Updated at: 2023-04-29 22:52:23 (2 years ago by Melkisedeck Leon Shine)
1.Mwenye mpira Lazima acheze ata kama hajui mpira 2.Dogo mnene Lazima awe golikipa 3.Mwenye mpira ataamua nan acheze na nan asicheze
4.kama haujashiriki kufuma mpira unaweza ucpate namba 5.Ukichaguliwa mwishon ujue uwezo wako ni mdogo kuliko wote 6.Mwenye mpira akikaclika mpira umeisha 7.Inaruhusiwa kubadili golikipa kama ikitokea penat na baada ya apo ataendelea kudaka yule yule 8.Mechi itaisha pale giza linapoingia 9.wale ambao wamekosa namba kazi yao ni kufata mpira ukitoka 10.yule mtaalam wa soka {KM MIMI } huwa hakoc namba ata cku moja! Ukiikumbuka lazima utabasam!
Angalia kilichojiri katika semina ya wanandoa kuhusu upendo
Updated at: 2024-05-25 18:00:09 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kulikuwa na semina ya wanawake kuhusu namna ya kuishi kwa upendo katika ndoa. Mwalimu aliwauliza ni wangapi wanawapenda waume zao? Wote wakanyoosha mikono kama ishara ya kuwa wanawapenda waume zao. Mwalimu akauliza tena, “Ni lini mara ya mwisho umemwambia mumeo “Nakupenda Mpenzi”?
Majibu yalikuwa kama ifuatavyo: Wengine wakisema Asubuhi ya leo, Wengine jana, Wengine wiki iliyopita Wengine mwezi uliopita Na wengine wakasema hawakumbuki! Mwalimu aliwapa kazi kila mwanasemina achukue simu yake na kumtumia mume wake meseji yenye neno “NAKUPENDA MPENZI” Baada ya meseji kwenda aliwaamuru kubadilishana simu kila mtu na jirani yake. Kila mwanasemina aliambiwa kusoma meseji za majibu kwenye simu aliyoshika
Simu ya 1 – “Samahani, nani mwenzangu”! Simu ya 2 – “Samahani, wrong number”! Simu ya 3 – “Si nimekuambia usinitumie messages kwenye namba hii”! Simu ya 4 – “Mh! leo mvua itanyesha”! Simu ya 5 – “Nikija tutaongea zaidi”! Simu ya 6 – “……Imedhibitishwa umepokea Tsh300,000 kutoka kwa ……”! Simu ya 7 – “Me too”! Simu ya 6 – “Huu ujumbe ndio ulikuwa unamtumia huyo hawara yako ee, leo utanikoma”!
Updated at: 2024-05-25 16:57:53 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Ukimchoka mkeo, waweza kumtaftia sababu za kumuacha kama hizi
_ 1. Missed calls 16? Umeua betri la simu yangu. Kwa hiyo hata mimi unaweza kuniua… It's Over!!! _ 2. Hata hunieshimu. Mi naongea na wewe lakini we upo bize unavuta pumzi? It's over! _ 3. Nimekupigia umepokea simu hapohapo. Huna subira. It’s over!! _
4. Nilikwambia huwa napenda chakula cha moto lakini hujanipashia ice cream. Hunijali. It's over! _ 5. Nimekupa mayai mawili, moja uchemshe jingine ukaange. We umekaanga ambalo ulitakiwa kuchemsha na umechemsha ulilotakiwa kukaanga. Huniheshimu, It’s over! _ 6. Nimekuita DARLING na wewe ukaniita HONEY. Yani kwa maana nyingine unamuita mama yangu NYUKI. Huheshimu wazazi wangu, fungasha kilicho chako. its over.
Hapo sasa patamu, cheki jamaa alivyowezwa na huyu dogo
Mfugaji mmoja alikwenda kwa mfugaji mwenzake (ambae pia ni bwana mifugo wa eneo lao) asubuhi moja. Alipobisha hodi mtoto wa kiume wa umri upatao miaka 12 akamfungulia mlango. Mazungumzo yafuatayo yakafuatia:
Mkulima: Baba yako yupo?
Mtoto: Hapana Mzee, amekwenda mjini.
Updated at: 2024-05-25 18:13:40 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mfugaji mmoja alikwenda kwa mfugaji mwenzake (ambae pia ni bwana mifugo wa eneo lao) asubuhi moja. Alipobisha hodi mtoto wa kiume wa umri upatao miaka 12 akamfungulia mlango. Mazungumzo yafuatayo yakafuatia:
Mkulima: Baba yako yupo?
Mtoto: Hapana Mzee, amekwenda mjini.
Mkulima: Mama yako?
Mtoto: Nae kaenda mjini na baba.
Mkulima: Kaka yako Howard yupo?
Mtoto: Nae hayupo, wote yeye, baba na mama wamekwenda mjini. Kwani una shida gani? Kama kuna kitu unahitaji niambie maana nimeachiwa funguo na najua vifaa vinapowekwa. Mzee akawaza kidogo halafu akasema: Kwa kweli nilitaka kuongea na baba, mama au kaka yako kwa kuwa kaka yako amempa mimba binti yangu.
Mtoto akafikiria kidogo halafu akasema: Kusema ukweli itabidi umsubirie baba, ila kwa kukusaidia ni kuwa baba hulipisha shilingi laki moja kwa kupandisha dume la ng'ombe na elfu hamsini kwa beberu. Ila sijui baba hutoza shilingi ngapi kwa Howard akifanikiwa kutia mimba.
Updated at: 2024-05-25 18:09:37 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mchaga baada ya kufa akaulizwa na malaika anayetoa roho: Mangi hapa ni njiapanda kulia ni Mbinguni na kushoto ni Jehanamu, Je unachagua kwenda wapi?
MANGI: Bwashee, mi nabaki hapa hapa njiapanda aisee. MALAIKA: Kwa nini? MANGI: Aisee, nikifungua duka hapa si nitapata wateja wa Mbinguni na Jehanam. Yani patakuwa senta ya hatari, supu na nyama choma muda wote. Hata we utafaidi, unavyoenda kuchukua roho unaniletea stock nakupa hela yako cash mkononi. Na kila ukipita hapa unapiga mchemsho wako wa ulimi na bia mbili chap kabla ya kuingia mbinguni. Kwanza nashangaa Shirima alipitaje hapa bila kushika ploti, au alikufa amelewa sana?
Updated at: 2023-04-29 22:52:35 (2 years ago by Melkisedeck Leon Shine)
Baba- : Halloo mke wangu.. yaani ni shida sitaweza kurudi nyumban, daraja limevunjika na kutoka morogoro kurudi dar haiwezekani MAMA:- Mme wangu morogoro ulienda bila kuniaga! ? BABA:- Ilikuwa ni ghafla sana mke wangu sikuweza kukwambia MAMA:- kha! Sasa watoto nani atawaangalia BABA:- Unasemaje! We uko wapi kwan MAMA:- Niko bagamoyo na daraja limeondolewa na maji sitaweza kurudi. BABA:- Unasemaje we mwanamke.. nakwambia nikukute nyumban ndani ya dk 15 Baada ya dk 15 Baba kafika nyumban. MAMA:- Haya umefkaje kutoka morogoro? BABA:- Nimepewa lift na helkopta ya Mbowe..
Updated at: 2024-05-25 18:09:43 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
FUNDISHO : SAFARI NI SAFARI
Maisha ni ya ajabu sana, wakati mwingine maisha ni mazuri na mwingine ni mabaya, katika maisha yetu tumeshapitia safari nyingi sana na za aina mbalimbali kwa nyakati mbalimbali. Lakin kiukweli kila safari ni safari tuu.
Japokua kila safari ina changamoto zake lakini mwisho wake ni ule ule , kila safari ina uzuri na upekee wake.
Vile vile kila safari ina ubaya wake, kwa mfano kila safari ina gharama yake kulingana na upekee wake.
Usiwe na wasiwasi na mashaka na aina ya safari ulionayo, jipe moyo utaimaliza na kupata ulichokitarajia. Haya ndio maisha na wote tunatakiwa tuyafurahie.
Ingawa kila mtu ana safari yake bado wote tunatakiwa tufurahie pamoja kwa safari tuliyo nayo. Hata Uwe Na safar ya aina gani wewe furahi tuu. Hii ni kwa sababu safari mwisho wake ni mmoja kwa wote burudani ni ile ile
Safari🍺 ni safari 🍺hata kama ni ya chupa au ya kopo mwisho wake 💤💤