Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Kisa cha kusisimua: Funzo kwa mabinti

Featured Image

Kijana maskini na mwenye maisha duni alimpenda msichana mmoja
Baada ya kutumia muda mwingi kumfikiria msichana huyo,
Siku moja akaamua kumwita na kumwambia ukweli ya kwamba amempenda na angehitaji kumuoa.

Msichana kwa nyodo na jeuri akasema "sikiliza tena unisikilize kwa makini wewe maskini mshahara wako unaopokea kwa mwezi hautoshi hata kwa matumizi yangu ya siku moja sasa utawezaje kunitunza mm!

Kwaufupi mm sio levo zako hivyo basi sahau kabisa kuhusu kunipata mimi
Nenda katafute maskini mwenzio atakae endana na maisha yako,
Mwisho akamwangalia kwa dharau na kisha akaenda zake.

Kwanzia siku ile kijana hakubahatika tena kumuona msichana yule lkn kwakuwa alimpenda basi hakuweza kumsahau kirahisi rahisi siku zilienda na miezi ikasonga,
Miaka 10 baadae wawili hawa walikuja kukutana katika supermarket moja hivi mjini

Kijana alipomwona msichana alitabasamu lakin kabla hajasema chochote msichana kama kawaida yake kwa dharau akasema "we maskin upo! hivi na ww unaingiaga supermarket eh!

Akaongeza huku akisema walau sasahivi nakuona umependeza inaonekana boss wako kakuongeza mshahara
ila kwa kifupi naomba nikwambie sasahivi nimeshaolewa mume wangu anafanya kazi kwenye kampuni moja hivi ya mtu binafsi kampuni maarufu sana na mshahara wa mume wangu ni shilingi milioni moja na laki mbili kwa mwezi na malupulupu mengine kibao,
Unafikiri ww na umaskini wako kuna siku utakuja kufikia kiwango cha mshahara anachopokea mume wangu!

Macho ya kijana yalitokwa na machozi kwa kuona msichana hajabadilika na anaendelea kuwa na maneno ya kejeri na dharau.

Mara hii mume wa yule dada akaingia ktk supermarket
Ile kumuona yule kijana mume akasema "ooh! Kiongozi upo hapa! Leo imekuwa bahati umekutana na mke wangu!" Kisha akamgeukia mke wake na kusema "mke wangu huyu ndo boss wangu

Na unajua nn mke wangu usishangae kumuona boss wangu anakuja kununua vitu mwenyewe hapa supermarket ukweli ni kwamba boss wangu hana mke, anasema alisha wahi kumpenda msichana mmoja lakini hakufanikiwa kumpata na amekuwa na ndoto ya kuja kukutana tena na msichana huyo ndio maana mpaka sasa bado hajaoa.

Akaendelea kusema hebu fikiria ni bahati kiasi gani alikuwa nayo msichana huyo kama angekubali kuolewa na boss wangu leo hii siangekuwa
maisha!

Muda wote msichana alikuwa kimya hajui hata ajibu nn kwa dharau alizomuonyesha kijana tangu mwanzo.


UJUMBE WANGU
Kwenye maisha mambo huweza kubadilika kama vile upepo unavoweza kubadili mwelekeo kulingana na masaa Hivyo basi usimdharau na kumbeza mtu yeyote kwa sababu ya hali aliyonayo,
Maana kila mtu anafungu lake alilopangiwa na Mungu,

Lakini pia kumbuka hakuna ajuaye kesho
Wakati mwingine mtu unayemdharau leo ndiye huyohuyo ambaye kesho utasimulia mafanikio yake.

Kwako unayesoma ujumbe huu nakuombea Mungu akakufungulie milango ya baraka na kuyapa thamani maisha yako ili pale ulipozomewa ukashangiliwe na wale wote waliokudharau punde wakapate kukupigia magoti kwa uweza wa Mungu.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Director J (User) on May 15, 2025

Good story πŸ’ͺ

Related Posts

Jinsi ya Kuimarisha mawasiliano ya kimapenzi na mpenzi wako

Jinsi ya Kuimarisha mawasiliano ya kimapenzi na mpenzi wako

Kuimarisha mawasiliano ya kimapenzi na mpenzi wako ni muhimu kwa kuendeleza uhusiano wenye afya na k... Read More
Ushawishi wa Vyombo vya Habari katika Maoni yetu ya Kufanya Mapenzi: Kuchambua na Kuelimisha

Ushawishi wa Vyombo vya Habari katika Maoni yetu ya Kufanya Mapenzi: Kuchambua na Kuelimisha

Ushawishi wa vyombo vya habari katika maoni yetu ya kufanya mapenzi ni suala ambalo limekuwa liki... Read More

Jinsi ya Kudumisha Afya ya Akili katika Familia: Kuwa na Nafasi ya Msaada na Uelewa

Jinsi ya Kudumisha Afya ya Akili katika Familia: Kuwa na Nafasi ya Msaada na Uelewa

Karibu kwenye makala hii ambayo inakupa vidokezo juu ya jinsi ya kudumisha afya ya akili katika f... Read More

Jinsi ya Kujenga Mazingira ya Ushirikiano na Kuelimisha na mke wako

Jinsi ya Kujenga Mazingira ya Ushirikiano na Kuelimisha na mke wako

Kujenga mazingira ya ushirikiano na kuelimisha na mke wako ni muhimu sana kwa kukuza uhusiano wenu n... Read More
Jinsi ya Kukuza Heshima na Uaminifu katika Mahusiano ya Familia

Jinsi ya Kukuza Heshima na Uaminifu katika Mahusiano ya Familia

Mahusiano ya familia ni muhimu sana kwani ndiyo yanayotufanya tuwe na furaha na amani katika mais... Read More

Kukuza Mshikamano na Umoja katika Mahusiano ya Kifamilia

Kukuza Mshikamano na Umoja katika Mahusiano ya Kifamilia

Mahusiano ya kifamilia ni muhimu sana katika maisha yetu ya kila siku. Ni muhimu sana kukuza mshi... Read More

Njia za Kuimarisha Ushirikiano wa Kijamii na Kuweka Mipango ya Shughuli za Familia

Njia za Kuimarisha Ushirikiano wa Kijamii na Kuweka Mipango ya Shughuli za Familia

Katika jamii, ushirikiano wa kijamii ni muhimu sana katika kuwezesha maendeleo na ustawi wa wanaj... Read More

Kufanya Mapenzi Salama na Kuepuka Hatari za Afya: Miongozo na Mbinu

Kufanya Mapenzi Salama na Kuepuka Hatari za Afya: Miongozo na Mbinu

Habari! Karibu kwenye makala hii ambayo itakupa miongozo na mbinu za kufanya mapenzi salama na ku... Read More

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya burudani na michezo

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya burudani na michezo

Kuwasiliana na mpenzi wako ni muhimu sana ili kudumisha uhusiano wenye afya na furaha. Kuna mambo... Read More

Kujenga Ushirikiano wenye Kusudi na Kuunga Mkono Malengo ya Kila Mwanafamilia

Kujenga Ushirikiano wenye Kusudi na Kuunga Mkono Malengo ya Kila Mwanafamilia

Kujenga Ushirikiano wenye Kusudi na Kuunga Mkono Malengo ya Kila Mwanafamilia

  1. Ku... Read More

Jinsi ya Kuanzisha Mawasiliano ya Kwanza na Msichana

Jinsi ya Kuanzisha Mawasiliano ya Kwanza na Msichana

Leo, tutazungumzia jinsi ya kuanzisha mawasiliano ya kwanza na msichana. Ni muhimu sana kwa kila ... Read More

Njia za Kuwa na Mazungumzo ya Kujenga na Msichana

Njia za Kuwa na Mazungumzo ya Kujenga na Msichana

Njia za Kuwa na Mazungumzo ya Kujenga na Msichana

Mawasiliano ni muhimu katika kila uhusia... Read More