Updated at: 2024-05-25 10:23:11 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI YA WALI
Mchele - 3 Magi
Mafuta - 1/4 kikombe
Karoti unakata refu refu - 3
Vitunguu maji kata vikubwa vikubwa - 1 kikubwa
Pilipli manga - 1/2 kijicho chai
Hiliki - 1/2 kijiko chai
Karafuu ya unga - 1/4 kijiko cha chai
Mdalasini wa unga - 1/2 kijiko cha chai
Zaafarani (ukipenda) roweka katika maji - 1 kijiko cha chai
Zabibu kavu (ukipenda) - 1/4 kikombe
Chumvi kiasi
KUPIKA WALI
Kwenye sufuria tia mafuta na kaanga karoti kidogo. Tia vitunguu kisha tia bizari zote. Tia maji kiasi (kutegemea aina ya mchele) na chumvi Tia mchele upike uwive. Karibu na kuwvia tia zabibu ukipenda. Funika endelea kuupika hadi uwive.
MAHITAJI KWA NYAMA
Nyama - 2 Ratili (LB)
Chumvi - Kiasi
Mafuta - 1/4 kikombe
Kitunguu (kata virefu virefu) - 1 Kikubwa
Pilipili mboga kubwa - 2 ukipenda moja nyekundu moja kijani unazikata vipande virefu virefu.
Figili mwitu (celery) kata vipande virefu virefu- Miche miwili.
KUPIKA NYAMA
Chemsha nyama hadi iwive Ikaange kwa mafuta hadi iwe nyekundu Weka vitunguu, pilipili mboga na figili mwitu Kaanga kidogo tu kama dakika moja. Tayari kuliwa na wali.
Updated at: 2024-05-25 10:23:11 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI VYA TUNA
Tuna (samaki/jodari) - 2 Vikopo
Vitunguu (kata kata) - 4
Nyanya zilizosagwa - 5
Nyanya kopo - 3 Vijiko vya supu
Viazi (vilivyokatwa vipande vidogo - cubes) - 4
Dengu (chick peas) - 1 kikombe
Kitunguu saumu(thomu/galic)&Tangawizi iliyosagwa 1 Kijiko cha supu
Hiliki - 1/4 kijiko cha chai
Mchanganyiko wa bizari - 1 kijiko cha supu
Chumvi - kiasi
Pilipili manga - 1 Kijiko cha chai
Vipande cha Maggi (Cube) - 2
VIAMBAUPISHI VYA WALI
Mchele - 3 Vikombe vikubwa (Mugs)
Mdalasini - 2 Vijiti
Karafuu - chembe 5
Zaafarani - kiasi Jirsh (Komamanga kavu au zabibu kavu -raisins) - 1/2 Kikombe
JINSI YA KUANDAA
Kosha Mchele na roweka. Kaanga vitunguu hadi viwe rangi ya hudhurungi (brown) chuja mafuta uweke kando. Kaanga viazi, epua Punguza mafuta, kaanga nyanya. Tia thomu/tangawizi, bizari zote, vipande vya Maggi, nyanya kopo, chumvi. Mwaga maji ya tuna iwe kavu, changanyisha kwenye sosi. Tia zaafarani kidogo katika sosi na bakisha ya wali. Chemsha mchele pamoja na mdalasini na karafuu. Karibu na kuwiva, chuja maji utie katika chombo cha kupikia katika jiko (oven) Nyunyizia zaafarani, mwagia vitunguu, viazi, na dengu juu ya wali. Mwagia sosi ya tuna na pambia jirshi (au zabibu). Funika wali na upike katika jiko moto wa 450º kwa muda wa kupikika wali. Epua upakue.
Updated at: 2024-05-25 10:37:40 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Choroko kikombe 1 na nusu Nazi kopo 1 Kitunguu kikubwa 1 Nyanya 1/2 kopo Swaum 1 kijiko cha chai Curry powder 1 kijiko cha chai Chumvi kiasi Olive oil Pilipili nzima
Matayarisho
Loweka choroko usiku mzima kisha zichemshe mpaka ziive na ziweke pembeni. Baada ya hapo saga pamoja nyanya, kitunguu, na swaum kisha vipike mpaka maji yote, baada ya hapo tia mafuta na curry powder, pika mpaka nyanya zitoe mafuta kisha tia choroko,tui la nazi, maji nusu kikombe,pilipili na chumvi, kisha koroga vizuri na uache ichemke. Pika mpaka tui la nazi litakapoiva na rojo ibakie kidogo sana, kisha ipua na mboga yako itakuwa tayari kwa kuliwa. Mi huwa napenda kuila na wali ila hata na ugali au chapati inaenda pia.
Updated at: 2024-05-25 10:37:42 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Bamia (okra) 20 Nyanya chungu (garden eggs) 5 Magadi soda (Bicabonate soda) 1/4 ya kijiko cha chai Nyanya (fresh tomato) 1 Chumvi (salt) kidogo Pilipili 1/4
Matayarisho
Osha bamia, nyanya chungu na nyanya kisha vikatekate katika vipande vidogovidogo. Baada ya hapo vitie kwenye sufuria na vitu vyote vilivyobakia na kisha tia maji kidogo.Chemsha mpaka bamia na nyanya chungu ziive na vimaji vibakie kidogo sana. Baada ya hapo ziponde na mwiko kidogo kisha zikoroge na uipue na mlenda utakuwa tayari kwa kuliwa na ugali.
Updated at: 2024-05-25 10:37:43 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele 2 vikombe vya chai Choroko kikombe 1 na 1/2 Nazi kopo 1 Swaum 1 kijiko cha chakula Kitunguu 1 kikubwa Binzari nyembamba 1 kijiko cha chai Chumvi Mafuta
Matayarisho
Loweka choroko usiku mzima, pindi ukianza kupika loweka mchele nusu saa kisha katika sufuria kubwa, kaanga vitunguu vikianza kuwa vya brown tia swaum na binzari nyembamba kisha tia choroko, mchele, chumvi,nazi na maji mengi kiasi yakuivisha choroko pamoja na mchele. Pika mpaka vitu vyote viive na viwe vilaini kisha upondeponde kiasi.Baada ya mseto wako kuiva utakuwa unaonekana kama uji wa mchele vile. Na Baada ya hapo mseto wako utakuwa tayari kwa kuliwa na mboga yoyote uipendayo.Inapendeza zaidi kuliwa vile tu ukishamalizwa kupikwa
Updated at: 2024-05-25 10:37:46 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Ndizi laini (Matoke 6) Viazi mbatata (potato 3) Samaki wabichi wa wastani ( Fresh tilapia 2) Kitunguu swaum (garlic 6 cloves) Tangawizi (fresh ground ginger vijiko 2 vya chai) Nyanya ya kopo (tin tomato 1/2 kopo) Vitunguu (onion 1) Pilipili (chilli 1 nzima) Chumvi (salt to your taste) Mafuta (vegetable oil) Limao (lemon 1/2) Curry powder (1/2 kijiko cha chai)
Matayarisho
Safisha samaki kisha wakate vipande vitatu. Wakaushe maji kisha wamarinate na kitunguu swaum,tangawizi, chumvi, na limao kwa muda wa masaa 2. baada ya hapo waoke kwenye oven kwa muda wa dakika 30. baada ya hapo andaa ndizi na viazi kwa kuzimenya na kuziosha kisha ziweke pembeni. Kisha katakata vitunguu maji, Tangawizi, vitunguu swaum na nyanya kisha vitie kwenye blenda na usage mpaka mchanganyiko usagike vizuri. Baada ya hapo tia mchanganyiko katika sufuria na ubandike jikoni, acha uchemke mpaka maji yote yakauke. Maji yakisha kauka punguza moto na utie mafuta, curry powder, pilipili na chumvi. Kaangiza mpaka mchanganyiko uive na baada ya hapo tia viazi na maji kiasi na uache viazi vichemke mpaka vikaribie kuiva kisha tia ndizi na samaki na ufunike. Pika mpaka ndizi na viazi viive. Baada ya hapo chakula kitakuwa tayari kwa kuseviwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:44 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Pilipili hoho (Red pepper 3) Cougette 1 Kitunguu (onion 1) Uyoga (mashroom 1 kikombe cha chai) Carrot 1 Nyanya (fresh tomato 1) Nyanya ya kopo iliyosagwa (tomato paste 3 vijiko vya chai) Giligilani (fresh coriander) Binzari manjano (Turmaric 1/2 ya kijiko cha chai) Curry powder 1/2 ya kijiko cha chai Chumvi (salt) Mafuta (vegetable oil)
Matayarisho
Kata hoho kati na utoe moyo wake kisha ziweke pembeni, Kisha katakata cougette, kitunguu, uyoga, carrot, nyanya katika vipande vidogo vidogo, Weka sufuria jikoni na uanze kupika uyoga kwa muda wa dakika 5, kisha weka curry powder, turmaric na chumvi na kaanga kidogo kisha weka vegetable zilizobakia pamoja na nyanya ya kusaga pamoja na giligilani. Zikaange kwa muda wa dakika 5 kisha zitie kwenye hoho na kisha uzibake kwa muda wa dakika 20 na hapo zitakuwa tayari kuseviwa na wali. Wali: angalia katika recipe zilizopita
Updated at: 2024-05-25 10:37:38 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Majimbi (Eddoes) kiasi 6 au 7
Nyama ng’ombe ½ kilos
Tangawizi ilosagwa 1 kijiko cha kulia
Haldi (bizari manjano/turmeric) ½ kijiko cha chai
Tui zito la nazi vikombe 2
Chumvi kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Safisha nyama kisha weka chumvi, bizari ya manjano, tangawizi mbichi, ukaushe kwanza katika sufuria kwa kukaanga kaanga. Ikianza kukauka, weka maji funika uchemshe iwive. Menya majimbi ukate kate na uweke katika sufuria nyengine. Mimina supu na nyama katika majimbi uchemshe yawive majimbi. Mwisho weka tui zito la nazi uchanganye vizuri kisha weka katika moto kidogo tu bila kufunika yakiwa tayari.
Updated at: 2024-05-25 10:23:10 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Unga - 6 vikombe
Samli - ½kikombe
Baking Powder - ½kijiko cha chai
Maziwa- 1 kikombe
Maji -Kisia kiasi kama unga bado mzito
VIAMBAUPISHI VYA SHIRA
Sukari - 5 vikombe
Maji - 2 1/2 vikombe
Vanilla - 2 vijiko vya chai
Rangi ya orange - 1 kijiko cha chai
Iliki ya unga - 1 Kijiko cha chai
MAANDALIZI
Changanya unga wa dengu, samli, baking powder pamoja na maziwa katika mashine ya keki (cake mixer). Ukisha changanya angalia kama mchanganyiko wako umekua mwepesi kidogo kuliko wa keki, kama bado mzito basi ongeza maji kiasi. Kisha weka mafuta kiasi kwenye karai,weka na samli kikombe kimoja, weka kwenye moto wa kiasi. Mafuta yakisha pata moto, chukua kijiko kikubwa cha matundu chota mchanganyiko wako na kijiko cha kawaida tia kwenye kijiko cha matundu. Hakikisha kijiko cha matundu kiwe juu ya karai ili mchanganyiko wako uchuruzike ndani ya mafuta yalio pata moto. Pika ndani ya mafuta mpaka iwive, ila usiache ikawa brown. Toa mchanganyiko ulowiva tia ndani ya shira uliyo pika. Hakikisha shira iwe imepoa kabla ya kutia mchanganyiko huo. Endelea kupika mchanganyiko wako mpaka uishe, kila ukitoa katika mafuta hakikisha unatia ndani ya shira. Ukishamaliza wote kanda huo mchanganyiko ulokua ndani ya shira mpaka uone shira yote imekauka (yaani iwe imeingia ndani ya mchanganyiko). Tupia zabibu kavu na lozi zilizo katwa, changanya na mkono. Wacha mchanganyiko katika bakuli, funika na foil mpaka siku ya pili. Siku ya pili chukua mchanganyiko kiasi katika mkono tengeneza mviringo (round).
MAANDALIZI YA SHIRA
Katika sufuria, tia sukari, maji, iliki, vanilla na rangi. weka kwenye moto wacha ichemke mpaka itowe povu (bubbles) juu. Kisha toa povu, wacha shira kwenye moto kama dakika 3. Hakikisha shira yako iwe inanata kiasi kwenye vidole, lakini iwe nyepesi kidogo kuliko shira ya kaimati.
Jinsi ya kupika Pilau ya Mpunga Na Nyama Ya Ng’ombe
Updated at: 2024-05-25 10:23:15 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mpunga - 4 vikombe
Nyama - 1 kilo moja
Kitunguu maji - 3
Mbatata/viazi - 7 vidogodogo
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi ilosagwa 3 vijiko cha supu
Bizari nzima/ya pilau/uzile/cumin - 3 vijiko vya supu
Mdalasini - 3 vipande
Hiliki - 7 punje
Pilipili manga nzima - 1 kijiko cha supu
Chumvi kiasi
Mafuta - ½ kikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha mchele weka kando Katakataka vitunguu slice ndogo ndogo. Weka mafuta katika sufuria kisha ukaange vitunguu pamoja na mdalasini, hiliki pilipilimanga. Vitunguu vikigeuka rangi unatia kitunguu thomu na tangawizi. Tia supu kidogo na nyama, kisha tia bizari ya pilau/uzile, na viazi/mbatata. Maliza kutia supu yote, na ikiwa ni kidogo ongeze maji kiasi cha kuivisha mchele. kisha tia mchele ufunike hadi wali uwe tayari. Ikiwa unatumia mkaa palia juu yake, ikiwa hutumii uache uive kwa moto mdogo mdogo.