Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMS๐Ÿ’Œ๐Ÿ’•
โ˜ฐ
AckyShine

Jifunze kitu kupitia kisa hiki cha mume na mke

Featured Image

Mwanaume mmoja alimuoa mwanamke mrembo. Alikuwa akimpenda sana. Siku moja mwanamke alipatwa na maradhi ya ngozi. Kidogokidogo alianza kupoteza urembo wake.
.
.
.


Mume alipata safari na wakati akirudi alipata ajali iliyomfanya apoteze uwezo wake wa kuona. Hata hivyo, maisha yao ya ndoa yaliendelea kama kawaida. Lakini kadiri siku zilivyosonga mbele ndivyo mke alivyoendelea kupoteza urembo wake. Kwa kuwa mume alikuwa kipofu hakulijua hilo na hivyo hakuna kilichobadilika kwenye upendo wao. Aliendelea kumpenda, na mke alimpenda sana mumewe.
.
.
.


Siku moja mke alifariki dunia. Ilikuwa huzuni kubwa sana kwa mume.
Baada ya kumaliza taratibu zote za maziko, mazishi na kutandua msiba, alipanga kuhama kwenye mji huo na kwenda kuishi kwenye mji mwingine.
.
.
.


Mtu mmoja aliposikia habari hiyo alimwendea na kumuuliza: โ€œSasa utawezaje kutembea peke yako? Maana siku zote hizi mkeo alikuwa akikusaidia kukuonesha njia.โ€


Akajibu: โ€œMimi si kipofu. Nilifanya ionekane hivyo kwa sababu angejua kwamba ninauona mwili wake ulivyobadilika kuwa mbaya angepata maumivu makubwa zaidi kuliko ugonjwa wake wenyewe. Alikuwa mke mwema sana. Nilitaka aendelee kuwa na furaha.โ€
.
.
.


FUNZO:


Wakati fulani ni vizuri ukajifanya kipofu na kuyapuuza mapungufu ya mwenzako ili kumfanya awe mwenye furaha.


Meno huungโ€™ata ulimi mara nyingi, lakini vinaendelea kuishi pamoja kinywani. Huo ndio moyo wa KUSAMEHEANA. Macho hayaonani, lakini yanatazama na kuona vitu kwa pamoja, hupepesa na kulia pamoja. Huo unaitwa UMOJA.


1. Ukiwa peke yako unaweza kuongea, lakini ukiwa pamoja na mwenzako mnaweza KUZUNGUMZA.


2. Ukiwa peke yako unaweza KUFURAHI, lakini ukiwa na mwenzako unaweza KUFURAHIA.


3. Ukiwa peke yako unaweza KUTABASAMU, lakini ukiwa na mwenzako mnaweza KUCHEKA.


Huo ndio UZURI wa mahusiano yetu kama binadamu. Tunategemeana.


Kiwembe kina ukali lakini hakiwezi kukata mti; shoka lina nguvu na imara lakini haliwezi kukata nywele.


*Kila mtu ni muhimu kulingana na kusudio na lengo la uwepo wake. Usimdharau mtu yeyote kwa hali yoyote, kwa sababu huwezi kuwa yeye.


Mwenyezi Mungu atujaalie nguvu na moyo wa kusamehe, kustahmiliana na kuishi kwa umoja.
.
Tafakari
Mm na ww tunaweza kufanya haya!!!






Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE




Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke





Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.





[products columns="2" ids="30827"]


AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu ndoto na malengo ya maisha yenu

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu ndoto na malengo ya maisha yenu

Kama wapenzi, ni muhimu sana kujadili ndoto na malengo ya maisha yenu. Kuwa na mawazo sawa juu ya... Read More

Jinsi ya Kujenga Furaha ya Kweli katika Maisha ya Familia

Jinsi ya Kujenga Furaha ya Kweli katika Maisha ya Familia

  1. Kuwa na mawasiliano bora: Kujenga furaha ya kweli katika maisha ya familia ni lazima ku... Read More

Njia za Kupata Msichana Mzuri wa Kuwa Naye Maisha Yote

Njia za Kupata Msichana Mzuri wa Kuwa Naye Maisha Yote

Njia za Kupata Msichana Mzuri wa Kuwa Naye Maisha Yote

Kila mwanamume anataka kupata msich... Read More

Mbinu za Kujenga Upendo na Shukrani Ndani ya Familia: Mwongozo wa Mtaalamu

```html

Njia za Kujenga Utamaduni wa Upendo na Shukrani Ndani ya Familia: Msingi wa Furaha na Ms... Read More

Jinsi ya Kutambua Ishara za Upendo kutoka kwa Msichana

Jinsi ya Kutambua Ishara za Upendo kutoka kwa Msichana

Upendo ni hisia ambazo zinafanya maisha kuwa na maana zaidi. Kila mtu anapaswa kupata upendo, na ... Read More

Njia za Kuimarisha Ushirikiano wa Kijamii na Kuwa na Maisha ya Kijamii katika Familia

Njia za Kuimarisha Ushirikiano wa Kijamii na Kuwa na Maisha ya Kijamii katika Familia

Njia za Kuimarisha Ushirikiano wa Kijamii na Kuwa na Maisha ya Kijamii katika Familia

Fami... Read More

Je, ngono/kufanya mapenzi ni sehemu muhimu ya uhusiano wa kimapenzi?

Je, ngono/kufanya mapenzi ni sehemu muhimu ya uhusiano wa kimapenzi?

Je, ngono/kufanya mapenzi ni sehemu muhimu ya uhusiano wa kimapenzi?

Kwa wengi, kufanya ma... Read More

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya historia na utamaduni wa jamii yenu

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya historia na utamaduni wa jamii yenu

Siku zote ni muhimu kuwa na mawasiliano mazuri na mpenzi wako, na moja ya mambo muhimu ni kuwasil... Read More

Kukabiliana na Mazoea ya Kutowajibika katika Familia: Kuweka Nafasi ya Ushiriki na Ushirikiano

Kukabiliana na Mazoea ya Kutowajibika katika Familia: Kuweka Nafasi ya Ushiriki na Ushirikiano

Mazoea ya kutowajibika katika familia ni kitu ambacho kinaweza kusababisha migogoro kati ya wanaf... Read More

Jinsi ya Kuelewa na kuheshimu mafanikio na changamoto za kazi za mpenzi wako

Jinsi ya Kuelewa na kuheshimu mafanikio na changamoto za kazi za mpenzi wako

Kama mpenzi wako ana kazi, ni muhimu kuelewa na kuheshimu mafanikio na changamoto zake. Hii itaon... Read More

Vidokezo vya Kujenga Ukaribu na Msichana Wako

Vidokezo vya Kujenga Ukaribu na Msichana Wako

  1. Anza kwa kujenga urafiki mzuri Kabla ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi, ni muhimu kujeng... Read More

Jinsi ya Kupata Msichana wa Kuwa na Uhusiano wa Mbali

Jinsi ya Kupata Msichana wa Kuwa na Uhusiano wa Mbali

Jinsi ya Kupata Msichana wa Kuwa na Uhusiano wa Mbali

Kuwa na uhusiano wa mbali sio rahisi... Read More