Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Njia za Kuzuia Mimba

Featured Image
Njia za uzazi wa mpango zinatofautiana sana na zinaweza kugawanywa katika makundi mengi:

Vizuizi


(hizi huzuia mbegu kulifikia yai): Kuna mpira wa kiume (kondomu ya kiume), yaani mfuko wa mpira uliozibwa upande moja. Unavishwa kwenye uume uliosimama kabla ya kuingia ukeni. Pia kuna mpira wa kike (kondomu ya kike), yaani mpira unaoingizwa ukeni kabla ya kujamiiana.

Vidonge vya kuzuia mimba:


Lazima mwanamke anywe vidonge hivi kila siku hata kama hajamiiani.

Njia nyingine za kuzuia mimba kwa muda mrefu


. Njia hizi hazihitaji maandalizi maalum, ili kuzuia mimba, kabla ya kujamiiana na pia mwanamke hahitaji kukumbuka kufanya chochote kila siku. Kati ya njia hizi ni pamoja na sindano anazopewa mwanamke kila baada ya miezi mitatu. Pili, kuna vipandikizi, yaani vijiti vyembamba vya plastiki vinavyowekwa kwenye sehemu ya juu ya mkono wa mama kwa njia ya upasuaji mdogo. Vijiti vina kichocheo kinachozuia kupevuka kwa yai. Pia, kuna kitanzi ambacho ni kitu kidogo kilichotengenezwa kwa aina maalum ya plastiki. Kwa ufupi kinaitwa IUD. Huwekwa kwa utaalamu ndani ya mfuko wa uzazi. Sindano, vipandikizi na vitanzi lazima viwekwe na mtaalamu mwenye ujuzi kwenye kituo cha afya chenye vifaa vya kutosha. Kwa vile dawa za kuzuia mimba kwa muda mrefu zinaingiliana na mzunguko wa kawaida wa hedhi kwa kiasi, athari zake ni kubwa kuliko kutumia vidonge.

Kwa mwanaume na mwanamke kuna njia ya kudumu ya kufunga kizazi kwa njia ya upasuaji


. Kwa mwanaume mirija inayopitisha mbegu hukatwa na kufungwa, ili kuzuia mbegu zisitoke. Akijamiiana, anaweza kumwaga shahawa, lakini ndani ya shahawa hakuna mbegu. Kama mwanaume amefunga kizazi uume utadinda kama kawaida na kufikia mshindo atamwaga maji ya shahawa ambayo hayatakuwa na mbegu. Kwa mwanamke mirija ya kupitisha mayai hukatwa na kufungwa, ili kuzuia mayai kufika kwenye mfuko wa uzazi. Baada ya upasuaji huu, mama ataendelea na hedhi kama mwanzo, lakini yai halitaweza kukutana na mbegu za kiume tena.

Vilevile kuna njia nyingine mbalimbali ambazo hazina uhusiano na matumizi ya dawa au vizuizi vya mimba. Njia hizi hazina uhakika mkubwa wa kutopata mimba. Mara nyingine mama anatumia ishara mbalimbali, au tarehe kujua lini anaweza kupata mimba, ili kuepuka kujamiiana katika kipindi hicho. Kumwaga mbegu za kiume nje ya uke, au kutegemea kwamba mimba hazishiki wakati wa kunyonyesha ni njia nyingine za asili zinazotumiwa. Kumbuka kwamba njia hizi hutumika sana, lakini si njia salama sana za kuzuia mimba wala kuambukizwa na magonjwa ya zinaa.
Ni muhimu kukumbuka kwamba njia ya uzazi wa mpango inaweza kufaa kwa mtu huyu na isifae kwa mtu mwingine. Kwa hiyo, ni vizuri kila mtu aliyeamua kupanga uzazi apate ushauri kwenye kliniki kuhusu njia inayomfaa zaidi
AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya Kuonyesha Ukarimu kwa Msichana Wako

Jinsi ya Kuonyesha Ukarimu kwa Msichana Wako

Habari za leo! Leo nataka kuzungumza juu ya jinsi ya kuonyesha ukarimu kwa msichana wako. Kama mw... Read More

Je, watu wanaoishi na ualbino wanafanana wote?

Je, watu wanaoishi na ualbino wanafanana wote?

Hapana. Albino wote hawafanani, wanatofautiana kufuatana na
kiasi cha melanini walicho nacho... Read More

Uhusiano wa ubakaji na uvaaji wa nguo fupi?

Uhusiano wa ubakaji na uvaaji wa nguo fupi?

Ubakaji kamwe siyo kosa linalomhusu yeye aliyebakwa; ni kosa
linalomuhusu yeye aliyebaka. Un... Read More

Kwa nini ni Lazima Kufanya Ngono na Mtu Mmoja Tu?

Kwa nini ni Lazima Kufanya Ngono na Mtu Mmoja Tu?

Kwa nini ni Lazima Kufanya Ngono na Mtu Mmoja Tu? 🌸

Asante kwa kujiunga nami katika mak... Read More

Magonjwa ya zinaa na dalili zake

Magonjwa ya zinaa na dalili zake

Kuna magonjwa mengi tofauti ya zinaa, lakini yale ambayo yameenea sana ni kisonono, kaswende, klamdi... Read More
Vidokezo vya Kuwa na Tarehe ya Kufurahisha na Msichana

Vidokezo vya Kuwa na Tarehe ya Kufurahisha na Msichana

Hakuna kitu kizuri kama kuwa na tarehe ya kufurahisha na msichana wako. Iwe ni siku ya kuzaliwa, ... Read More

Kufahamu tabia ya rafiki yako wa kike/kiume kabla ya kuoana hata kama anaishi mbali

Kufahamu tabia ya rafiki yako wa kike/kiume kabla ya kuoana hata kama anaishi mbali

Unaweza kufanya uchunguzi wa kutosha kuhusu tabia, muono na imani ya rafiki yako hata kama mnaish... Read More

Kama wameoana mume na mke na ikatokea hawapati mtoto, je, utajuaje kuwa tatizo liko kwa mwanamke au mwanaume?

Kama wameoana mume na mke na ikatokea hawapati mtoto, je, utajuaje kuwa tatizo liko kwa mwanamke au mwanaume?

Kwa wastani i i inachukua kama muda wa mwaka mmoja kwa mwanamke kuanza kupata ujauzito, wakikutan... Read More

Vidokezo vya Kuwa na Mazungumzo ya Kina na Msichana

Vidokezo vya Kuwa na Mazungumzo ya Kina na Msichana

Kama kijana, kuna wakati unaweza kukutana na msichana na unataka kuzungumza naye kwa kina lakini ... Read More

Jinsi ya Kuzungumza na Mwenzi Wangu kuhusu Kujikinga na Mimba

Jinsi ya Kuzungumza na Mwenzi Wangu kuhusu Kujikinga na Mimba

Jinsi ya Kuzungumza na Mwenzi Wako kuhusu Kujikinga na Mimba

Karibu sana marafiki zangu! L... Read More

Kwa nini Ni Lazima Kufanya Ngono na Mtu Mmoja Tu?

Kwa nini Ni Lazima Kufanya Ngono na Mtu Mmoja Tu?

Kwa nini Ni Lazima Kufanya Ngono na Mtu Mmoja Tu? 😊

Habari za leo vijana wangu! Leo tut... Read More

Nifanyeje Kukabiliana na Hisia za Aibu Kuhusu Ngono?

Nifanyeje Kukabiliana na Hisia za Aibu Kuhusu Ngono?

Jinsi ya Kukabiliana na Hisia za Aibu Kuhusu Ngono 🌟

Karibu vijana wenzangu! Leo, tutaj... Read More