Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Magonjwa ya zinaa na dalili zake

Featured Image
Kuna magonjwa mengi tofauti ya zinaa, lakini yale ambayo yameenea sana ni kisonono, kaswende, klamdia, kankroidi, utando mweupe , Virusi vya UKIMWI na UKIMWI. Shida kubwa ya magonjwa mengi ya zinaa ni kwamba dalili zake hazionekani kwa urahisi na kama yasipotibiwa kikamilifu yanaweza kuleta madhara makubwa. Maelezo kuhusu magonjwa ya zinaa yaliyoenea sana ni kama yafuatayo:

Kisonono:


Huchukua muda wa siku 1 hadi 14 tangu kuambukizwa mpaka kuonyesha dalili za kuumwa. Kwa wanawake dalili za kisonono ni maumivu chini ya tumbo ambayo yanaweza kuambatana na homa na kutokwa uchafu ukeni. Wapo wanawake wengine ambao hawaoni dalili zozote. Kwa wanaume dalili ni kutokwa na usaha uumeni na kupata maumivu wakati wa kukojoa. Athari yake kwa mwanamke ni kuziba mirija ya kupitisha mayai na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi, na vilevile ugumba. Kwa mtoto aliye tumboni mwa mama mjamzito kisonono cha mama yake kinaweza kusababisha upofu. Kwa mwanaume athari yake ni kuziba mirija ya kupitisha mkojo.
The ListPages module does not work recursively.

Kaswende:


Dalili ya kaswende kwa mwanamke ni vidonda sehemu za siri hasa kwenye mashavu ya uke na sehemu ya njia ya haja kubwa, pamoja na sundosundo sehemu ya siri. Kwa mwanaume dalili ni vidonda. Mara nyingi kimoja kwenye kichwa cha uume, kwenye kishina cha uume na kuzunguka njia ya haja kubwa. Pia mwanaume anaweza kupata sundosundo sehemu za siri. Ugonjwa huu husababisha matatizo ya moyo, na kuharibu ubongo na kuzaa watoto walemavu.

Klamdia:


Dalili yake kwa mwanamke mara nyingi siyo rahisi kuonekana. Kwa mwanaume dalili ni kupata maumivu wakati wa kukojoa, na kukojoa mara kwa mara. Athari kwa mwanamke ni kuziba kwa mirija ya kupitisha mayai na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi. Mimba hizi kuhatarisha maisha ya mama na kuleta ugumba vinaweza kutokea. Kwa mwanaume athari ni kuziba mirija ya kupitisha mbegu na utasa.
The ListPages module does not work recursively.

Kankroidi:


Dalili yake ni vidonda sehemu za siri vinavyokuwa na maumivu makali, maumivu wakati mkojo unapopita kwenye vidonda na kuvimba tezi sehemu za siri. Tezi huweza kupasuka na kutoa uchafu na maumivu makali.

Utando mweupe:


Dalili kwa mwanamke ni kutokwa na uchafu ukeni (kama maziwa yaliyoganda), kuwashwa na kuwa na michubuko sehemu za siri. Kwa mwanaume ni kuwashwa sehemu za siri na kusikia maumivu wakati wa kukojoa. Athari ni maumivu wakati wa kujamiiana.
The ListPages module does not work recursively.

Virusi vya UKIMWI:


Katika hatua ya mwanzo baada ya kuambukizwa hakuna dalili maalum. Hatua hii inaweza kuchukua mpaka miaka kumi. Lakini mara mtu anapoanza kuugua UKIMWI dalili zinakuwa nyingi. Pamoja na kupungua kinga ya mwili, kupungua uzito na kuumwa mara kwa mara. Matokeo ya kuugua UKIMWI baada ya muda fulani ni kifo.
AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Vidokezo vya Kuwa na Uwazi katika Uhusiano wako na Msichana

Vidokezo vya Kuwa na Uwazi katika Uhusiano wako na Msichana

Kuwa na uwazi katika uhusiano wako na msichana ni jambo muhimu kwa sababu inajenga uaminifu na up... Read More

Je, ukinywa pombe unaongeza damu?

Je, ukinywa pombe unaongeza damu?

Si kweli.
Pombe haiongezi damu, vitamini wala nguvu. Ukweli ni kwamba unywaji po... Read More

Je, watu wanamaaoni gani katika kuelewa na kuheshimu tofauti za kijinsia wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, watu wanamaaoni gani katika kuelewa na kuheshimu tofauti za kijinsia wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Kuheshimu tofauti za kijinsia wakati wa ngono/kufanya mapenzi ni jambo muhimu sana. Kila mtu anap... Read More

Ugumba wa mwanamke unasababishwa na nini?

Ugumba wa mwanamke unasababishwa na nini?

Ugumba wa mwanamke ni hali ya mwanamke kushindwa kupata mimba. Kama kwa wanaume kuna mambo mengi ... Read More

Ukubwa wa kondomu

Ukubwa wa kondomu

Kuna aina kondomu za ukubwa mbalimbali. Kwa wastani ukubwa wa kondomu unafaa kwa wanaume watu waz... Read More

Jinsi ya Kuonyesha Ukarimu kwa Msichana Wako

Jinsi ya Kuonyesha Ukarimu kwa Msichana Wako

Habari za leo! Leo nataka kuzungumza juu ya jinsi ya kuonyesha ukarimu kwa msichana wako. Kama mw... Read More

Vidokezo vya Kuonyesha Shukrani kwa Msichana Wako

Vidokezo vya Kuonyesha Shukrani kwa Msichana Wako

Hivi karibuni, wanaume wengi wamekuwa wakikosa jinsi ya kuonyesha shukrani kwa msichana wao. Hata... Read More

Je, kwa nini watu waanzao kutumia dawa za kulevya hupenda kuendelea kuzitumia?

Je, kwa nini watu waanzao kutumia dawa za kulevya hupenda kuendelea kuzitumia?

Hii ndio hasa sababu kwa nini dawa za kulevya ni hatari! Mara unapozizoea unakuwa na ugumu wa kue... Read More

Nikitumia nyembe kali au sindano pamoja na mtu mwenye Virusi vya UKIMWI ninaweza kupata Virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Nikitumia nyembe kali au sindano pamoja na mtu mwenye Virusi vya UKIMWI ninaweza kupata Virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Ndiyo, unaweza kuambukizwa ukitumia nyembe kali au sindano kwa kuchangia pamoja na mtu mwenye vir... Read More

Nifanyeje Kujikinga na Maambukizi ya magonjwa ya zinaa (STIs)?

Nifanyeje Kujikinga na Maambukizi ya magonjwa ya zinaa (STIs)?

Nifanyeje Kujikinga na Maambukizi ya Magonjwa ya Zinaa (STIs)?

Jambo wapenzi wa vijana! Le... Read More

Dalili za kwanza za msichana au mwanamke kuwa na mimba ni zipi?

Dalili za kwanza za msichana au mwanamke kuwa na mimba ni zipi?

Dalili moja i iliyo wazi zaidi ni kukosa hedhi. Mwanamke akijamii ana na mwanaume bila kutumia kinga... Read More
Nifanyeje Kuzungumzia Suala la Kukosa Hamu ya Ngono?

Nifanyeje Kuzungumzia Suala la Kukosa Hamu ya Ngono?

Nifanyeje Kuzungumzia Suala la Kukosa Hamu ya Ngono? 😊

  1. Jambo la kwanza kabisa... Read More