Ujumbe wa kumwambia mpenzi wako kuwa huna linalokuhuzunisha maishani kwa kuwa mnapendana
Updated at: 2024-05-25 15:22:49 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Imani hufanya mambo yote yawezekane, Matumaini hufufua yaliyopoteza uhai, lakini mapenzi hufanya mambo yote yaonekane mazuri. Sina linalonihuzunisha maishani mwangu kwa kuwa tunapendana!
Updated at: 2024-05-25 15:36:04 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mungu akupe umri wa mnazi uishi mingi miaka. Akupe thamani ya mnazi kila kitu chatumika. Kuanzia kuti lake mpaka kwenye kidaka. Kitale katikati yake ukila utaridhika. Matamu na maji yake hukata kiu haraka. Weupe watui lake lina ladha ukipika. Kupaka mafuta yake mwili hulainika. Na kwenye machicha yake kazi nying hufanyika. Hata na upepo wake uvumapo utacheka. Sikijui kitu chake kipi kisichotumika.usiku mwema
Ujumbe wa kumsifia mpenzi wako kumwambia kuwa hakuna anayemfikia yeye
Updated at: 2024-05-25 15:26:31 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Baadhi ya watu huzaliwa na vipaji. Huweza kufanya mambo mazuri kwa ujuzi wao, lakini hamna anayekufikia wewe, kwani ukinisogelea tu kila kitu huwa kizuri.
Ujumbe mzuri wa kumwambia mpenzi wako kuwa yeye tuu mdiye kakutawala
Updated at: 2024-05-25 15:36:48 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Fikra hutawala mtima wangu, Kwa madhila yalojaa duniani, Kwa muhali wa yanayojiri, Kwa machweo na mawio, Kwa totoro ama nuruni, Nao moyo hukosa ukamilifu, Kwa utashi wa zake hisia, Zinipazo sababu kuu, Ya upendo juu yako, Ya kukufanya daima uwe, Mawazoni mwangu.
Mawazoni ama ndotoni, Daima wewe hutawala, Kila asubuhi niamkapo, Nao usiku nilalapo, U chakula changu akilini, Nalo tulizo langu moyoni, Daima huuwaza upekee, Wewe uliojaaliwa, Na hivyo naihisi furaha, Daima wewe uwapo, Mawazoni mwangu.
SMS yakumtumia mtu unayempenda lakini hamko kwenye mahusiano
Updated at: 2024-05-25 15:26:59 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
macho huona na moyo hurdhia,ila co kila kitu jicho lionalo moyo hurdhia.lakn pind moyo urdhiapo upendo moyon huingia.moyo huwa kpofu japo wng wa hisia.upendo ndan ya moyo haupimwi kwa mizani kwa unayemzimikia. moyo wangu umepata hisia Kwa flan licha bdo cjamjua.
Ama baada ya salamu, mimi ni mzima wa afya njema. Mie ni ndege nipo angani na nimetafuta mti wa kutua kila pembe ya dunia lakini sijaupata bado. Je naweza nikatua kwako?
Updated at: 2024-05-25 15:37:25 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Ama baada ya salamu, mimi ni mzima wa afya njema. Mie ni ndege nipo angani na nimetafuta mti wa kutua kila pembe ya dunia lakini sijaupata bado. Je naweza nikatua kwako?
SMS kali ya kimahaba ya kumtumia mpenzi wako kumwambia alivyokuteka moyo na akili zako
Updated at: 2024-05-25 15:25:53 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mpenzi wangu kukutana nawe ilikuwa ni bahati, kukuchagua kuwa rafiki yangu ilikuwa ni maamuzi yangu, lakini kuanguka kwenye penzi lako haikuwa hiyari yangu. Umeniteka moyo na akili yangu pia.