Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Kisa cha kusisimua cha kijana na mke wake na mama yake

Featured Image

Kuna kijana mmoja daktari alikwenda kuposa. Binti aliyemposa akamuwekea masharti mazito. Akamwambia chagua mawili imma kunioa mimi au kukaa na mama yako, kwa sababu ukinioa mimi sitokubali mama yako aje hata harusini kwangu! Yule kijana aliemewa. Hakujua la kufanya. Mke anamtaka, lakini mama yake pia anampenda.


Hivyo aliamua kuomba ushauri kwa mwalimu wake wa chuo kikuu. Alimwambia: moyo wangu unampenda mno binti niliyekwenda kumposa, lakini pia siwezi kuishi mbali na mama yangu. Nifanye nini?


Yule mwalimu mwenye hekima ambaye alikuwa anajua tabu alizopitia mama wa kijana yule, alimjibu kwa kumwambia: Kabla ya kukueleza uchague yupi kati ya wawili hao, rudi nyumbani, na leo usifanye chochote, ila kuikosha mikono ya mama yako. Yule kijana alifanya kama alivyotakiwa na mwalimu wake. Alipofika nyumbani aliomba idhini kwa mama yake amruhusu kuikosha mikono yake, na yule mama alimkubalia bila ya ajizi yoyote.



Yule kijana alipoanza kuikosha mikono ya mama yake na kuona jinsi ilivyogugutaa kwa kazi za sulubu, alilia sana. Muda wote huu alikuwa hajawahi kuangalia viganja vya mama yake. *Je, na wewe umewahi kukaa na kuangalia viganja vya mama au baba yako kuona tabu walizopitia kukulea?* Kumbe baba wa yule kijana alifariki dunia yeye akiwa bado mdogo, yule mama aliamua kusamehe kila kitu kwa ajili ya mustakbali wa mwanawe. Alijitolea kufanya kazi za sulubu. Alikubali kuwa mtumishi wa ndani, kukosha nguo, kupiga deki na kila kazi ambayo alihisi ingelimletea chumo la halali bila ya kujali ugumu wa jkazu hiyo.



Juhudi zake zilizaa matunda na kufanikiwa kumlea na kumsomesha mwanawe hadi chuo kikuu na sasa ni daktari ambaye ana mustakbali mzuri. Baada ya yule kijana kukumbuka yote hayo, alifanya haraka kumpigia simu mwalimu wake huku macho yakiendelea kububujikwa na machozi akimwambia, siwezi kusubiri hadi kesho. Jibu nimeshalipata. Siwezi kumtupa mama yangu kwa ajili ya mtu asiyejua thamani ya mama. Ahsante sana kwa kunionesha njia sahihi! Kamwe siwezi kumuuza mama yangu kwa ajili ya leo yangu wakati yeye ameuza maisha yake yote kwa ajili ya mustakbali wangu.
NANI KAMA MAMA?!? Maa! Tabasamu lako ni ufunguo wangu wa ofanisi.
Kama umeipenda.


Share kwa wengine ili nao wazinduke.






Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE




[products columns="2" ids="30827"]


AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Njia za Kuwa na Uhusiano Wenye Furaha na Msichana

Njia za Kuwa na Uhusiano Wenye Furaha na Msichana

Leo, tutajadili njia za kuunda uhusiano mzuri na wa furaha na msichana. Kuwa na uhusiano mzuri na... Read More

Kupanua Wigo wa Uzoefu wa Kufanya Mapenzi: Kujaribu Mazoea Mapya na Nafasi

Kupanua Wigo wa Uzoefu wa Kufanya Mapenzi: Kujaribu Mazoea Mapya na Nafasi

Leo hii, tunataka kuzungumzia kuhusu kupanua wigo wa uzoefu wa kufanya mapenzi. Kwa wengi wetu, t... Read More

Je, kuna umuhimu kuweka mazingira ya kimapenzi kabla ya kufanya ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu kuweka mazingira ya kimapenzi kabla ya kufanya ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu wa kuweka mazingira ya kimapenzi kabla ya kufanya ngono au kufanya mapenzi? Ndio... Read More

Jinsi ya kuwasiliana kwa ufanisi na mpenzi wako

Jinsi ya kuwasiliana kwa ufanisi na mpenzi wako

Kuwasiliana kwa ufanisi na mpenzi wako ni muhimu sana kwa uhusiano wa kudumu na wenye furaha. Hapa k... Read More
Kufikia Kilele: Umuhimu wa Ushirikiano wa Kufikia Kilele katika Kufanya Mapenzi

Kufikia Kilele: Umuhimu wa Ushirikiano wa Kufikia Kilele katika Kufanya Mapenzi

Mapenzi ni hisia za moyoni ambazo zinaweza kumfanya mtu kufikia kilele cha furaha na utimilifu wa... Read More

Jinsi ya Kusimamia tofauti za maoni na migogoro katika uhusiano wa mapenzi

Jinsi ya Kusimamia tofauti za maoni na migogoro katika uhusiano wa mapenzi

Kusimamia tofauti za maoni na migogoro ni sehemu muhimu ya kujenga uhusiano wa mapenzi wenye afya. H... Read More
Njia za Kuimarisha Ushirikiano wa Kijamii na Jamaa katika Familia Yako

Njia za Kuimarisha Ushirikiano wa Kijamii na Jamaa katika Familia Yako

Kuimarisha ushirikiano wa kijamii na jamaa katika familia yako ni muhimu sana kwa afya na ustawi ... Read More

Majukumu ya mke katika ndoa

Majukumu ya mke katika ndoa

Katika ndoa, jukumu la mke ni jukumu muhimu na linajumuisha majukumu mengi. Hapa kuna baadhi ya maju... Read More
Dalili za mahusiano feki, mahusiano ya kichina

Dalili za mahusiano feki, mahusiano ya kichina

Ukitaka kujua Simu ya Kichina utajua tu jinsi ilivyo na makelele mengiiiii sana wakati wa kuitaβ€... Read More

Kukabiliana na Mazoea ya Kutowasiliana katika Mahusiano: Kujenga Mawasiliano ya Kina

Kukabiliana na Mazoea ya Kutowasiliana katika Mahusiano: Kujenga Mawasiliano ya Kina

Mahusiano ni kitu muhimu sana katika maisha yetu. Kupitia mahusiano tunapata faraja, upendo, na m... Read More

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kukuza na kudumisha stadi za mawasiliano

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kukuza na kudumisha stadi za mawasiliano

Kama wapenzi, tunahitaji kuwa na uhusiano mzuri na kudumisha stadi za mawasiliano ili kuboresha u... Read More

Mambo 10 ambayo wanawake wamewazidi wanaume

Mambo 10 ambayo wanawake wamewazidi wanaume

1. Wana Nguo Nyingi KulikoWanaume.
2. Wanafahamu Nani Ni Baba HalisiWa Watoto Wao.

3. N... Read More