Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Magonjwa ya zinaa na dalili zake

Featured Image
Kuna magonjwa mengi tofauti ya zinaa, lakini yale ambayo yameenea sana ni kisonono, kaswende, klamdia, kankroidi, utando mweupe , Virusi vya UKIMWI na UKIMWI. Shida kubwa ya magonjwa mengi ya zinaa ni kwamba dalili zake hazionekani kwa urahisi na kama yasipotibiwa kikamilifu yanaweza kuleta madhara makubwa. Maelezo kuhusu magonjwa ya zinaa yaliyoenea sana ni kama yafuatayo:

Kisonono:


Huchukua muda wa siku 1 hadi 14 tangu kuambukizwa mpaka kuonyesha dalili za kuumwa. Kwa wanawake dalili za kisonono ni maumivu chini ya tumbo ambayo yanaweza kuambatana na homa na kutokwa uchafu ukeni. Wapo wanawake wengine ambao hawaoni dalili zozote. Kwa wanaume dalili ni kutokwa na usaha uumeni na kupata maumivu wakati wa kukojoa. Athari yake kwa mwanamke ni kuziba mirija ya kupitisha mayai na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi, na vilevile ugumba. Kwa mtoto aliye tumboni mwa mama mjamzito kisonono cha mama yake kinaweza kusababisha upofu. Kwa mwanaume athari yake ni kuziba mirija ya kupitisha mkojo.
The ListPages module does not work recursively.

Kaswende:


Dalili ya kaswende kwa mwanamke ni vidonda sehemu za siri hasa kwenye mashavu ya uke na sehemu ya njia ya haja kubwa, pamoja na sundosundo sehemu ya siri. Kwa mwanaume dalili ni vidonda. Mara nyingi kimoja kwenye kichwa cha uume, kwenye kishina cha uume na kuzunguka njia ya haja kubwa. Pia mwanaume anaweza kupata sundosundo sehemu za siri. Ugonjwa huu husababisha matatizo ya moyo, na kuharibu ubongo na kuzaa watoto walemavu.

Klamdia:


Dalili yake kwa mwanamke mara nyingi siyo rahisi kuonekana. Kwa mwanaume dalili ni kupata maumivu wakati wa kukojoa, na kukojoa mara kwa mara. Athari kwa mwanamke ni kuziba kwa mirija ya kupitisha mayai na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi. Mimba hizi kuhatarisha maisha ya mama na kuleta ugumba vinaweza kutokea. Kwa mwanaume athari ni kuziba mirija ya kupitisha mbegu na utasa.
The ListPages module does not work recursively.

Kankroidi:


Dalili yake ni vidonda sehemu za siri vinavyokuwa na maumivu makali, maumivu wakati mkojo unapopita kwenye vidonda na kuvimba tezi sehemu za siri. Tezi huweza kupasuka na kutoa uchafu na maumivu makali.

Utando mweupe:


Dalili kwa mwanamke ni kutokwa na uchafu ukeni (kama maziwa yaliyoganda), kuwashwa na kuwa na michubuko sehemu za siri. Kwa mwanaume ni kuwashwa sehemu za siri na kusikia maumivu wakati wa kukojoa. Athari ni maumivu wakati wa kujamiiana.
The ListPages module does not work recursively.

Virusi vya UKIMWI:


Katika hatua ya mwanzo baada ya kuambukizwa hakuna dalili maalum. Hatua hii inaweza kuchukua mpaka miaka kumi. Lakini mara mtu anapoanza kuugua UKIMWI dalili zinakuwa nyingi. Pamoja na kupungua kinga ya mwili, kupungua uzito na kuumwa mara kwa mara. Matokeo ya kuugua UKIMWI baada ya muda fulani ni kifo.
AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Je, watu wanaoishi na hali ya ualbino wanaweza kuzaa watoto bila matatizo?

Je, watu wanaoishi na hali ya ualbino wanaweza kuzaa watoto bila matatizo?

Ulemavu wa watu wanaoishi na ualbino hauingiliani na uwezo
wa kuweza kuzaa. Tuelewe kwamba u... Read More

Je, Ni Vipi Kupata Msaada wa Kielimu Kuhusu Ngono?

Je, Ni Vipi Kupata Msaada wa Kielimu Kuhusu Ngono?

Je, umewahi kujiuliza ni vipi unaweza kupata msaada wa kielimu kuhusu masuala ya ngono? Leo, tuta... Read More

Jinsi ya Kukabiliana na Ushinikizaji wa Kufanya Ngono kabla ya Wakati

Jinsi ya Kukabiliana na Ushinikizaji wa Kufanya Ngono kabla ya Wakati

Jinsi ya Kukabiliana na Ushinikizaji wa Kufanya Ngono kabla ya Wakati

Karibu vijana wapend... Read More

Je, watu wanapendelea ngono/kufanya mapenzi ya kawaida au ngono/kufanya mapenzi ya kufanya mazoezi ya kimwili?

Je, watu wanapendelea ngono/kufanya mapenzi ya kawaida au ngono/kufanya mapenzi ya kufanya mazoezi ya kimwili?

Habari rafiki! Karibu katika makala hii ambayo itakupa mwanga kuhusu kile watu wanapendelea kati ... Read More

Je, Ni Sahihi Kuanza Kujihusisha na Ngono nikiwa na Mpenzi Wangu?

Je, Ni Sahihi Kuanza Kujihusisha na Ngono nikiwa na Mpenzi Wangu?

Je, Ni Sahihi Kuanza Kujihusisha na Ngono nikiwa na Mpenzi Wangu? πŸ€”

Jambo zuri kujiuliz... Read More

Je, ngono/kufanya mapenzi inaathiri furaha ya uhusiano wa kimapenzi?

Je, ngono/kufanya mapenzi inaathiri furaha ya uhusiano wa kimapenzi?

Je, ngono/kufanya mapenzi inaathiri furaha ya uhusiano wa kimapenzi?

Haya ni maswali mengi... Read More

Kwa nini inapendekezwa Kufanya Ngono na Mtu Mmoja Tu?

Kwa nini inapendekezwa Kufanya Ngono na Mtu Mmoja Tu?

Kwa nini inapendekezwa Kufanya Ngono na Mtu Mmoja Tu? 🌟

Karibu vijana wenzangu! Leo tut... Read More

Nitafanya nini kuzuia dawa za kulevya na jinsi gani nitaepukana na marafiki wabaya?

Nitafanya nini kuzuia dawa za kulevya na jinsi gani nitaepukana na marafiki wabaya?

Wakati mwingine ni vigumu kusema hapana ukiwa na
maana ya hapana. Jaribu kuwa mpole na usiwe... Read More

Ni tahadhari gani nichukue ninapomhudumia mgonjwa wa UKIMWI?

Ni tahadhari gani nichukue ninapomhudumia mgonjwa wa UKIMWI?

Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI mara nyingi huenea sana kwa njia ya kujamii ana, na hauambukizwi ... Read More

Mtu anaweza kurithi uvutaji wa bangi?

Mtu anaweza kurithi uvutaji wa bangi?

Hapana, huwezi ukarithi uvutaji wa bangi. Lakini mara nyingi watoto huiga tabia za wazazi wao. Wa... Read More

Je, kuna vitu fulani ambavyo hupendezwa nayo katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna vitu fulani ambavyo hupendezwa nayo katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna vitu fulani ambavyo hupendezwa nayo katika ngono/kufanya mapenzi? Ndio, kuna mambo mengi... Read More

Je, watu wanapendelea ngono/kufanya mapenzi ya kawaida au ngono/kufanya mapenzi yenye michezo ya kubahatisha?

Je, watu wanapendelea ngono/kufanya mapenzi ya kawaida au ngono/kufanya mapenzi yenye michezo ya kubahatisha?

Je, unajua kwamba wengi wetu tunapenda kufanya mapenzi ya kawaida? Na pia unajua kwamba kuna wale... Read More