Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMS💌💕
AckyShine

Ushauri kwa vijana wenye miaka 22 nakuendelea

Featured Image

Ikiwa wewe ni kijana na Una umri wa kuanzia miaka 22 na Kuendelea
Soma hapa ujifunze maisha ya hekima na namna bora ya kuishi na kufanikiwa ungali kijana

1. Kama uko shule au chuo soma na usicheze ukifeli unajipotezea muda. Soma sana utafanikiwa…

2. Jifunze kuweka akiba ya pesa. Pia jifunze kuwa na matumizi mazuri ya pesa,bajeti vizuri na jiwekee akiba bank au popte unapoona panafaa.

3. Jitengenezee good character yaani tabia yako njema ili uwe tofauti na wengine.. Jitofautishe na wengine, uwe mfano bora

4. Jifunze kufanya kazi tofauti tofauti. Fanya hiki ama kile ili angalau uweze kuishi popote kwani dunia inabadilikaa na huwezi jua kesho yako

5. Anza kununua na kumiliki vitu kama kitanda godoro vyombo na ardhi au kiwanja. Kumbuka msingi mzuri wa maisha ni fikra za ujana na kujiwekea mali

6. Kama utaweza kapange ujifunze maisha. Anza kujitegemea ili kujipa confidenece na maisha.

7. Weka falsafa yako katika maisha na uiishi. Falsafa ni dira ya kukuongoza. Mfano unataka kumiliki nini katika maisha? Unataka mke au mume wa aina gani? Aina gani ya maisha unaipenda? Hiyo ndiyo falsafa…

8. Tengeneza mahusiano yaliyotulia na weka malengo. (Kwa wale wa ndoa) Jichagulie kijana au binti aliyemzuri katika wengi, kijana au binti wa moyo wako, mpende… Kipindi hiki ni cha kuwa na mwenza aliyetulia kama unafikiri kuoa au kuolewa. Ukicheza ukafikisha 30 bila kuwa na mtu maaalumu basi utaoa au kuolewa bora mradi ila siyo na mtu wa ndoto yako..

9. Kuwa na marafiki imara, jichagulie katika wengi marafiki kadhaa waliotulia wenye nidhamu ya maisha na wanaopenda uende mbele. Kijana chunga marafiki ulionao wengi leo wanajuta kwaa urafiki m'baya uliowapoteza… a

10. Kumbuka ibada na kumshukuru Mungu. Kipindi hiki ni cha misukosuko na mihemko mingi. Usiache mafundisho ya imani yako, usimsahau Mungu. Mshukuru Mungu kwa uhai na kila jema au baya likupatalo.

11. Jitume katika kazi, watu waliofanikiwa wanajua thamani ya juhudi na kujituma. Usikate tamaa hata kama unapata kidogo. Fanya kazi kama vile kesho haipo. Matunda utayaona

12. Zingatia kujiweka safi. Kuwa msafi na mtanashati huanza na ubongo, muonekano wako ndivyo watu watakavyo kuchukulia. Jiweke safi na jitunze..

13. Kula kwa afya, wengi wanachukia miili yao. Wanauchukia aidha unene au wembamba, ila ukila kwa afya, ukafanya mazoezi unatengeneza afya bora ya sasa na baaadae..

14. Vaa kwa heshima, usivae kama mcheza disko au teja. Kumbuka thamani yako kwa Mungu. Kwanini uvae nguo za machukizo mbele yake! Kwanini ukubali kuwa wakala na kutumiwa na shetani kuwaaangamiza wengine kwa kuvaa ovyo? Vaa kwa heshima..

15. Pendelea kusafiri maeneo tofauti na ujifunze! Asafiriye hupata maarifa na hujifunza mengi. Penda kusafiri, tembelea maeneo tofauti utakuwa na mengi ya kujifunza.

16. Kumbuka kupumzisha mwili. Kuishi kwetu kupo katika chembe ya uhai iliyopo mwilini. Upe mwili na ubongo chakula chake cha kupumzika. Nenda maeneo yatakayofanya mwili na akili vipumzike angalau kila baada ya miezi kadhaa..

17. Jifunze kuamua mwenyewe. Usisubiri kila kitu kumshirikisha mtu ndio uamue. Jifunze kuwa mwamuzi wa mambo yako mwenyewe haijalishi kwa gharama ipi. Watu wawe washauri ila ubaki kuwa mwamuzi mwenyewe.

18. Kuwa mtu wa kutunza siri. Jitahidi kuwa na shingo nzito na akili yenye kuweka siri. Usiwe mtu wa kusema kila uonacho au uambiwacho.

19. Jfunze na zitawale hisia zako. Hisia ziwe za hasira, mapenzi au ugomovi zitawale na utaishi miaka mingi. Asiye tawala hisia zake hata awe mkubwa bado ni mdogo…

20. Jitolee kwaajili ya wengine, fundisha kemea saidia. Unaweza kufundisha kupitia facebook wasap nk. Kemea ukiona mtu anafanya kitu kibaya, saidia wenye shida wakumbuke wagonjwa yatima wazee na wenye mahitaji. Wewe ni yatima, mzee, au muhitaji wa kesho.. Weka akiba ya wema

21 Jenga mazingira ya kuishi na watu vizuri. Usijione mzuri au HB sana ukadharau wengine. Ishi na kila mtu kwa upendo hata kama wanakuchukia..

22. Tunza muda, muda ni mali huwezi kuurudisha, kuusimamisha au kuuzuia. Ukishapotea ndio basi tena. Tambua thamani ya muda na fanya vitu kwa wakati..

23. Pendelea kusoma hasa vitabu vya dini, kuhusu mali, elimu, mchumba, afya, maisha, uongozi, hekima, busara, utu, uchaji, utii, maarifa, utajiri, heshima, uvumilivu, matumaini, upendo, na kila kitu vimo katika Biblia na Qur'an ..soma uchote hekimaa…

24. Acha kujifunza matumizi ya pombe, sigara , dawa za kulevya. Kama unatumia jitahidi uache, kama unajifunza acha na kama kuna mtu anakushawishi kataa. Afya ni mali na mtaji usichoshe na kuumiza uhai wako kwa pombe sigara na madawa ya kulevya…

Inafaa ukishare kwa wengine wajifunze maarifa haya..
*Maisha ni maamuzi yako wewe*
Kuamua kufanikiwa au kushindwa,
kuamua utajiri au umasikini yote ni mipango na hutokana na fikra zako..

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Njia za Kupunguza Mazoea ya Kutothamini katika Familia: Kuweka Nafasi ya Kuonyesha Shukrani

Njia za Kupunguza Mazoea ya Kutothamini katika Familia: Kuweka Nafasi ya Kuonyesha Shukrani

Familia nyingi zinapitia changamoto ya kutothamini mazoea ya ndani ya familia. Hii inaweza kuathi... Read More

Jinsi ya Kusaidiana katika Mazoezi na Huduma ya Kimwili na mke wako

Jinsi ya Kusaidiana katika Mazoezi na Huduma ya Kimwili na mke wako

Kusaidiana katika mazoezi na huduma ya kimwili ni njia nzuri ya kujenga afya na ustawi pamoja na mke... Read More
Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya kiuchumi na kuwekeza

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya kiuchumi na kuwekeza

Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya kiuchumi na kuwekeza ni jambo muhimu katika uhusiano... Read More

Jinsi ya Kujenga Ushirikiano wenye Msingi imara katika Mahusiano yako

Jinsi ya Kujenga Ushirikiano wenye Msingi imara katika Mahusiano yako

Karibu kwenye makala hii ambayo itakupa mbinu mbalimbali kuhusu jinsi ya kujenga ushirikiano weny... Read More

Jinsi ya Kuwa na Muda Mzuri na Msichana Bila Kutumia Fedha Nyingi

Jinsi ya Kuwa na Muda Mzuri na Msichana Bila Kutumia Fedha Nyingi

Kutumia fedha nyingi kupata muda mzuri na msichana siyo lazima. Kuna njia nyingi za kuwa na muda ... Read More

Njia za Kujenga Hisia za Usalama katika Uhusiano wako na Msichana

Njia za Kujenga Hisia za Usalama katika Uhusiano wako na Msichana

Njia za Kujenga Hisia za Usalama katika Uhusiano wako na Msichana

Hakuna kitu kizuri kama ... Read More

Kuunda Muda na Nafasi ya Ubunifu katika Mahusiano yako

Kuunda Muda na Nafasi ya Ubunifu katika Mahusiano yako

Mahusiano ni muhimu sana katika maisha ya binadamu. Kuunda muda na nafasi ya ubunifu katika mahus... Read More

Jinsi ya Kuelewa na kushughulikia tofauti za kiutamaduni na maadili katika mahusiano na mpenzi wako

Jinsi ya Kuelewa na kushughulikia tofauti za kiutamaduni na maadili katika mahusiano na mpenzi wako

Mahusiano ni jambo la muhimu sana katika maisha yetu na wengi wetu tunataka kuwa na uhusiano mzur... Read More

Jinsi ya Kuweka Malengo ya Ndoa na mke wako

Jinsi ya Kuweka Malengo ya Ndoa na mke wako

Kuweka malengo ya ndoa na mke wako ni hatua muhimu katika kujenga msingi imara na kufikia furaha na ... Read More
Njia za Kuimarisha Heshima na Kusaidia Familia Iwe na Amani na Furaha

Njia za Kuimarisha Heshima na Kusaidia Familia Iwe na Amani na Furaha

  1. Kutumia mawasiliano mazuri na wapendwa wako ili kuimarisha uhusiano kati yenu. Hakikish... Read More

Kufanya Mapenzi na Kuzeeka: Kufurahia Intimiteti katika Hatua Zote za Maisha

Kufanya Mapenzi na Kuzeeka: Kufurahia Intimiteti katika Hatua Zote za Maisha

Kufanya Mapenzi na Kuzeeka: Kufurahia Intimiteti katika Hatua Zote za Maisha

Kuna wakati m... Read More

Mambo 6 ambayo ni siri ya mwanamke na sio rahisi kukwambia

Mambo 6 ambayo ni siri ya mwanamke na sio rahisi kukwambia

1. Idadi ya wapenzi wake wa zamani

Wanaume wengi hupenda kujua wao ni wangapi kuwa na mw... Read More