Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMS💌💕
AckyShine

Mapishi ya Biriyani Ya Kuku

Featured Image

Vipimo

Mrowanishe kuku na viungo hivi kwa muda mdogo tu

Kuku (Mkate kate Vipande) - 4 LB

Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi - 2 Vijiko vya supu

Chumvi - kiasi

Pilipili nyekundu ya unga - 1 Kijiko cha supu

Bizari ya manjano (Haldi au Tumeric) - 1 Kijiko cha chai

Bizari ya pilau ya powder (Jeera) - 1 Kijiko cha chai

Gilgilani powder (Dania) - 1 Kijiko cha chai

Ndimu - 1 Kijiko cha supu

Mchele na vitu vya Masala:

Mchele (Basmati mzuri) (rowanisha) - 7 cups

Mafuta ya kupikia - kiasi

Vitunguu Vilivyokatwa - 8

Nyanya iliyokatwa katwa - 3

Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi - 1 Kijiko cha supu

Garam Masala -1 Kijiko cha supu

Hiliki powder - ½ Kijiko cha chai

Tomatoe paste - 1 Kijiko cha supu

Pilipili mbichi zipasue katikati - 4

Chumvi - kiasi

Mtindi - 4 Vijiko vya supu

Kotmiri iliokatwa (Chopped) - ½ Kikombe

Mafuta ya kunyunyuzia katika wali - 3 Vijiko vya supu

Zaafarani au rangi ya biriani - kiasi

Namna Ya Kutaarisha Na Kupika

Weka kuku aliyerowanishwa na viungo vyake katika Foil tray au chombo chocote utakachomwagia wali humo humo na kupikia biriani, kisha mchome (Bake) mpaka awive na awe mkavu kiasi.

Wakati kuku anapikika, kaanga vitunguu katika karai au sufuria mpaka viwe brown na epua nusu yake weka kando.

Punguza mafuta yabakie kiasi tu, ongeza Thomu na tangawizi, na viungo vyote vya hapo juu isipokuwa Mtindi na kotmiri, endelea kukaanga hadi tomatoe zilainike.

Ongeza chumvi, malizia mwisho kwa kutia mtindi, kotmiri na vile vitunguu ulivyoweka kando. Masala yako tayari.

Mwagia masala juu ya kuku uliyekwishmpika changanya vizuri.

Chemsha Mchele uwive nusu, chuja na mwagia juu ya masala.

Nyunyiza mafuta kidogo juu ya mchele na zaafarani au rangi ya biriani.

Bake katika moto wa 350 – 400 kwa muda wa 15 – 20 minutes. Biriyani imekuwa tayari kuliwa.

Mtindi wa kutolea Biriyani:

Mtindi - 1 kikombe

Pilipili mbichi - 1 ndogo

Kitunguu saumu(/galic) thomu - chembe mbili

Nanaa - kiasi

Chumvi - chembe tu

Weka kwenye Blender na uchanganye, kisha mimina katika bakuli

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Mapishi ya Biskuti Za Mtindi/Yoghurt

Mapishi ya Biskuti Za Mtindi/Yoghurt

MAHITAJI

Chenga za biskuti - 3 gilasi

Mtindi (yogurt) - 1 Kopo (750g)

Maziwa ... Read More

Mapishi ya Biriani Ya Tuna

Mapishi ya Biriani Ya Tuna

MAHITAJI

Mchele Basmati - Mugs 2 ½

Vitunguu (Vikubwa kiasi) - 3

Tuna - Vibat... Read More

Jinsi ya kupika Biskuti Za Kopa Za Kunyunyuziwa Sukari Za Rangi

Jinsi ya kupika Biskuti Za Kopa Za Kunyunyuziwa Sukari Za Rangi

MAHITAJI

Unga vikombe 2 ¼

Siagi 250g

Sukari kukaribia kikombe ½ (au takriba... Read More

Jinsi ya kupika Wali Wa Sosi Ya Tuna

Jinsi ya kupika Wali Wa Sosi Ya Tuna

Viambaupishi

Sosi Ya tuna

Tuna (samaki/jodari) 2 Vikopo

Vitunguu (kata kata) ... Read More

Jinsi ya kuandaa Vileja Vya Tambi

Jinsi ya kuandaa Vileja Vya Tambi

MAHITAJI

Tambi (vermiceli Roasted) Mifuko 2

Siagi - 4 Vijiko vya supu

Maziwa ... Read More

Mapishi ya Wali Wa Kukaanga Kwa Kidari Cha Kuku (Chicken Breast) Wa Kukausha

Mapishi ya Wali Wa Kukaanga Kwa Kidari Cha Kuku (Chicken Breast) Wa Kukausha

Viambaupishi

Vipimo vya Wali:

Mchele 3 vikombe

*Maji ya kupikia 5 vikombe

... Read More
Jinsi ya kutengeneza juisi ya nyanya

Jinsi ya kutengeneza juisi ya nyanya

Viamba upishi

Nyanya 1 kg
Maji Iita ½
Chumvi kijiko kidogo 1
Sukari

<... Read More
Mapishi ya Wali Wa Nyanya Wa Kukaanga

Mapishi ya Wali Wa Nyanya Wa Kukaanga

Vipimo

Mchele basmati, pishori - 3 vikombe

Vitunguu katakata - 2

Nyanya/tungu... Read More

Mapishi ya Kidheri - Makande

Mapishi ya Kidheri - Makande

Mahitaji

Nyama (kata vipande vidogodogo) - ½ kilo

Maharage - 3 vikombe

Mahin... Read More

Mapishi ya Pilau ya nyama ya ng'ombe na kachumbari

Mapishi ya Pilau ya nyama ya ng'ombe na kachumbari

Mahitaji

Mchele (rice vikombe 3)
Nyama ya ng'ombe (beef 1/2 kilo)
Viazi mbatata... Read More

Jinsi ya kupika Donati

Jinsi ya kupika Donati

Viamba upishi

Unga
2 Magi (kikombe kibuwa cha chai)

Sukari
1/3 Kikombe ch... Read More

Mapishi ya Wali Wa Mboga Na Samaki Wa Pink Salmon

Mapishi ya Wali Wa Mboga Na Samaki Wa Pink Salmon

Vipimo

Mchele 3 vikombe

Mboga mchanganyiko 1 kikombe

Samaki wa Pink Salmon 5 ... Read More