Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMS๐Ÿ’Œ๐Ÿ’•
โ˜ฐ
AckyShine

Ushauri wa ukweli Ili Uwe mwanaume wa Ukweli

Featured Image

1. Ukija kijiweni au pub au kwenye nyama choma acha zile stori za sijui umesoma wapi hadi wapi, sijui una madigirii mangapi. Piga stori nyingine, mbona ziko nyingi tu. Kujielezea sana shule yako ni ushamba fulani hivi, dizaini kama hujiamini so lazima ujivishe nyota. Unaboa.


2. Tembea na keshi mfukoni kama vipi, stori za kadi yangu ya benki imegoma sio ishu.


3. Punguza mambo yako ya kuvaa sana kipapaa. Sometimes ibuka na pensi na jinsi tu mwana.


4. Punguza kukesha nje mfululizo, iwe umeoa, una mpenzi au upo upo. Kikanuni kabisa usikae nje hadi usiku wa manane siku tatu mfululizo labda uwepo mchongo wa maana sana. I mean wa maana sana.


5. Epuka sana mchezo wa kujipiga tattoos. Kuna watu wamekosa wake au michongo hevi in life kisa hizo mambo.


6. Nasisitiza sana epuka kumtaka mpenzi wa zamani wa mshikaji wako. Pigia mstari hii pointi. Kwani lazima upite palepale? Tusiishi kikondoo bro.


7. Jiunge walau na mtandao mmoja wa kijamii. Keep in touch na washikaji. Kuna wana toka mmemaliza primary hamjachekiana, utawakuta mitandaoni. Unaweza kupata mchongo au kujifunza ishu mbili tatu, au kuwa fala zaidi ukiamua.


8. Maisha mafupi sana, jitahidi kupunguza kukunja ndita. Jiachie mara moja moja.


9. Ukifika baa uwe tayari unajua unakunywa nini. Sio Mhudumu anakuja kukusikiliza unawaaaaaza. Inaonyesha hujisomi na huna mipango. Samahani lakini.


10. Kama hujaalikwa kwenye ishu, usiende mwanangu. Sometimes hata ukialikwa usiende pia. Unaweza kualikwa ili useme no, kiushahidi tu.


11. Halafu tumechoka wewe kuwa kituko ukilewa. Kama pombe huziwezi ziache, piga juisi tu au maji wakati wana tunapiga monde, sio kesi, ni uwezo tu wa kuhimili.


12. Toa tip bila kuomba namba ya baamedi basi mwanangu. Jifanye kama umetoa tu msaada. Hata simba sio swala wote huwa anawala porini, wengine anawacheki anapita zake.


13. Punguza kutumia simu sana, tena wakati mwingine kwa ishu ambazo hazina mpango.
Ukumbuke juzi juzi hapa wataalamu wamesema simu zinaleta ugumba.


14. Nunua tumiwani twa jua twa bei bei hivi, inakupa mwonekano wa kijentlomani sometimes.


15. Piga push-ups walau 50, sit ups na dips kabla ya kuoga asubuhi, hii afya tumeazimwa tu, jiweke fit.


16. Toka out na washikaji zako at least mara moja kwa mwezi mpige msosi na kinywaji. Wife au demu wako na wanao waache home! Sio kila kona kila siku uko nao kama mkoba, kichwa kitatia kutu.


17. Julikana walau hata baa mbili tatu au sehemu mbili tatu. Baa, basketball ground, soccer ground, acha kujikunyata home. Wewe mtoto wa kiume man.


18. Jifanye mjuaji sometimes, then jifunze baadaye. Sio kila kitu wewe ni โ€œI donโ€™t knowโ€.


19. Beer moja au glass moja ya wine baada ya mlo haiwezi kukuvurga, kama hutaki, kunywa majuisi yako basi ulete inzi, au misoda ujijazie magonjwa.


20. MTOTO WA KIUME HAPIGI SELFIE OVYO OVYO NA KUBINUA MIDOMO na KULAMBA LIPSI. PIGA SELFIE KWENYE ISHU MUHIMU. FAMILIA HIVI, DEMU MKALI, etc. Umenisoma?


21. Ukiweza miliki hata panga ghetto, maana bastola najua ngumu. Sio nyumba nzima huna hata kasilaha kadogo.


22. Ridhika. Hamna hata siku moja utakuwa na kila kitu. Jifunze kushukuru kwa ulicho nacho.


23. Sometimes agiza matunda badala ya chipsi.


24. Ukikutana na demu mzuri kiwanja yuko peke yake, muongeleshe.


25. Miliki walau suti moja kabla hujapitisha miaka 30 bro. Please. Na tupafyumu.


26. Kuwa na mpenzi moja
kwa wakati mmoja. Anatosha sana. Trust me.


27. Ukitaka kujilinganisha, jilinganishe wewe wa jana na wewe wa leo. Utafika mbali. Ukijilinganisha na wana utapasuka kichwa.


28. Piga picha nyingi kwa camera (again, sio selfies) tunza kumbukumbu.


29. Ukialikwa kwenye party usiende mikono mitupu. Nenda walau na kachupa kamoja ka mvinyo.


30. Date demu nje ya wale unaokutana nao club au baa mara wa mara. Utakuja kuniambia faida zake.


31. Huwezi kuwa mpenzi wa pombe au sigara kwa sababu hivyo vitu havitakaa vikupende.


32. Hata siku moja usirudiane na demu aliyekuacha kisa huna mkwanja. Kaenda kutafuta kakosa ndio maana kakurudia labda baada ya kuona umepata. Siku akikutana na mwenye chambi kukuzidi? Jibu kaa nalo.


33. Sometimes jitoe out mwenyewe, kaa mahali piga msosi wako na kinywaji chako, tafakari ishu zako. Alone.


34. Jisomee ukiwa na time. Inakupa chance kuazima ubongo wa mtu mwingine lakini pia inakupa matirio kwenye maongezi, ila stori za kuja kwenye joint na washikaji na kuanza kusema oh nimesoma kitabu hiki na kile kausha!


35. Puuza wanaozomea. Huwa wamekaa viti vile vya bei rahisi.


36. Hata siku moja usiseme โ€œNdo hivyo bwana, hamna namna tenaโ€. Ipo namna bro.


37. Usi-bet kama ukipoteza buku 5 we ni mtu wa kulia lia kindezi.


38. Muombe na Mshukuru Mungu wako. Kama huna Mungu jishukuru mwenyewe, kiazi wewe.


39. Kumbuka, sheria hufuatwa na wajinga lakini huwaongoza wenye busara.






Kama Mwanamme Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE




[products columns="2" ids="30827"]


AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Kukabiliana na Mazoea ya Kukosa Mawasiliano katika Mahusiano: Kuunda Nafasi ya Mazungumzo

Kukabiliana na Mazoea ya Kukosa Mawasiliano katika Mahusiano: Kuunda Nafasi ya Mazungumzo

Mawasiliano ni muhimu sana katika mahusiano. Hata hivyo, kuna wakati tunapokumbana na changamoto ... Read More

Jinsi ya Kufanya Familia kuwa Kitovu cha Huduma na Kujitolea: Kuleta Mabadiliko Chanya

Jinsi ya Kufanya Familia kuwa Kitovu cha Huduma na Kujitolea: Kuleta Mabadiliko Chanya

  1. Kuanzisha mazungumzo ya familia: Familia inapaswa kuwa kitovu cha huduma na kujitolea. ... Read More

Je, nini imani ya watu katika kuzungumza waziwazi juu ya ngono/kufanya mapenzi na kutokuwa na aibu?

Je, nini imani ya watu katika kuzungumza waziwazi juu ya ngono/kufanya mapenzi na kutokuwa na aibu?

Habari rafiki yangu! Leo tutaongea kuhusu umuhimu wa kuzungumza waziwazi juu ya ngono na kufanya ... Read More

Kuelewa na Kuheshimu Matakwa ya Kijinsia: Kuunda Mazingira Salama na Furaha

Kuelewa na Kuheshimu Matakwa ya Kijinsia: Kuunda Mazingira Salama na Furaha

  1. Kuelewa na kuheshimu matakwa ya kijinsia ni jambo muhimu katika kujenga mazingira salama na... Read More
Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu maadili na maadili ya familia

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu maadili na maadili ya familia

Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu maadili na maadili ya familia ni muhimu kwa kujenga msingi imara k... Read More
Je, kuna umuhimu wa kujadili haki na usawa katika uhusiano wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu wa kujadili haki na usawa katika uhusiano wa ngono/kufanya mapenzi?

Kila siku, tunaishi katika jamii ambayo ina maadili na kanuni za kufuata katika uhusiano wa ngono... Read More

Je, watu wanapendelea kujaribu mbinu za kuleta msisimko wa kihisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, watu wanapendelea kujaribu mbinu za kuleta msisimko wa kihisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Leo, tutazungumzia kuhusu mbinu za kuleta msisimko wa kihisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi. Ni... Read More

Je, nini imani ya watu katika kutumia mawasiliano ya kimwili kama ishara ya mapenzi wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, nini imani ya watu katika kutumia mawasiliano ya kimwili kama ishara ya mapenzi wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, nini imani ya watu katika kutumia mawasiliano ya kimwili kama ishara ya mapenzi wakati wa ngo... Read More

Je, kuna umuhimu wa kujadili kuhusu upendeleo wako wa ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Je, kuna umuhimu wa kujadili kuhusu upendeleo wako wa ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Upendeleo wa ngono na kufanya mapenzi ni jambo muhimu katika mahusiano yetu ya kimapenzi. Inapasw... Read More

Njia za Kupunguza Mazoea ya Kukosa Uwiano na Kuunda Amani na Furaha katika Familia

Njia za Kupunguza Mazoea ya Kukosa Uwiano na Kuunda Amani na Furaha katika Familia

Familia ni kitu muhimu sana katika maisha ya kila mtu. Ni katika familia ndipo tunapopata upendo,... Read More

Njia za Kuimarisha Ushirikiano wa Kijamii na Kuwa na Urafiki katika Familia

Njia za Kuimarisha Ushirikiano wa Kijamii na Kuwa na Urafiki katika Familia

Ushirikiano wa kijamii ni jambo muhimu sana katika maisha yetu. Ni muhimu kwa sababu inatupa furs... Read More

Jinsi ya Kuelewa na kukabiliana na changamoto za kulea watoto na mpenzi wako

Jinsi ya Kuelewa na kukabiliana na changamoto za kulea watoto na mpenzi wako

Kulea watoto na mpenzi wako ni moja ya majukumu magumu yanayoweza kuwa na changamoto nyingi. Kuna... Read More