Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Kisa cha kusisimua cha kijana na mke wake na mama yake

Featured Image

Kuna kijana mmoja daktari alikwenda kuposa. Binti aliyemposa akamuwekea masharti mazito. Akamwambia chagua mawili imma kunioa mimi au kukaa na mama yako, kwa sababu ukinioa mimi sitokubali mama yako aje hata harusini kwangu! Yule kijana aliemewa. Hakujua la kufanya. Mke anamtaka, lakini mama yake pia anampenda.


Hivyo aliamua kuomba ushauri kwa mwalimu wake wa chuo kikuu. Alimwambia: moyo wangu unampenda mno binti niliyekwenda kumposa, lakini pia siwezi kuishi mbali na mama yangu. Nifanye nini?


Yule mwalimu mwenye hekima ambaye alikuwa anajua tabu alizopitia mama wa kijana yule, alimjibu kwa kumwambia: Kabla ya kukueleza uchague yupi kati ya wawili hao, rudi nyumbani, na leo usifanye chochote, ila kuikosha mikono ya mama yako. Yule kijana alifanya kama alivyotakiwa na mwalimu wake. Alipofika nyumbani aliomba idhini kwa mama yake amruhusu kuikosha mikono yake, na yule mama alimkubalia bila ya ajizi yoyote.



Yule kijana alipoanza kuikosha mikono ya mama yake na kuona jinsi ilivyogugutaa kwa kazi za sulubu, alilia sana. Muda wote huu alikuwa hajawahi kuangalia viganja vya mama yake. *Je, na wewe umewahi kukaa na kuangalia viganja vya mama au baba yako kuona tabu walizopitia kukulea?* Kumbe baba wa yule kijana alifariki dunia yeye akiwa bado mdogo, yule mama aliamua kusamehe kila kitu kwa ajili ya mustakbali wa mwanawe. Alijitolea kufanya kazi za sulubu. Alikubali kuwa mtumishi wa ndani, kukosha nguo, kupiga deki na kila kazi ambayo alihisi ingelimletea chumo la halali bila ya kujali ugumu wa jkazu hiyo.



Juhudi zake zilizaa matunda na kufanikiwa kumlea na kumsomesha mwanawe hadi chuo kikuu na sasa ni daktari ambaye ana mustakbali mzuri. Baada ya yule kijana kukumbuka yote hayo, alifanya haraka kumpigia simu mwalimu wake huku macho yakiendelea kububujikwa na machozi akimwambia, siwezi kusubiri hadi kesho. Jibu nimeshalipata. Siwezi kumtupa mama yangu kwa ajili ya mtu asiyejua thamani ya mama. Ahsante sana kwa kunionesha njia sahihi! Kamwe siwezi kumuuza mama yangu kwa ajili ya leo yangu wakati yeye ameuza maisha yake yote kwa ajili ya mustakbali wangu.
NANI KAMA MAMA?!? Maa! Tabasamu lako ni ufunguo wangu wa ofanisi.
Kama umeipenda.


Share kwa wengine ili nao wazinduke.






Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE




[products columns="2" ids="30827"]


AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya Kuunga Mkono Kazi na Mafanikio ya Mke wako

Jinsi ya Kuunga Mkono Kazi na Mafanikio ya Mke wako

Kuunga mkono kazi na mafanikio ya mke wako ni muhimu sana katika kujenga uhusiano imara na kuimarish... Read More
Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya burudani na michezo

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya burudani na michezo

Kuwasiliana na mpenzi wako ni muhimu sana ili kudumisha uhusiano wenye afya na furaha. Kuna mambo... Read More

Njia za Kujenga Heshima na Usawa katika Kufanya Mapenzi: Kupigania Mahusiano ya Kijinsia yenye Afya

Njia za Kujenga Heshima na Usawa katika Kufanya Mapenzi: Kupigania Mahusiano ya Kijinsia yenye Afya

Mapenzi ni sehemu muhimu sana ya maisha yetu, lakini wakati mwingine yanaweza kuwa magumu kuyashu... Read More

Jinsi ya Kuunda Mazingira ya Kuwasaidia Watoto Kufanikiwa Shuleni na Maisha

Jinsi ya Kuunda Mazingira ya Kuwasaidia Watoto Kufanikiwa Shuleni na Maisha

Karibu kwenye makala hii ambayo itakupa mwongozo wa jinsi ya kuunda mazingira ya kuwasaidia watot... Read More

Kukabiliana na Mazoea ya Kukosa Heshima katika Familia: Kuweka Mipaka na Kuheshimiana

Kukabiliana na Mazoea ya Kukosa Heshima katika Familia: Kuweka Mipaka na Kuheshimiana

Kukabiliana na Mazoea ya Kukosa Heshima katika Familia: Kuweka Mipaka na Kuheshimiana

Kati... Read More

Kukabiliana na Mazoea ya Kukosa Heshima katika Mahusiano: Kuweka Mipaka na Kuheshimiana

Kukabiliana na Mazoea ya Kukosa Heshima katika Mahusiano: Kuweka Mipaka na Kuheshimiana

Habari za leo wapenzi wa Kiswahili! Leo tutajadili kuhusu kukabiliana na mazoea ya kukosa heshima... Read More

Jinsi Mwanamme Unavyoweza kubobea katika Mapenzi na Mahusiano

Jinsi Mwanamme Unavyoweza kubobea katika Mapenzi na Mahusiano

Read More
Jinsi Kuaminiana na Kuwa Wazi katika Mahusiano yako na mke wako

Jinsi Kuaminiana na Kuwa Wazi katika Mahusiano yako na mke wako

Kuaminiana na kuwa wazi ni msingi muhimu wa mahusiano imara na yenye furaha na mke wako. Hapa kuna n... Read More
Jinsi ya Kuwa na Mazungumzo ya Afya na Watoto kuhusu Mahusiano na Mapenzi

Jinsi ya Kuwa na Mazungumzo ya Afya na Watoto kuhusu Mahusiano na Mapenzi

Ulizia mtu yeyote anapenda kuzungumza na mtoto wake kuhusu mahusiano na mapenzi, na utapata majib... Read More

Je, watu wanapendelea ngono/kufanya mapenzi ya kawaida au ngono/kufanya mapenzi ya kufanya mazoezi ya kimwili?

Je, watu wanapendelea ngono/kufanya mapenzi ya kawaida au ngono/kufanya mapenzi ya kufanya mazoezi ya kimwili?

Habari rafiki! Karibu katika makala hii ambayo itakupa mwanga kuhusu kile watu wanapendelea kati ... Read More

Jinsi ya Kujenga Uaminifu katika Familia: Kuheshimu na Kutimiza Ahadi

Jinsi ya Kujenga Uaminifu katika Familia: Kuheshimu na Kutimiza Ahadi

Leo, tutajadili jinsi ya kujenga uaminifu katika familia kwa njia ya kuheshimu na kutimiza ahadi.... Read More

Je, kuna umuhimu wa kujadili matakwa ya kujamiiana na ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Je, kuna umuhimu wa kujadili matakwa ya kujamiiana na ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Habari wapendwa wasomaji, leo tutaangazia swali muhimu sana ambalo wapenzi wengi hujiuliza. Je, k... Read More