Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Madhara ya pombe kwa mwili na akili

Featured Image

Pombe huingia kwenye damu na kuzunguka mwili mzima pamoja
na kwenye ubongo wako. Ina madhara kwa viungo vya mwili
wako na ubongo wako na hivyo huathiri tabia na hisia zako.

Unywaji wa pombe kupita kiasi unaweza kuathiri viungo vingi
kwa mfano, ini ambalo ndilo huathirika zaidi. Ini hilo linafanya
kazi ya kufyonza kilevi katika mwili wako. Kama ukinywa zaidi
utaathiri ini kiasi kwamba halitaweza kufanya kazi kikamilifu au
litashindwa kabisa hatimaye utakufa. Kilevi kingi husababisha
kansa ya ini na tumbo.

Hatari kubwa siku hizi ni kupata na kusambaza virusi vya
UKIMWI. Mlevi mara nyingi huwa mzembe na husahau kinga
muhimu kama vile kutumia kondomu wakati wa kufanya mapenzi.
Anaweza pia kufanya mapenzi na watu ambao hafahamu afya
zao, kama ni wagonjwa au la. Zaidi ya hayo mlevi mara nyingi
huwa dhaifu, hivyo ni rahisi kushambuliwa na magonjwa
mbalimbali pamoja na VVU.

Pombe inaathiri pia uwezo wa kufanya tendo la ndoa. Huwa ni
vigumu kwa uume kusimama. Pia huathiri ubongo hasa sehemu
zile zinazomiliki ufahamu na mihemko.

Kwanza unaweza kujisikia mchangamfu na huru, lakini mara
tu unaanza kujisikia taabu na kushindwa kutembea vizuri.
Utakuwa na matatizo ya kutoona vizuri na matatizo ya kutoa
uamuzi sahihi. Watu huanza kuwa na vijitabia vya ajabu na
vipya baada ya kulewa. Kugombana na watu wengine na kufanya
mambo yasiyokubalika kama vile kujikojolea mbele za watu.
Kama utaendelea kunywa kuna uwezekano mkubwa wa kupata
madhara. Kila dhara huharibu mamilioni ya seli za ubongo wa
binadamu.

Kwanza hutakuwa na kumbukumbu ya nini kimetokea, lakini
unaweza pia kupoteza kabisa kumbukumbu zako. Kama ukinywa
pombe kupita kiasi kwa muda mrefu unaweza kupungukiwa
akili na mwisho kuharibu kabisa akili. Pombe pia ni dawa ya
kulevya kwani huweza kukutawala. Watu waliotawaliwa na
pombe, hutumia pesa nyingi na muda mwingi kwenye pombe,
hali ambayo inaweza kuwa ni mzigo mzito kwa familia na jamii,
na pindi mtu anapotawaliwa, ni vigumu kunywa kidogo au kuacha
kabisa. Kama mtu atajaribu kuacha, hupata matatizo kama
kutetemeka, mapigo ya moyo kuongezeka, kutokwa na jasho
jingi, na kukosa usingizi wakati wa usiku. Hali hiyo husababisha
maumivu na ni hatari kwa watu ambao wametawaliwa na pombe.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Je, ni kweli kuwa madhara ya uvutaji moshi wa sigara yako ni kidogo kuliko yale yatokananyo na kuvuta moshi kutoka kwa mvutaji?

Je, ni kweli kuwa madhara ya uvutaji moshi wa sigara yako ni kidogo kuliko yale yatokananyo na kuvuta moshi kutoka kwa mvutaji?

Uvutaji wa aina zote una madhara. Kama utavuta sigara na
kuvuta moshi kwa kutumia mdomo hadi... Read More

Je, mvulana afanye nini ili kuzuia ndoto nyevu?

Je, mvulana afanye nini ili kuzuia ndoto nyevu?

Ndoto nyevu ni kitu kinachowatokea vijana wakiwa usingizini. Haiwezekani kuzuiwa kwa sababu uko usin... Read More
Je, watu wanapendelea kujaribu kufanya mapenzi?

Je, watu wanapendelea kujaribu kufanya mapenzi?

Habari za leo wapendwa wasomaji! Leo, tunajadili kuhusu je, watu wanapendelea kujaribu kufanya ma... Read More

Jinsi ya Kujikinga na Maambukizi ya VVU na UKIMWI

Jinsi ya Kujikinga na Maambukizi ya VVU na UKIMWI

Jinsi ya Kujikinga na Maambukizi ya VVU na UKIMWI

Karibu vijana wapendwa! Leo, nataka kuzu... Read More

Njia za Kujenga Uvumilivu na Msichana katika Changamoto za Maisha

Njia za Kujenga Uvumilivu na Msichana katika Changamoto za Maisha

Njia za Kujenga Uvumilivu na Msichana katika Changamoto za Maisha

Hakuna ubishi kwamba mai... Read More

Nifanyeje Kukabiliana na Hisia za Kukosa Ujasiri wa Kujihusisha na Ngono?

Nifanyeje Kukabiliana na Hisia za Kukosa Ujasiri wa Kujihusisha na Ngono?

Nifanyeje Kukabiliana na Hisia za Kukosa Ujasiri wa Kujihusisha na Ngono? 🌈

Karibu kija... Read More

Jinsi ya Kuwa na Mawasiliano Mzuri na Msichana

Jinsi ya Kuwa na Mawasiliano Mzuri na Msichana

Leo tutazungumzia jinsi ya kuwa na mawasiliano mzuri na msichana. Kwa sababu ya tofauti za kijins... Read More

Ninaweza kupata mimba wakati nipo kwenye hedhi?

Ninaweza kupata mimba wakati nipo kwenye hedhi?

Ili mwanamke aweze kushika mimba, i inabidi yai lililopevuka likutane na mbegu za kiume. Yai pevu... Read More

Nifanyeje Kuzungumza na Mwenzi Wangu kuhusu Matumizi ya Vidonge vya Kuzuia Mimba?

Nifanyeje Kuzungumza na Mwenzi Wangu kuhusu Matumizi ya Vidonge vya Kuzuia Mimba?

Nifanyeje Kuzungumza na Mwenzi Wangu kuhusu Matumizi ya Vidonge vya Kuzuia Mimba? 🌸🌍

Read More
Kwa nini pombe za kienyeji ni hatari kuliko pombe za viwandani?

Kwa nini pombe za kienyeji ni hatari kuliko pombe za viwandani?

Pombe zinazotengenezwa kiwandani zinafuata viwango
ambavyo ubora wake umethibitishwa kihalal... Read More

Kwa nini vijana wengine Albino wanaanza kujamiiana katika umri mdogo?

Kwa nini vijana wengine Albino wanaanza kujamiiana katika umri mdogo?

Kuna sababu nyingi ambazo zinamfanya kijana kuanza kujamiiana
katika umri mdogo. Baadhi ya s... Read More

Kwa nini Ni Lazima Kufanya Ngono na Mtu Mmoja Tu?

Kwa nini Ni Lazima Kufanya Ngono na Mtu Mmoja Tu?

Kwa nini Ni Lazima Kufanya Ngono na Mtu Mmoja Tu? 😊

Habari za leo vijana wangu! Leo tut... Read More