Updated at: 2024-05-25 16:24:18 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Ingawaje, akili zao hazina hitilafu watoto Albino mara nyingi hawafanyi vizuri shuleni, na huchukuliwa kuwa ni wajinga kwa sababu hawawezi kusoma vizuri ubaoni. Mara nyingi watoto Albino hujikuta wameaachwa katika shughuli za nje, ya madarasa zinazojumuisha wenzao shuleni. Walimu lazima watambue watoto Albino darasani mwao na wawe na mikakati maalumu wa kuwawezesha kufuatilia masomo. Wanafamilia pamoja na walimu shuleni wahakikishe kuwa Albino hawatengwi katika shughuli za vikundi. Kuwakutanisha na Albino wenzao au na watu wenye Albino kwenye familia zao na jamii kwa ujumla itawasaidia zaidi. Watoto Albino wanajifunza kufidia upungufu walionao wa kujithamini kwa kuweka jitihada katika masomo na shughuli nyingine. Wana mwelekeo wa kushinda zaidi katika mambo wanayojaribu. Watu weusi wengi wanaoishi na ualbino wamefanikiwa kuwa mafundi wazuri, wanasheria, wakunge wajasiriamali wataalamu wa kompyuta na hata maprofessa wa vyuo vikuu.
Inatokeaje, katika baadhi ya mazingira baba anakataa kuwa mtoto si wake?
Updated at: 2024-05-25 16:24:13 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Katika mazingira fulani, baba anapomuona mtoto ana ngozi nyeupe anakataa ya kwamba mtoto si wake akimlaumu mama wa mtoto kuwa amekuwa na mahusiano ya ngono na mzungu. Huu ni upuuzi kwa sababu kila mtu anajua kuwa watoto waliozaliwa kutoka familia za watu weusi na wazungu siyo Albino kwa mfano Rais wa Marekani Obama ni mtoto wa mama mzungu na baba mweusi.
Dhana hii potofu ni matokeo ya uelewa mdogo na kutoaminiana. Watu watakapokuwa na ufahamu na uelewa kuhusu ualbino watapunguza kuwa na hisia kama alivyofanya huyu mzazi aliyetajwa hapa juu.
Madhara ya dawa za kulevya yanadumu kwa muda gani?
Updated at: 2024-05-25 16:22:39 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Ni vigumu sana kujibu swali hili kwa sababu muda wa madhara hutegemea sababu mbalimbali kama vile aina za dawa za kulevya, njia za utumiaji, hali ya mtu na mazingira anapozitumia dawa hizo za kulevya. Mtu anaweza kuanza kutumia dawa za kulevya mara kwa mara i ili kukidhi kile anachokihitaji. Kwa baadhi ya dawa za kulevya, na baadhi ya watu, matumizi ya mara kwa mara kwa kipindi cha zaidi ya wiki mbili ni kipimo tosha cha kumfanya aishi kwa kutegemea dawa za kulevya.
Je, mtu anaweza kuambukizwa virusi vya UKIMWI na UKIMWI iwapo atavaliana nguo na mtu mwenye Virusi vya UKIMWI na UKIMWI?
Updated at: 2024-05-25 16:22:29 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Hapana, Virusi vya UKIMWI na UKIMWI hauambukizwi kwa kuvaliana nguo na mgonjwa, kwa sababu vijidudu vya UKIMWI vinakufa baada ya muda mfupi vikiwa hewani. Hata hivyo, kufuatana na kanuni za usafi, ni vizuri zaidi kuvaa nguo zilizofuliwa na kupigwa pasi.
Nifanye nini ili kuepuka kubakwa na mpenzi/ rafiki?
Updated at: 2024-05-25 16:22:07 (2 years ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kuna baadhi ya vidokezo ambavyo vinaweza kukusaidia:
1. Usikae faragha na mwenzi wako kabla hujawa tayari na kumwamini. Ongozana na marafiki wengine hasa mwanzoni mwa urafiki wenu. Msitoke tu nyie wawili hadi hapo utakapojisikia kuwa umemjua kiasi cha kumwelewa na kumwamini. Pia jiepushe kukaa sehemu za faragha naye.
2. Kama utatoka naye, hakikisha kuwa kuna mtu anayejua mnakokwenda na ni muda gani unakusudia kurudi nyumbani. Ikiwezekana kuwa na namba ya simu ya mmoja kati ya rafiki zako. Hii itakusaidia kama ikijitokeza hali ya kutaka msaada.
3. Usikubali yeye alipe gharama zote. Ni vizuri kugawa gharama hizo kati yenu. Kama mtakwenda kwenye tamasha au kupata kinywaji hakikisha kulipia nusu ya hizo gharama. Ukifanya hivyo utamzuia mwenzio mawazo ya kukufikiria “kuwa anakudai ngono“ kama malipo ya pesa yake aliyotumia.
4. Ni vizuri kutafakari na kuweka kichwani kabla ya kwenda naye popote juu ya nini unachotaka na kile usichotaka kitokee.
5. Onyesha wazi kuwa unaposema “hapana“ unamaanisha “hapana“ usimpe nafasi ya kuchukulia hiyo “hapana“ kuwa ndiyo.
6. Amini hisia zako. Kama unaona unalazimishwa usisite kueleza maoni yako / unavyojisikia. Ikibidi ondoka sehemu hiyo.