Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Ishara 10 za mwanamke aliyekuzimia na anayekupanda

Featured Image

Ishara hizi zinaweza zikakusaidia kumgundua msichana anayekupenda, wasichana wanatofautiana ila wengi wao wana-share ishara tofauti. Mwanamke anayekupenda hatakosa kati ya hizi


 

Siyo kwamba ishara hizi zote anaweza kuwanazo msichana mmoja, ila kila mmoja kwa ishara zake.


Ishara hizo ni kama ifuatavyo


1. Mnapokutana na kuongea


Msichana anayekupenda anakuwa na tabasamu unapoongea naye kama amekuzoea, ila kama hajakuzoea anapokuona gafla tabasamu hutoweka maana anakuwa na aibu. Hawezi akakuangalia machoni atakuwa anakuangalia kwa kuibia. Sikiliza sauti yake, kama anaona aibu sauti yake itakuwa ya upole/laini anaweza akaanza kushika shika nywele zake au kuweka sawa mavazi yake.


 

2. Ajali za kijitakia


Anaweza akatafuta sababu yoyote ilimradi tu akushike. Anaweza akaona kitu kidogo tu au mdudu halafu anakurukia, au anakukumbatia.


3. Anaibia kukuchunguza


Unapokuwa umetulia zako unakuta anakuangalia kwa kuibia, ukigeuka anajifanya yuko bize na mambo yake kumbe anakuchunguza taratibu.


4. Anapenda mgusane


Mwanamke anayevutiwa na wewe mnapotembea naye mahali anapenda kushika mkono wako, au unapokutana naye anaweza kukukumbatia.


 

5. Anatafuta ukaribu


Mwanamke aliyevutiwa na wewe anapenda kuwa karibu na wewe muda wote. Mfano akiwa na marafiki zake halafu mkakutana gafla atakufuata halafu waangalie marafiki zake utakuta kama wanateta, ukiona hali hiyo kuna siri yao yeye na marafiki zake kuhusu wewe. Anapokuwa na marafiki zake akikuona anaweza akajitenga, hata kama mmeenda out pamoja na marafiki
zake utakuta yupo karibu na wewe.


6. Anapenda umjali


Anapokuwa na tatizo au anajisikia vibaya lazima akuambie, mfano mmeenda mahali kukawa na baridi hata kama si baridi sana atasema anahisi baridi ili mradi umsaidie koti lako, hata kama kuna watu hawezi kuona aibu kuvaa badala yake atajisikia vizuri anapovaa koti lako.


7. Hawezi kuzuia tabasamu


Unapomwonyeshea tabasamu lazima na yeye akuonyeshee, hata kama kuna kitu kimemwudhi atakuonyeshea tabasamu ili mradi aonyeshe umemkuta katika hali ya furaha.


 

8. Ishara za mwili


Anapopita mbele yako anaweza akafanya madoido mengi ambayo yatakuvutia ila kama anajiamini. Kama hajiamini anapokuona gafla anakosa amani, utamwona anashtuka gafla.


9. Anafurahishwa na vituko vyako


Mwanamke anayekupenda daima ni mwenye furaha mkiwa pamoja. Huwezi ukamboa, hata kama ukifanya kituko ambayo haichekeshi utakuta anafurahia.


10. Anakujali


Anakuwa anakujali, mfano akiona umeumia labda umejigonga, yupo radhi akuhudumie. unapokuwa naye anaweza kuuliza "unahitaji chochote? unaweza ukasema "nina kiu ngoja ninunue maji" utamsikia "nina maji, kunywa haya yangu kwanza".basi ujue kwamba anakujali.






Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE




Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke





Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.





[products columns="2" ids="30827"]


AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Je, kuna umuhimu wa kujifunza kuhusu anatomi ya mwili wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu wa kujifunza kuhusu anatomi ya mwili wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu wa kujifunza kuhusu anatomi ya mwili wakati wa ngono/kufanya mapenzi? Ndiyo! Kwa... Read More

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kuishi na kukabiliana na msongo wa mawazo

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kuishi na kukabiliana na msongo wa mawazo

Kuishi na kukabiliana na msongo wa mawazo ni changamoto inayoweza kuathiri uhusiano na ustawi wa mpe... Read More
Jinsi ya Kupanga Tarehe ya Kipekee na Msichana Wako

Jinsi ya Kupanga Tarehe ya Kipekee na Msichana Wako

Jinsi ya Kupanga Tarehe ya Kipekee na Msichana Wako

Kupanga tarehe ya kipekee na msichana ... Read More

Kujenga Ushirikiano wenye Uwiano na Kuhamasisha Uadilifu katika Familia

Kujenga Ushirikiano wenye Uwiano na Kuhamasisha Uadilifu katika Familia

Kujenga Ushirikiano Wenye Uwiano na Kuhamasisha Uadilifu katika Familia

Familia ni moja ya... Read More

Jinsi ya Kuzungumza na mpenzi wako kuhusu mafanikio na changamoto za kazi

Jinsi ya Kuzungumza na mpenzi wako kuhusu mafanikio na changamoto za kazi

Kuzungumza na mpenzi wako kuhusu mafanikio na changamoto za kazi ni muhimu katika kujenga uelewa na ... Read More
Jinsi ya Kusaidia Watoto kukabiliana na Mafadhaiko na Shinikizo katika Maisha ya Familia

Jinsi ya Kusaidia Watoto kukabiliana na Mafadhaiko na Shinikizo katika Maisha ya Familia

Karibu kwenye makala hii ambapo tutajadili jinsi ya kusaidia watoto kukabiliana na mafadhaiko na ... Read More

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kujenga na kudumisha mipango ya muda mrefu

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kujenga na kudumisha mipango ya muda mrefu

Kusaidiana na mpenzi wako katika kujenga na kudumisha mipango ya muda mrefu ni muhimu katika kuweka ... Read More
Kuunda Uhusiano wenye Furaha na Chanya na Marafiki wa Mwenzi wako

Kuunda Uhusiano wenye Furaha na Chanya na Marafiki wa Mwenzi wako

Kuunda uhusiano wenye furaha na chanya na marafiki wa mwenzi wako ni muhimu sana katika kudumisha... Read More

Jinsi ya Kuelewa na kushughulikia tofauti za kiimani na mafundisho ya kidini na mpenzi wako

Jinsi ya Kuelewa na kushughulikia tofauti za kiimani na mafundisho ya kidini na mpenzi wako

Kama unapenda mtu wa imani tofauti na wewe, hapa kuna maoni kadhaa ambayo yanaweza kukusaidia kue... Read More

Jinsi ya Kupambana na Mawazo na Hisia Hasi za mke wako

Jinsi ya Kupambana na Mawazo na Hisia Hasi za mke wako

Kupambana na mawazo na hisia hasi za mke wako ni muhimu katika kujenga na kuimarisha uhusiano wenye ... Read More
Je, ni muhimu kuwa na usawa wa ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Je, ni muhimu kuwa na usawa wa ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Habari za leo wapenzi! Sijui kama umewahi kujiuliza kuhusu umuhimu wa usawa wa ngono/kufanya mape... Read More

Kujenga Uhusiano wa Kudumu: Je, Kufanya Mapenzi ya Mara Moja Inafaa?

Kujenga Uhusiano wa Kudumu: Je, Kufanya Mapenzi ya Mara Moja Inafaa?

Kujenga uhusiano wa kudumu ni jambo muhimu sana katika maisha ya kimapenzi. Kuna mambo mengi amba... Read More