Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Jinsi ya kumshawishi mwanamke kufanya mapenzi

Featured Image

Zifuatazo ni njia za kuamsha hamu ya kufanya mpenzi ya mwanamke. Njia hizi zimegawanyika katika hatua mbili kuu, kwanza ni kumfanya akukubali na kisha kuamsha hisia zake.


 

Mfanye akukubali


Njia za kumfanya akukubali ni kama ifuatavyo


Uwe na muonekano mzuri


Wanawake wanapenda wanaume wasafi na watanashati kwa hiyo ukiwa msafi na mtanashati utakua na mvuto kwake. Hivyo utakapoamua kumshawishi kufanya mapenzi itakua rahisi yeye kuwa rahisi kukubali.


Mfanye ajisikie huru


Ni rahisi mwanamke kufanya mapenzi na mtu anayejisikia huru mbaele zake na ambaye yupo huru kuongea na kufanya nae mambo mengine ya kawaida katika maisha. Kwa hiyo ili uweze kumshawishi mwanamke kufanya mapenzi na wewe njia nzuri ni kumfanya ajisikie yupo huru mbele yako na kasha atakua huru kufanya mapenzi na wewe.


 

Mfurahishe


Mfanye ajisikie mwenye furaha kila anapokuwa na wewe na atamani kuwa na wewe. Akishajiskia mwenye furaha kila anapokuwa na wewe ni rahisi kushawishika kuwa na wewe kimapenzi.


Mfanye ajione kuwa yeye ni mzuri


Mwanamke anapenda sana na anavutiwa na mwanamme anayeona ubora wake au anayemsifia kuwa ni mzuri.


Mfanye akuamini


Mfanye aamini kwamba hata baada ya kufanya mapenzi bado mtakua pamoja na sio mwisho wa mahusiano yenu au urafiki wenu.


 

Usiwe na haraka, Mpe muda


Usiwe na haraka ya kumwambia kuwa unataka kufanya mapenzi na yeye bali subiri mpaka utakapoona yupo tayari au anaelekea kukuhitaji.


Mfanye akuone mwaminifu


Mfanye akuone mwaminifu kwa kutomchanganya na wanawake wengine. Usimuonyeshe kuwa una mahusiano na wanawake wengine. Mfanye aamini kuwa unamuhitaji yeye tuu.


 

Mjali kama mwanamke


Mfanye ajiskie kuwa mwanamke. Jaribu kuonyesha kuwa mwelewa, onyesha kuwa unajali, mkarimu na muonyeshe kuwa wewe ni msaada kwake. Mfungulie mlango, mbebee begi au pochi yake n.k.


Onyesha kuwa unapenda kila kitu kutoka kwake


Muonyeshe kuwa unampenda yeye na vyote vyake. Onyesha kuwa umevutiwa na yeye na mambo yake yote na sio mwili wake tuu.


 

Amsha Hisia zake


Baada ya kumvutia, sasa amsha hisia zake. Njia za kuamsha hamu ya kufanya mpenzi ya mwanamke au Hatua za kufuata kuamsha hisia za mwanamke ni kama ifuatavyo


Andaa mazingira


Andaa mazingira ya kuamsha hisia zake, fanya kitu kitakachowasogeza karibu na kuamsha hisia zake Kwenye akili yake kabla ya kugusa mwili. Mfano, weka mziki au muvi nzuri n.k. Kisha tengeneza mazingira ya kuwa karibu kimwili na kugusana.


 

Kaa kwa kubanana naye


Unapokuwa na mwanamke ambaye umemzimia, tafuta kisababu cha kukaa na yeye karibu. Toa simu muangalie pamoja videos kama vile za kuchekesha, ama unaweza kuchukua kitabu/gazeti umuonyeshe habari ambazo anapenda ilimradi tuu muwe karibu.


Usimwonyeshe/usiongee wazi kile unachotaka


Usijaribu kutumia lugha ya kutongoza ama utamfanya aanze kukushuku. Tayari anajua kuwa miguso ya mikono yako ya mara kwa mara inaashiria kitu fulani. Kile unachotakiwa kufanya ni kuivuruga akili yake kwa kuleta mada ambayo itamvutia huku ukiendelea gusa mwili wake


 

Anza kutumia lugha ya kumsuka


Wakati mtakuwa mnaendelea unaweza kutumia maneno ya kumsuka lakini yawe ya kichini chini. Mfano unaweza kumwambia "Unanukia utamu", "nimependa kitambaa cha nguo yako","nishawahi kukuambia kuwa macho yako yanapendeza? Nimependa vile yanang'aa nikiwa karibu yako." Maneno kama haya unaweza kumrushia mwanamke huyu bila hata yeye kusongea mbali na wewe. Mwanzo atakuwa anapenda kuyaskia.


Isome miondoko yake


Ukianza kumuona anazungumza polepole na kukusongelea karibu yako, ishara kuu ni kuwa yupo tayari. Kwa hiyo kufikia hapa unaweza kurudia hatua za kumsuka, kumgusa na kujaribu kufikia viungo vyake vingine vya mwili ilimradi nyote wawili mnafurahia.


 

Mbusu


Baada ya kuandaa mudi au mazingira na kuamsha hisia zake sasa tafuta namna ya kumbusu. Mbusu taratibu kwa namna ambayo haitamshtua na kumfanya aogope au akatae.


Mhikeshike


Wakati wa kumbusu mshike mwili wake ili kuamsha hisia zake. Anza na mikono kasha rudi kichwani Kwenye nywele zake na kisha maliza sehemu nyingine za kuamsha hisia zake


Usimlazimishe bali mbembeleze


Kama hataki usimlazimishe bali mbembeleze au muache mpaka wakati mwingine atakapokuwa tayari.


 

NB: Ni makosa makubwa na ni dhambi kufanya mapenzi kabla ya ndoa. Mbinu hizi zitumie kwa mwenzi wako wa ndoa






Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE




Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke





Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.





[products columns="2" ids="30827"]


AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu mipango ya likizo na safari za pamoja

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu mipango ya likizo na safari za pamoja

Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu mipango ya likizo na safari za pamoja ni muhimu sana katika mah... Read More

Kuhamasisha Ushirikiano wa Kiroho katika Mahusiano: Kuungana kwa Kiimani

Kuhamasisha Ushirikiano wa Kiroho katika Mahusiano: Kuungana kwa Kiimani

  1. Kutafuta jambo la pamoja: Uhusiano wa kiroho unahitaji kuwa na jambo la pamoja ambalo linaw... Read More
Jinsi ya Kufanya Familia kuwa Kitovu cha Huduma na Kujitolea: Kuleta Mabadiliko Chanya

Jinsi ya Kufanya Familia kuwa Kitovu cha Huduma na Kujitolea: Kuleta Mabadiliko Chanya

  1. Kuanzisha mazungumzo ya familia: Familia inapaswa kuwa kitovu cha huduma na kujitolea. ... Read More

Je, nini imani ya watu katika kuzungumza waziwazi juu ya ngono/kufanya mapenzi na kutokuwa na aibu?

Je, nini imani ya watu katika kuzungumza waziwazi juu ya ngono/kufanya mapenzi na kutokuwa na aibu?

Habari rafiki yangu! Leo tutaongea kuhusu umuhimu wa kuzungumza waziwazi juu ya ngono na kufanya ... Read More

Jinsi ya Kuonyesha upendo na heshima kwa mpenzi wako

Jinsi ya Kuonyesha upendo na heshima kwa mpenzi wako

Kuonyesha upendo na heshima kwa mpenzi wako ni muhimu katika kudumisha uhusiano mzuri na wa afya. Ha... Read More
Kujenga Ushirikiano wenye Uaminifu na Kujenga Imani katika Familia

Kujenga Ushirikiano wenye Uaminifu na Kujenga Imani katika Familia

Katika familia, ushirikiano wenye uaminifu na imani ni muhimu sana kwa ustawi wa kila mmoja. Ni m... Read More

Kujenga Mazingira ya Upendo na Ukarimu katika Familia ili Kuwa na Amani na Furaha

Kujenga Mazingira ya Upendo na Ukarimu katika Familia ili Kuwa na Amani na Furaha

Karibu kwenye makala hii inayojadili jinsi ya kujenga mazingira ya upendo na ukarimu katika famil... Read More

Kukabiliana na Mazoea ya Kutowasiliana katika Mahusiano: Kujenga Mawasiliano ya Kina

Kukabiliana na Mazoea ya Kutowasiliana katika Mahusiano: Kujenga Mawasiliano ya Kina

Mahusiano ni kitu muhimu sana katika maisha yetu. Kupitia mahusiano tunapata faraja, upendo, na m... Read More

Jinsi ya Kudumisha Afya ya Akili katika Familia: Kuwa na Nafasi ya Msaada na Uelewa

Jinsi ya Kudumisha Afya ya Akili katika Familia: Kuwa na Nafasi ya Msaada na Uelewa

Karibu kwenye makala hii ambayo inakupa vidokezo juu ya jinsi ya kudumisha afya ya akili katika f... Read More

Njia za Kujenga Tabia ya Kushukuru na Kuwa na Amani na Furaha katika Familia

Njia za Kujenga Tabia ya Kushukuru na Kuwa na Amani na Furaha katika Familia

Familia ni muhimu sana katika maisha yetu. Ili kufurahia maisha na kuishi kwa amani, tabia ya kus... Read More

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kujenga na kudumisha mahusiano ya kifamilia

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kujenga na kudumisha mahusiano ya kifamilia

Kujenga na kudumisha mahusiano ya kifamilia ni muhimu sana. Familia inategemea upendo, maelewano,... Read More

Njia za Kuunda Utamaduni wa Ushirikiano na Heshima katika Familia

Njia za Kuunda Utamaduni wa Ushirikiano na Heshima katika Familia

Njia za Kuunda Utamaduni wa Ushirikiano na Heshima katika Familia

Familia ni kitovu cha ma... Read More