Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Magonjwa ya zinaa na dalili zake

Featured Image
Kuna magonjwa mengi tofauti ya zinaa, lakini yale ambayo yameenea sana ni kisonono, kaswende, klamdia, kankroidi, utando mweupe , Virusi vya UKIMWI na UKIMWI. Shida kubwa ya magonjwa mengi ya zinaa ni kwamba dalili zake hazionekani kwa urahisi na kama yasipotibiwa kikamilifu yanaweza kuleta madhara makubwa. Maelezo kuhusu magonjwa ya zinaa yaliyoenea sana ni kama yafuatayo:

Kisonono:


Huchukua muda wa siku 1 hadi 14 tangu kuambukizwa mpaka kuonyesha dalili za kuumwa. Kwa wanawake dalili za kisonono ni maumivu chini ya tumbo ambayo yanaweza kuambatana na homa na kutokwa uchafu ukeni. Wapo wanawake wengine ambao hawaoni dalili zozote. Kwa wanaume dalili ni kutokwa na usaha uumeni na kupata maumivu wakati wa kukojoa. Athari yake kwa mwanamke ni kuziba mirija ya kupitisha mayai na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi, na vilevile ugumba. Kwa mtoto aliye tumboni mwa mama mjamzito kisonono cha mama yake kinaweza kusababisha upofu. Kwa mwanaume athari yake ni kuziba mirija ya kupitisha mkojo.
The ListPages module does not work recursively.

Kaswende:


Dalili ya kaswende kwa mwanamke ni vidonda sehemu za siri hasa kwenye mashavu ya uke na sehemu ya njia ya haja kubwa, pamoja na sundosundo sehemu ya siri. Kwa mwanaume dalili ni vidonda. Mara nyingi kimoja kwenye kichwa cha uume, kwenye kishina cha uume na kuzunguka njia ya haja kubwa. Pia mwanaume anaweza kupata sundosundo sehemu za siri. Ugonjwa huu husababisha matatizo ya moyo, na kuharibu ubongo na kuzaa watoto walemavu.

Klamdia:


Dalili yake kwa mwanamke mara nyingi siyo rahisi kuonekana. Kwa mwanaume dalili ni kupata maumivu wakati wa kukojoa, na kukojoa mara kwa mara. Athari kwa mwanamke ni kuziba kwa mirija ya kupitisha mayai na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi. Mimba hizi kuhatarisha maisha ya mama na kuleta ugumba vinaweza kutokea. Kwa mwanaume athari ni kuziba mirija ya kupitisha mbegu na utasa.
The ListPages module does not work recursively.

Kankroidi:


Dalili yake ni vidonda sehemu za siri vinavyokuwa na maumivu makali, maumivu wakati mkojo unapopita kwenye vidonda na kuvimba tezi sehemu za siri. Tezi huweza kupasuka na kutoa uchafu na maumivu makali.

Utando mweupe:


Dalili kwa mwanamke ni kutokwa na uchafu ukeni (kama maziwa yaliyoganda), kuwashwa na kuwa na michubuko sehemu za siri. Kwa mwanaume ni kuwashwa sehemu za siri na kusikia maumivu wakati wa kukojoa. Athari ni maumivu wakati wa kujamiiana.
The ListPages module does not work recursively.

Virusi vya UKIMWI:


Katika hatua ya mwanzo baada ya kuambukizwa hakuna dalili maalum. Hatua hii inaweza kuchukua mpaka miaka kumi. Lakini mara mtu anapoanza kuugua UKIMWI dalili zinakuwa nyingi. Pamoja na kupungua kinga ya mwili, kupungua uzito na kuumwa mara kwa mara. Matokeo ya kuugua UKIMWI baada ya muda fulani ni kifo.
AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Je, ni muhimu kuwa na usawa wa ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Je, ni muhimu kuwa na usawa wa ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Habari za leo wapenzi! Sijui kama umewahi kujiuliza kuhusu umuhimu wa usawa wa ngono/kufanya mape... Read More

Kwa nini watu wasio na ualbino wanaogopa kuoa Albino kwa imani kuwa watawazalia watoto Albino?

Kwa nini watu wasio na ualbino wanaogopa kuoa Albino kwa imani kuwa watawazalia watoto Albino?

Ualbino ni hali ya
kurithi, hii inamaanisha
kuwa unapata ualbino
kutoka kwa wazazi... Read More

Je, mapacha wanapatikanaje?

Je, mapacha wanapatikanaje?

Zipo aina mbili za mapacha, wale wanaofanana na wale wasiofanana. Karibu robo ya mapacha wote hufana... Read More
Ushauri kwa mtu aliyebakwa

Ushauri kwa mtu aliyebakwa

Jambo la kwanza jaribu kumwondoa hofu mwathiriwa na
muliwaze maana amepata jambo la kutisha.... Read More

Je, kwa nini inatokea kuzaa mtoto mlemavu?

Je, kwa nini inatokea kuzaa mtoto mlemavu?

Kuna aina mbalimbali za ulemavu na kuna sababu mbalimbali za kuzaa mtoto mlemavu. Ulemavu wa mtot... Read More

Kwa nini Albino hawapewi kazi kwa mtazamo kwamba hawawezi kazi?

Kwa nini Albino hawapewi kazi kwa mtazamo kwamba hawawezi kazi?

Watu wengi katika jamii hawana uelewa unaotosheleza kuhusu
ulemavu wa ngozi na ulemavu wa ma... Read More

Je, ni muhimu kujadili mipaka na dhibitisho wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, ni muhimu kujadili mipaka na dhibitisho wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, ni muhimu kujadili mipaka na dhibitisho wakati wa ngono/kufanya mapenzi? Ndio, ni muhimu sana... Read More

Watu wanasema kuwa unaweza kupona UKIMWI kwa kujamiiana na Albino. Hii ni kweli?

Watu wanasema kuwa unaweza kupona UKIMWI kwa kujamiiana na Albino. Hii ni kweli?

Watu wanaweza kuvumisha uongo wowote ili kupotosha
ukweli na kufanya mambo yao maovu wanayoy... Read More

Kwa nini ngozi ya Albino inafanana ya watu weupe?

Kwa nini ngozi ya Albino inafanana ya watu weupe?

Ngozi ya Albino ina ukosefu wa rangi. Inaonekana kama ya watu
weupe ambao wana kiasi cha pig... Read More

Mafuta kwenye kondomu

Mafuta kwenye kondomu

Mafuta yanayowekwa kwenye pakiti ya kondomu ni mafuta maalum na yana kazi ya kuhifadhi kondomu mp... Read More

Je , vipimo vya Virusi vya UKIMWI vinasema ukweli?

Je , vipimo vya Virusi vya UKIMWI vinasema ukweli?

Uwezekano wa kupata majibu ya uwongo ni mdogo sana, isipokuwa tu kama vipimo vitafanyika kipindi ... Read More

Je, Ni Vipi Kuepuka Kufanya Ngono Kwa Sababu ya Kubembelezwa?

Je, Ni Vipi Kuepuka Kufanya Ngono Kwa Sababu ya Kubembelezwa?

Je, Ni Vipi Kuepuka Kufanya Ngono Kwa Sababu ya Kubembelezwa? 😊✨

Karibu rafiki yangu!... Read More