Alichofanya mke baada ya mme wake kupenda kumchunga sana
Alifanya hivi; Siku ya kwanza
MUME: Halooo vipi mke wangu salama weye?. MKE: Salama tu MUME: Uko wapi? MKE: Jamani si niko nyumbani MUME: Mhh kama kweli uko nyumbani washa blender nisikie…..mke akawasha blender MKE: Umesikia? MUME: Okay haya mi natoka kazini naja
Updated at: 2023-04-29 22:53:52 (2 years ago by Melkisedeck Leon Shine)
Alifanya hivi; Siku ya kwanza
MUME: Halooo vipi mke wangu salama weye?. MKE: Salama tu MUME: Uko wapi? MKE: Jamani si niko nyumbani MUME: Mhh kama kweli uko nyumbani washa blender nisikie…..mke akawasha blender MKE: Umesikia? MUME: Okay haya mi natoka kazini naja
Siku ya pili MUME: Vipi mko salama huko? MKE: Tupo kama ulivyotuacha MUME: kwani uko wapi? MKE: Niko nyumbani napika MUME: Washa brender kama kweli uko nyumbani Mke akawasha blender MKE: Umesikia? MUME: Poa ntarudi baada ya masaa mawili
Siku sita baadae mume akaamua kurudi bila kumtaarifu mkewe alipofika home kamkuta mdada wa kazi yuko peke yake. MUME: We mama yako yuko wapi? MDADA: Sijui ameondoka na blender toka asubuhi
Jambazi mmoja aliingia kanisani na bunduki akapiga risasi juu ya bati akasema "asiyempenda YESU atoke nje" wakatoka wote ispokuwa Mchungaji na Wazee wawili.
Updated at: 2024-05-25 18:07:09 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Jambazi mmoja aliingia kanisani na bunduki akapiga risasi juu ya bati akasema "asiyempenda YESU atoke nje" wakatoka wote ispokuwa Mchungaji na Wazee wawili.
Jambazi likamwambia Mchungaji "unaweza kuendelea na ibada, nilikuwa nakuondolea wanafiki", Mchungaji akasema "ungewaacha kwanza nichukue sadaka…!
Cheki masifa yalivyomponza huyu, Sifa nyingine ni mbaya jamani
Mbongo, Mganda, na Mkenya walikamatwa na makosa Uchina.
Wakaambiwa adhabu ni ama kifo cha moja kwa moja au adhabu nyingine ambayo atakayeifaulu atakuwa huru, atakayeshindwa atauawa.
Basi wao wakaomba wapewe hiyo adhabu nyingine wajaribu bahati yao.
Wakapelekwa msituni wakaambiwa kila mmoja aende kwa njia yake halafu arudi na matunda kumi ya kufanana.
Updated at: 2024-05-25 18:01:48 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mbongo, Mganda, na Mkenya walikamatwa na makosa Uchina.
Wakaambiwa adhabu ni ama kifo cha moja kwa moja au adhabu nyingine ambayo atakayeifaulu atakuwa huru, atakayeshindwa atauawa.
Basi wao wakaomba wapewe hiyo adhabu nyingine wajaribu bahati yao.
Wakapelekwa msituni wakaambiwa kila mmoja aende kwa njia yake halafu arudi na matunda kumi ya kufanana.
Wakaingia msituni kila mtu njia yake.
… Mganda akarudi wa kwanza na machungwa kumi. Akaambiwa adhabu yake ni kumeza moja moja likiwa zima bila kufumba macho bila kulia wala kucheka wala kujitikisa mpaka yote kumi yaishe. Akameza la kwanza. Safi. Kumeza la pili, akashindwa kuvumilia akafumba macho. Akapigiwa risasi akafa.
Mkenya akaja. Ana vitunda vidogo vidogo kama pili vilaini. Akasomewa masharti. Akaanza kumeza bila kufumba macho wala kulia, wala nini… alipofika cha tisa akashindwa kuvumilia akaangua kicheko! Akapigwa risasi pia akafa.
Wakiwa kuzimu Mganda akamwuliza Mkenya, “Vipi, mbona ulishindwa kuvumilia wakati kilibaki kitunda kimoja tu?”
Mkenya akamjibu: “Mkuu, nilishindwa kuzuia kicheko maana nilimwona Mbongo anakuja na matikiti maji!”
Huu ndio mlolongo wa michepuko kuwahi kutokea kati ya mke, mume mwanafunzi na boss
BOSS anamwambia sekretari wake: Wiki hii tutaenda wote Serena Hotel kwenye mkutano fanya mipango yote.
SEKRETARI (anamuaga mumewe): Tunaenda na bosi Serena hotel kwenye mkutano for 1 week.
MUME (anampigia mpango wa kando): Mambo safi, wife anaenda kikazi Serena, jitayarishe tujipe raha for 1 week
(Mpango wa kando) anamwambia mwanafunzi wake wa tution: wiki hii nina kazi fulani hakuna tution mpaka week ijayo.
Updated at: 2023-04-29 22:53:20 (2 years ago by Melkisedeck Leon Shine)
BOSS anamwambia sekretari wake: Wiki hii tutaenda wote Serena Hotel kwenye mkutano fanya mipango yote. SEKRETARI (anamuaga mumewe): Tunaenda na bosi Serena hotel kwenye mkutano for 1 week. MUME (anampigia mpango wa kando): Mambo safi, wife anaenda kikazi Serena, jitayarishe tujipe raha for 1 week (Mpango wa kando) anamwambia mwanafunzi wake wa tution: wiki hii nina kazi fulani hakuna tution mpaka week ijayo. MWANAFUNZI anampigia simu sugar daddy wake ambaye ndo (BOSS): Dear hakuna tution wiki hii nakuja kwako…..
BOSS anamwambia sekretari wake: Siendi Serena tena coz mjukuu wangu atanitembelea. SEKRETARI: Mume wangu hatuendi Serena MUME (anampigia Mpango): dah! mpenzi, huyu mke wangu haendi tena. Shit! So hadi next time plz Mpango wa kando a.k.a teacher (anampigia mwanafunzi): Darasa kama kawaida sorry for the earlier message. MWANAFUNZI: darling tution inaendelea kumbe, so nakuja wiki ijayo!! BOSS: Sekretari sorry jitayarishe ile safari ya Serena iko palepale……
Utajuaje kama unachoangalia ni filamu ya kibongo!!!!
Updated at: 2024-05-25 17:59:35 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Angalia hivi
-Mlinzi wa Getini lazima awe chizi -Mtu yupo kijijini, maisha magumu ana Wave kichwani. -Kama bosi atakuwa na kampuni basi ni lazima itakuwa ya Clearing and Forwading au ya uuzaji Magari. -Lazima waende Kununua nguo. -Jambazi lazima avae koti lefu jeusi na Miwani. -Mtu akichapwa kofi huangukia kwenye kochi ama kitandani. -Actress huwa hawapiki hata chai. -Kwa mdada akiishi maisha ya kitajiri lazima avae nguo inayoishia mapajani. -Actress even after 5 yeas utakuta staili ya nywele na rangi za kucha ni zile zile. -Anaweka Sumu alafu anaonja kama imekolea. -Movie zote wapenzi huitana Baby.. -Main actor wote ni wafanya biashara na lazima wataongelea mizigo kutoka bandarini. -Wakinywa Soda basi lazima wabakishe.