Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
☰
AckyShine

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

Featured Image

Ee Yesu Mfungwa wa Upendo wa Mungu,/ ninapofikiri Upendo wako na jinsi ulivyojitolea kwa ajili yangu,/ nashindwa kuelewa./ Unaficha Ukuu wako usiofahamika/ na kujidhihirisha kwa ajili yangu mimi mnyonge./ Ee Mfalme wa utukufu,/ unaficha uzuri wako,/ lakini jicho la moyo wangu/ linapenya pazia na kuona Majeshi ya Malaika/ wakikuimbia kwa heshima bila kukoma/ na nguvu zote mbinguni zikikusifu bila mwisho zikisema:/ β€œMtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu..”/

Ni nani awezaye kufahamu Upendo wako/ na huruma yako isiyo na kipimo kwa ajili yetu!/ Ee Mfungwa wa Upendo,/ nafungia moyo wangu masikini/ kwenye Tabarnakulo hii/ ili niweze kukuabudu usiku na mchana bila mwisho./ Najua hakuna kizuizi/ na hata kama naonekana kukaa mbali,/ lakini moyo wangu u pamoja nawe/ katika ibada hii./ Hakuna kinachoweza kuzuia upendo wangu kwako./ Kwangu hakuna kizuizi chochote./

Ee Utatu Mtakatifu,/ Mungu Mmoja usiyegawanyika,/ utukuzwe kwa zawadi yako hii kuu/ na agano hili la huruma!/

Nakuabudu,/ Bwana na Muumba uliyefichika katika Sakramenti Takatifu!/ Ee Bwana,/ nakuabudu kwa kazi zote za mikono yako/ zinazonifunulia Hekima yako kuu,/ Wema wako na Huruma yako kuu./ Uzuri uliousambaza hapa/ Uzuri ulio nao Wewe mwenyewe/ ambaye U Uzuri usioelezeka;/ na ingawaje umejificha na kusitiri uzuri wako,/ jicho langu,/ kwa mwanga wa imani linafika kwako,/ na roho yangu inapata kumtambua Muumba wake/ aliye Uzuri usiopimika,/ ulio juu ya kila uzuri,/ na moyo wangu unazama kabisa katika sala ya kukuabudu./

Bwana wangu na Muumba wangu,/ wema wako wanitia moyo wa kuongea nawe,/ Huruma yako huondoa kiambaza/ kitenganishacho Muumba na kiumbe./ Furaha ya moyo wangu,/ ee Mungu, ni kuongea na Wewe./ Yote ambayo moyo wangu unayatamni nayapata kwako./ Hapa ndipo mwanga wako unaponiangaza akili yangu/ na kuiwezesha kukujua Wewe zaidi na zaidi/ – ndipo mikondo ya neema inapoutiririkia moyo wangu,/ ndipo roho yangu inapochota uzima wa milele./ Ee Bwana na Muumba wangu,/ licha ya mapaji yote haya,/ unajitoa mwenyewe kwangu,/ ili uweze kujiunganisha na kiumbe dhaifu na maskini./

Ee Kristu,/ nafurahi sana nionapo kwamba unapendwa/ na kwamba sifa na utukufu wako vinaongezwa/ hasa ya Huruma yako./ Ee Kristu,/ sitaacha kamwe kuutukuza wema wako na huruma yako,/ hadi dakika ya mwisho ya maisha yangu./ Kwa kila tone la damu yangu/ na kwa kila pigo la moyo wangu/ naitukuza Huruma yako./ Natamani kugeuzwa kabisa/ na kuwa utenzi wa utukufu wako./ Naomba siku ya kufa kwangu/ popote nitakapokuwa nimelala,/ pigo la mwisho la moyo wangu/ liwe utenzi mpendevu/ usifuo Huruma yako isiyo na kipimo./ Amina

(Na Mt. Faustina Kowalska).

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Nora Kidata (Guest) on September 3, 2018

πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu

Janet Mwikali (Guest) on August 29, 2018

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Hellen Nduta (Guest) on August 13, 2018

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Peter Mugendi (Guest) on May 3, 2018

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Victor Malima (Guest) on February 27, 2018

πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie

Anna Malela (Guest) on December 10, 2017

Neema ya Mungu inatosha kwako

George Mallya (Guest) on November 16, 2017

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Irene Makena (Guest) on July 16, 2017

Mwamini katika mpango wake.

Peter Mugendi (Guest) on June 7, 2017

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Sarah Karani (Guest) on March 20, 2017

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Nicholas Wanjohi (Guest) on February 4, 2017

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Catherine Naliaka (Guest) on January 2, 2017

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Joseph Kitine (Guest) on November 15, 2016

πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose

Mary Njeri (Guest) on October 15, 2016

πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe

Mercy Atieno (Guest) on July 23, 2016

πŸ™βœ¨πŸ’– Mungu atajibu maombi yako

Nancy Akumu (Guest) on May 11, 2016

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Anthony Kariuki (Guest) on May 9, 2016

πŸ™πŸ™πŸ™

Nancy Kabura (Guest) on April 26, 2016

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Margaret Anyango (Guest) on February 9, 2016

πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote

Mary Njeri (Guest) on December 15, 2015

Sifa kwa Bwana!

John Mwangi (Guest) on November 1, 2015

Nakuombea πŸ™

Diana Mumbua (Guest) on July 8, 2015

πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi

Peter Mbise (Guest) on May 1, 2015

πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe

Related Posts

Sala kwa Mtakatifu Yosefu

Sala kwa Mtakatifu Yosefu

Ee Yosef mwenye heri, tunakimbilia kwako, katika masumbuko yetu, na kishaomba shime ya Mchumba wa... Read More

SALA KWA MT. YOSEFU KWA WASIO NA AJIRA WAPATE AJIRA

SALA KWA MT. YOSEFU KWA WASIO NA AJIRA WAPATE AJIRA

Ee Mt. Yosefu, tunakuomba kwa ajili ya wale asio na ajira, kwa ajili ya wale wanaotaka kujipatia ... Read More

SALA KWA MAMA WA UCHUNGU KUOMBA NEEMA YA PEKEE

SALA KWA MAMA WA UCHUNGU KUOMBA NEEMA YA PEKEE

Ee Mama mbarikiwa na Bikira mwenye uchungu, Malkia wa Mashahidi, uliyesimama chini ya msalaba na ... Read More

Litani ya Bikira Maria

Litani ya Bikira Maria

  • Bwana utuhurumie
  • Bwana utuhurumie
  • Kristo utuhurumie
  • Bwana utuhurumie... Read More
SALA YA JIONI

SALA YA JIONI

TUNAKUSHUKURU, EE MUNGU KWA MAPAJI YOTE ULIYOTUJALIA LEO AMINA


BABA YETU…………β... Read More

ATUKUZWE BABA

ATUKUZWE BABA

Atukuzwe Baba
na Mwana
na Roho Mtakatifu
Kama mwanzo
na sasa,
na siku zo... Read More

Sala ya Usiku kabla ya kulala

Sala ya Usiku kabla ya kulala

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

SALA YA KUSHUKURU

Tunakus... Read More

Majitoleo ya Asubuhi

Majitoleo ya Asubuhi

Ee Baba yetu Mungu Mkuu, Umenilinda usiku huu, Ninakushukuru kwa moyo, Ee Baba, Mwana na Roho, Ni... Read More

KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU

KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU

Ee Mt. Yosefu, Baba Mlishi wa Mwokozi wangu, na mchumba safi wa Mama wa Mungu, leo ninakuchagua w... Read More

SALA KWA MT. YOSEFU KWA AJILI YA KULIOMBEA KANISA LA MAHUJAJI

SALA KWA MT. YOSEFU KWA AJILI YA KULIOMBEA KANISA LA MAHUJAJI

Ee Mtukufu Mt. Yosefu, ulichaguliwa na Mungu kuwa Baba Mlishi wa Yesu, mchumba safi kabisa wa Mar... Read More

SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI

SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI

Mama Mtakatifu, Mama wa Mungu na Malkia wa Mashahidi, leo nakuchagua Wewe uwe mfano wangu, mkinga... Read More

SALA YA MAPENDO

SALA YA MAPENDO

Mungu wangu,

nakupenda zaidi ya cho chote,

kwani ndiwe mwema,

ndiwe mwenye kupe... Read More