Raha ya ndege kichaka si tunduni asilani, Raha ya Ndege ujumbe nakupa mpelekee mwandani iwapo hukumkuta msubiri mlangoni, Usije ukaondoka hakuchinji asilani, Mwambie namkumbuka hatoki mwangu moyoni. ucku mwema
Updated at: 2024-05-25 15:37:50 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Raha ya ndege kichaka si tunduni asilani,
Raha ya Ndege ujumbe nakupa mpelekee
mwandani iwapo hukumkuta msubiri mlangoni,
Usije ukaondoka hakuchinji asilani,
Mwambie namkumbuka hatoki mwangu moyoni.
ucku mwema
Updated at: 2024-05-25 15:36:33 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Pokea sms yangu iliyojaa utamu, nimeipamba kwa maneno laini yenye ladha adimu, utamu wake ni kama apple haufanani na ndimu, nimeituma kwako sms hii ikuletee salamu "UHALI GANI MPENZI?"
Updated at: 2024-05-25 15:26:08 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
pongezi kwako mpenzi kuwa wangu mtetezi kwenye jahazi la mapenzi,ufundi na ujuzi unao hasa tuwapo wawili chumbani.penzi lako halichakai daima huzaliwa upya.
Ujumbe wa kimahaba wa kumtumia mpenzi wako aliyeko mbali na wewe kumwambia unavyommisi
Mawingu yametanda napanda kwenye kitanda, macho nayaangaza, taratibu navuta shuka na kujitanda, mishumaa pembezoni inaniangaza, mziki laini wanibembeleza
Updated at: 2024-05-25 15:37:23 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mawingu yametanda napanda kwenye kitanda, macho nayaangaza, taratibu navuta shuka na kujitanda, mishumaa pembezoni inaniangaza, mziki laini wanibembeleza kitu pekee nilichokikosa ni joto lako na vijimambo vyako kunako kitanda!
Ujumbe mzuri wa SMS wa kumfariji mpenzi wako maisha yake yanapokuwa magumu
Updated at: 2024-05-25 15:37:03 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Furaha yangu kubwa ni kuliona tabasamu lako, kujua uko na furaha, na kuhisi upendo wako. Najua kuwa maisha mara nyingine huwa ni makatili, na hiyo ni sababu niko hapa kukuonyesha kuwa maisha yanaweza kuwa mazuri kama kuna mtu anayekujali.
SMS ya kuasa na kutakia kila la heri katika mapenzi
Updated at: 2024-05-25 15:26:57 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mapenzi ni kitu kisichotabirika, ndio maana kila mwenye KUPENDA au KUPENDWA hana uhakika na PENZI lake kwa yule AMPENDAE, Muda wote huhisi anasalitiwa. PENZI Ni kama JENGO lililokosa NGUZO muda wowote unahisi litadondoka… Usinielewe vibaya sikukatazi KUPENDA au KUPENDWA, ila tazama wapi UMEPENDA au UMEPENDWA.kilalakher kwa umpendae
Updated at: 2024-05-25 15:36:04 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mungu akupe umri wa mnazi uishi mingi miaka. Akupe thamani ya mnazi kila kitu chatumika. Kuanzia kuti lake mpaka kwenye kidaka. Kitale katikati yake ukila utaridhika. Matamu na maji yake hukata kiu haraka. Weupe watui lake lina ladha ukipika. Kupaka mafuta yake mwili hulainika. Na kwenye machicha yake kazi nying hufanyika. Hata na upepo wake uvumapo utacheka. Sikijui kitu chake kipi kisichotumika.usiku mwema