Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMS๐Ÿ’Œ๐Ÿ’•
โ˜ฐ
AckyShine

Ushauri wa ukweli Ili Uwe mwanaume wa Ukweli

Featured Image

1. Ukija kijiweni au pub au kwenye nyama choma acha zile stori za sijui umesoma wapi hadi wapi, sijui una madigirii mangapi. Piga stori nyingine, mbona ziko nyingi tu. Kujielezea sana shule yako ni ushamba fulani hivi, dizaini kama hujiamini so lazima ujivishe nyota. Unaboa.


2. Tembea na keshi mfukoni kama vipi, stori za kadi yangu ya benki imegoma sio ishu.


3. Punguza mambo yako ya kuvaa sana kipapaa. Sometimes ibuka na pensi na jinsi tu mwana.


4. Punguza kukesha nje mfululizo, iwe umeoa, una mpenzi au upo upo. Kikanuni kabisa usikae nje hadi usiku wa manane siku tatu mfululizo labda uwepo mchongo wa maana sana. I mean wa maana sana.


5. Epuka sana mchezo wa kujipiga tattoos. Kuna watu wamekosa wake au michongo hevi in life kisa hizo mambo.


6. Nasisitiza sana epuka kumtaka mpenzi wa zamani wa mshikaji wako. Pigia mstari hii pointi. Kwani lazima upite palepale? Tusiishi kikondoo bro.


7. Jiunge walau na mtandao mmoja wa kijamii. Keep in touch na washikaji. Kuna wana toka mmemaliza primary hamjachekiana, utawakuta mitandaoni. Unaweza kupata mchongo au kujifunza ishu mbili tatu, au kuwa fala zaidi ukiamua.


8. Maisha mafupi sana, jitahidi kupunguza kukunja ndita. Jiachie mara moja moja.


9. Ukifika baa uwe tayari unajua unakunywa nini. Sio Mhudumu anakuja kukusikiliza unawaaaaaza. Inaonyesha hujisomi na huna mipango. Samahani lakini.


10. Kama hujaalikwa kwenye ishu, usiende mwanangu. Sometimes hata ukialikwa usiende pia. Unaweza kualikwa ili useme no, kiushahidi tu.


11. Halafu tumechoka wewe kuwa kituko ukilewa. Kama pombe huziwezi ziache, piga juisi tu au maji wakati wana tunapiga monde, sio kesi, ni uwezo tu wa kuhimili.


12. Toa tip bila kuomba namba ya baamedi basi mwanangu. Jifanye kama umetoa tu msaada. Hata simba sio swala wote huwa anawala porini, wengine anawacheki anapita zake.


13. Punguza kutumia simu sana, tena wakati mwingine kwa ishu ambazo hazina mpango.
Ukumbuke juzi juzi hapa wataalamu wamesema simu zinaleta ugumba.


14. Nunua tumiwani twa jua twa bei bei hivi, inakupa mwonekano wa kijentlomani sometimes.


15. Piga push-ups walau 50, sit ups na dips kabla ya kuoga asubuhi, hii afya tumeazimwa tu, jiweke fit.


16. Toka out na washikaji zako at least mara moja kwa mwezi mpige msosi na kinywaji. Wife au demu wako na wanao waache home! Sio kila kona kila siku uko nao kama mkoba, kichwa kitatia kutu.


17. Julikana walau hata baa mbili tatu au sehemu mbili tatu. Baa, basketball ground, soccer ground, acha kujikunyata home. Wewe mtoto wa kiume man.


18. Jifanye mjuaji sometimes, then jifunze baadaye. Sio kila kitu wewe ni โ€œI donโ€™t knowโ€.


19. Beer moja au glass moja ya wine baada ya mlo haiwezi kukuvurga, kama hutaki, kunywa majuisi yako basi ulete inzi, au misoda ujijazie magonjwa.


20. MTOTO WA KIUME HAPIGI SELFIE OVYO OVYO NA KUBINUA MIDOMO na KULAMBA LIPSI. PIGA SELFIE KWENYE ISHU MUHIMU. FAMILIA HIVI, DEMU MKALI, etc. Umenisoma?


21. Ukiweza miliki hata panga ghetto, maana bastola najua ngumu. Sio nyumba nzima huna hata kasilaha kadogo.


22. Ridhika. Hamna hata siku moja utakuwa na kila kitu. Jifunze kushukuru kwa ulicho nacho.


23. Sometimes agiza matunda badala ya chipsi.


24. Ukikutana na demu mzuri kiwanja yuko peke yake, muongeleshe.


25. Miliki walau suti moja kabla hujapitisha miaka 30 bro. Please. Na tupafyumu.


26. Kuwa na mpenzi moja
kwa wakati mmoja. Anatosha sana. Trust me.


27. Ukitaka kujilinganisha, jilinganishe wewe wa jana na wewe wa leo. Utafika mbali. Ukijilinganisha na wana utapasuka kichwa.


28. Piga picha nyingi kwa camera (again, sio selfies) tunza kumbukumbu.


29. Ukialikwa kwenye party usiende mikono mitupu. Nenda walau na kachupa kamoja ka mvinyo.


30. Date demu nje ya wale unaokutana nao club au baa mara wa mara. Utakuja kuniambia faida zake.


31. Huwezi kuwa mpenzi wa pombe au sigara kwa sababu hivyo vitu havitakaa vikupende.


32. Hata siku moja usirudiane na demu aliyekuacha kisa huna mkwanja. Kaenda kutafuta kakosa ndio maana kakurudia labda baada ya kuona umepata. Siku akikutana na mwenye chambi kukuzidi? Jibu kaa nalo.


33. Sometimes jitoe out mwenyewe, kaa mahali piga msosi wako na kinywaji chako, tafakari ishu zako. Alone.


34. Jisomee ukiwa na time. Inakupa chance kuazima ubongo wa mtu mwingine lakini pia inakupa matirio kwenye maongezi, ila stori za kuja kwenye joint na washikaji na kuanza kusema oh nimesoma kitabu hiki na kile kausha!


35. Puuza wanaozomea. Huwa wamekaa viti vile vya bei rahisi.


36. Hata siku moja usiseme โ€œNdo hivyo bwana, hamna namna tenaโ€. Ipo namna bro.


37. Usi-bet kama ukipoteza buku 5 we ni mtu wa kulia lia kindezi.


38. Muombe na Mshukuru Mungu wako. Kama huna Mungu jishukuru mwenyewe, kiazi wewe.


39. Kumbuka, sheria hufuatwa na wajinga lakini huwaongoza wenye busara.






Kama Mwanamme Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE




[products columns="2" ids="30827"]


AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Ushawishi wa Mazingira ya Kijinsia katika Mtazamo wetu wa Kufanya Mapenzi: Kuchunguza na Kubadili Dhana

Ushawishi wa Mazingira ya Kijinsia katika Mtazamo wetu wa Kufanya Mapenzi: Kuchunguza na Kubadili Dhana

  1. Ushawishi wa mazingira ya kijinsia katika mtazamo wetu wa kufanya mapenzi ni suala amba... Read More

Jinsi ya Kutunza Afya yako Mwenyewe wewe kama Mwanamme

Jinsi ya Kutunza Afya yako Mwenyewe wewe kama Mwanamme

Read More
Vidokezo vya Kuwa na Uhusiano Mzuri na Msichana

Vidokezo vya Kuwa na Uhusiano Mzuri na Msichana

Mara nyingi, wanaume wamekuwa wakipata wakati mgumu kuwa na uhusiano mzuri na msichana. Inawezeka... Read More

Jinsi ya Kuwa na Mazungumzo ya Kina na Msichana

Jinsi ya Kuwa na Mazungumzo ya Kina na Msichana

Wanaume wengi huwa na shida katika kuongea na wanawake, hasa katika mazungumzo ya kina. Hii mara ... Read More

Kuweka Kipaumbele cha Furaha na Ustawi wa Kila Mwanafamilia katika Familia Yako

Kuweka Kipaumbele cha Furaha na Ustawi wa Kila Mwanafamilia katika Familia Yako

Karibu katika makala hii kuhusu kuweka kipaumbele cha furaha na ustawi wa kila mwanafamilia katik... Read More

Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali baada ya kurusha voko a.k.a kutongoza

Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali baada ya kurusha voko a.k.a kutongoza

Dalili ni hizi;

Anaongeza ukaribu

Ukiona anapenda kuwa karbu na wewe na kuandaman... Read More

Jinsi ya Kutatua Migogoro na mke wako kwa Amani

Jinsi ya Kutatua Migogoro na mke wako kwa Amani

Kutatua migogoro na mke wako kwa amani ni muhimu katika kudumisha uhusiano mzuri na wenye afya. Hapa... Read More
Jinsi ya Kugawana Majukumu ya Nyumbani na mke wako

Jinsi ya Kugawana Majukumu ya Nyumbani na mke wako

Kugawana majukumu ya nyumbani ni muhimu katika kujenga usawa na ushirikiano katika ndoa. Hapa kuna n... Read More
Jinsi ya Kuelewa na kuheshimu mahitaji ya faragha na nafasi ya kibinafsi na mpenzi wako

Jinsi ya Kuelewa na kuheshimu mahitaji ya faragha na nafasi ya kibinafsi na mpenzi wako

Kuelewa na kuheshimu mahitaji ya faragha na nafasi ya kibinafsi ya mpenzi wako ni muhimu katika kuje... Read More
Je, watu wana amini katika kutumia mbinu za kujizuia mimba wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, watu wana amini katika kutumia mbinu za kujizuia mimba wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Salamu! Karibu kwenye makala ya leo kuhusu mbinu za kujizuia mimba wakati wa ngono. Ni jambo muhi... Read More

Kuweka Kipaumbele cha Uhusiano wa Karibu na Kuweka Nafasi ya Wakati wa Familia

Kuweka Kipaumbele cha Uhusiano wa Karibu na Kuweka Nafasi ya Wakati wa Familia

Kuweka Kipaumbele cha Uhusiano wa Karibu na Kuweka Nafasi ya Wakati wa Familia

Kuweka kipa... Read More

Kujenga Ushirikiano wenye Uwiano na Kuhamasisha Uadilifu katika Familia

Kujenga Ushirikiano wenye Uwiano na Kuhamasisha Uadilifu katika Familia

Kujenga Ushirikiano Wenye Uwiano na Kuhamasisha Uadilifu katika Familia

Familia ni moja ya... Read More