mbise (Guest) on April 17, 2015

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Related Posts

SALA ZA KUMWABUDU YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA ZA KUMWABUDU YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

Ee Yesu Kristu,/ Bwana wangu na M... Read More

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU II

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU II

Yesu, Mungu wangu mpenzi,/ upo hapa katika Altare mbele yangu;/ na mimi napiga magoti mbele yako.... Read More

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo na mafungu 7 yaani mateso 7 yenye Salamu Maria... Read More

Sala ya Malaika wa Bwana

Sala ya Malaika wa Bwana

Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria, naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Salamu M... Read More

SALA YA BWANA: SALA YA BABA YETU

SALA YA BWANA: SALA YA BABA YETU

Baba yetu uliye mbinguni
Jina lako litukuzwe
Ufalme wako ufike
Utakalo lifanyikeRead More

ROZARI YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

ROZARI YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Tumia tasbihi ya kawaida yenye chembe ndogo 53.

Kwenye Msalaba Sali:

... Read More
AMRI ZA MUNGU

AMRI ZA MUNGU

1. NDIMI BWANA MUNGU WAKO, USIABUDU MIUNGU WENGINE.
2. USILITAJE BURE JINA LA MUNGU WAKO.Read More

ATUKUZWE BABA

ATUKUZWE BABA

Atukuzwe Baba
na Mwana
na Roho Mtakatifu
Kama mwanzo
na sasa,
na siku zo... Read More

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

Ee Bwana Yesu Kristo. Mkombozi wetu, kwa mapendo na tamaa yako ya kutaka kulinda vema Kanisa lako... Read More

Sala fupi ya Asubuhi

Sala fupi ya Asubuhi

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, milele na milele, Amina... Read More

Majitoleo ya asubuhi kwa Bikira Maria

Majitoleo ya asubuhi kwa Bikira Maria

Ee Yesu, kupitia mikono safi ya Bikira Maria, na kwa maungano na sadaka yako kuu, ninakutolea sal... Read More

Sala kwa wenye kuzimia

Sala kwa wenye kuzimia

Ee Yesu mwenye huruma, mpenda roho za watu, nakuomba kwa ajili ya kuzimia kwa Moyo wako Mtakatifu... Read More