Updated at: 2024-05-25 17:52:24 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
MUME: "Unajua mi unanishangaza sana, kila siku nakusikia mara useme TV yangu, gari yangu, chumbani kwangu, mara hoo watoto wangu. Sisi ni mke na mume, kila kitu ni chetu. Jirekebishe bwana".👴😎😎😒 MKE: Yuko kimya anaendelea na shughuli zake za kupekua kabatini kama hasikii, na hakumjibu kitu mumewe.👵😷 MUME: Akamuuliza kwa hamaki,"Sasa hapo unatafuta nini?".👴😡 MKE: "Sidiria yetu!!"👙💏 MUME: (kamfungia kabatini alafu kamwambia. "nipo chumbani , ")👴😷😷 💃💃💃💃💃💃 😂😂😂😂😂😂
Updated at: 2024-05-25 17:50:48 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
CHEKA KIDOGO Majambaz waliliteka gar moja lililokua limeshehen abiria Baada ya abiria kusachiwa na majambaz hao na kukutwa hawana pesa, majambaz wakasema kila m2 atapigwa viboko (bakora) kutokana na namba ya shati alilovaa Aliyekua hana namba atasalimika Kaz ikaanza, jamaa alievaa jez ya ROONEY wa Man U akapigwa fimbo 10, mwengine alievaa nguo ya 50cent akapigwa 50, n.k, sasa kwa pemben kulikua na jamaa analia sn yaani kila akijiangalia, kumbe alikua amevaa fulana limeandikwa LOWASA 2015 duuuh! Unajua kilichotokea ngoja niweke cm chaji kwanza.
Updated at: 2024-05-25 17:04:12 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
😎 Jamaa kamuaga mkewe anaenda semina Songea kwa wiki nzima kumbe kahamia kwa demu nyumba ya pili toka kwake. Siku ya 1 kalala asubuhi alipoamka kachungulia kwake kukoje,
Si kamuona jamaa yuko nje ya nyumba yake kavaa taulo lake anapiga mswaki. Akapiga kelele, 'We nani?', Jamaa akajibu, 'Mshikaji mambo ya mjini, mume wa huyu demu kasafiri kaenda Songea mi ndo najivinjari hapa'. Mume kajibu kwa uchungu, Shenzi mkubwa, ngoja nirudi toka Songea nakuua.😆😆😆😆😆😆😆😆😆😆😆
Updated at: 2024-05-25 17:03:30 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Bosi wangu karudi safari yake kutoka serengeti..! Si akanitumia picha, lakini ilikuwa network yenyewe tabu.. kwahio picha haikufunguka na kwa vile niliona itachelewa kufunguka na ataona sikumjibu basi nami..
Nikampelekea msg nikamuandikia umependeza saana bosi mashaallah…!! sasa baada tu ya kumfika msg.. na huku picha ikafunguka kumbe picha ya Sokwe..!! Basi Kaniambia kesho niende ofsini kwake kuna barua yangu.. Nahisi hyo barua ina pesa, hapa cjalala, nmekosa usingizi kabisa,nawaza ninunulie nn hyo pesa.Na kesho asubuhi sa 12 asubuhi atanikuta ofisini kwake naisubiri barua, sipendagi ujinga mimi.
Updated at: 2024-05-25 16:53:11 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
1, mwanaume kuoga haraka haraka ili uwahi kuangalia igizo, huo ni UMAMA..😂
2, mwanaume kupiga picha umeng'ata Lips na Unapiga na Camera Beauty Plus huo ni UMAMA..😂
3, Mwanaume kuangalia tamthilia na Jamai Raja na Maigizo kwenye chanel ya sinema zetu wakati mechi za kombe la dunia zinaendelea, pia nawe ni MMAMAA…😂😂
4, Mwanaume kuandika 'Jomon' badala ya Jamani, kuandika 'Pw' badala ya Poa, kuandika 'Thatha' badala ya Sasa, kumwandikia mwanaume mwenzio 'Mambo my' Huu ni UDADA, tena UDADA wa CHUO..😂 . 5, Mwanaume kunywa soda au Juice na kubakisha, kununua chakula halafu unakibakisha, kubagua bagua chakula na kujamba hovyo hovyo baada ya kushiba, huo nao ni UMAMAA..😂 . 6, Mwanaume kumuuliza mwanaume mwenzio anapata faida gani kuangalia Mpira, pia nawe ni MMAMA… . 😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Polisi::: hodi, hodi
Jamaa::: kimya
Polisi::: hodi, hodi
Jamaa::: we nani kwani?
Polisi::: sisi polisi
Jamaa::: mnataka nini?
Updated at: 2024-05-25 18:08:23 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Polisi::: hodi, hodi Jamaa::: kimya Polisi::: hodi, hodi Jamaa::: we nani kwani? Polisi::: sisi polisi Jamaa::: mnataka nini?
Polisi::: kuongea na wewe Jamaa::: kuongea na mimi?! Polisi::: ndio Jamaa::: mko wangapi? Polisi::: tuko watatu Jamaa::: kama mko watatu si muongee wenyewe…!!!