Mapishi ya Haliym Ya Nyama Mbuzi -Bokoboko La Pakistan
Updated at: 2024-05-25 10:23:16 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Nyama ya mbuzi au ng’ombe ya mafupa - 2 LB
Mchanganyiko wa dengu (hadesi, mchele, chooko, ngano, dengu n.k au nunua ya tayari iliyokwisha changanywa - 2 Vikombe
Kitungu maji (vikate vidogo) - 1
Mafuta - ¼ Kikombe
Nyana kata ndogo ndogo - 1
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawazi iliyosagwa - 1 Kijiko cha supu
Bizari ya haliym - 2 vijiko vya supu
Nyanya ya kopo - 2 vijiko vya supu
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Chemsha nyama na chumvi ½ kijiko mpaka iive, toa mafupa. Chemsha mchanganyiko wa dengu mpaka ziive. Katika sufuria weka mafuta, kaanga vitunguu vilainike, tia thomu na tangawizi, bizari ya haliym, nyanya ya kopo. Kaanga mpaka iwive. Tia nyama iliyowiva na supu yake kidogo. Tia mchanganyiko wa dengu tia kwenye mashine ya kusaga (blender), saga na ile supu ya nyama isagike vizuri Mimina kwenye sufuria changanya, tia ndimu kidogo, acha moto mdogo mdogo kwa muda wa dakika 15. Tia katika bakuli, pambia kwa vitunguu vilivyokaangwa vya rangi ya hudhurungi vikavu, pilipili mbichi (ukipenda) na kotmiri, ikiwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:23:00 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Unga wa ngano (self risen flour) kikombe 1na 1/2 Sukari (sugar) 1/4 kikombe Barking powder 1/2 kijiko cha chai Magadi soda (bicarbonate soda) 1 kijiko cha chai Mafuta 2 vijiko vya chai Mafuta ya kukaangia Maji ya uvuguvugu kiasi
Matayarisho
Changanya unga na vitu vyote (kasoro mafuta ya kuchomea) kisha ukande (hakikisha unakuwa mgumu) Baada ya hapo sukuma na ukate shape uipendayo (hakikisha unakata vipande vinene kiasi na sio kama mandazi) Baada ya hapo ziweke sehemu yenye joto na uache ziumuke. Zikisha umuka zikaange katika moto mdogo ili ziive mpaka ndani. Zikisha iva zitoe na uziweke katika kitchen towel ili zichuje mafuta. Ziache zipoe na hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.
Mapishi ya Pilau Ya Nyama Ng'ombe Karoti Na Zabibu
Updated at: 2024-05-25 10:37:34 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo - Nyama
Nyama ng’ombe ya mifupa ilokatwa vipande - 1 kilo
Tangawizi na thomu (somu/garlic) ilosagwa - 2 vijiko vya supu
Bizari mchanganyiko/garama masala - 1 kijiko cha chai
Chumvi - Kiasi
Vipimo - Wali
Mchele - 4 glass
Mbatata/viazi menya katakata - 3 kubwa
Vitunguu katakata - 5
Kitunguu thomu kilosagwa (garlic/somu) - 1 kijiko cha supu
Hiliki ya unga - 1 kijiko cha chai
Bizari nzima ya pilau/cumin - 1 mti
Samli au mafuta - 2 Vijiko vya supu
Karoti zilokatwakatwa nyembamba - 6-7
Zabibu - Kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Katika sufuria weka mafuta kijiko kimoja cha supu tia nyama na viungo vyake. kaushe katika moto hadi ikaribie kukauka kisha tia maji kiasi cha kuivisha na kubakisha supu ya mchele. Katika sufuria ya kupikia weka samli au mafuta ishike moto. Tia mbatata/viazi kaanga, tia vitunguu kaanga kidogo. Tia kitunguu thomu, hiliki, bizari ya pilau endelea kukaanga hadi viwe rangi ya brown kidogo. Tia mchele kaanga kidogo, kisha mimina nyama na supu yake. Funika wali uwive. Weka kikaangio katika moto, tia samli kijiko kimoja kisha tia karoti na zabibu, kaanga kwa sekunde chache tu kwa ajili ya kulainisha karoti na zabibu. Utakapopakuwa wali, pambia juu karoti na zabibu.
Jinsi ya kupika Cookies Za Jam Ya Peach Na Raspberry
Updated at: 2024-05-25 10:34:43 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Unga kikombe 1 ½
Siagi ½ kikombe
Sukari ½ kikombe
Yai 1
Vanilla 1 kijiko cha chai
Jam ya peach na raspberry
MAANDALIZI
Wash oven moto wa takriban 180 – 190 Deg F Piga siagi na sukari katika mashine mpaka iwe laini na nyororo (creamy) kisha weka yai na vanilla. Tia unga kidogo kidogo uchanganye kwa mwiko wa mbao (wooden spoon). Pakaza mkononi unga uchukue vidonge ubonyeze kufanya vishimo vya kuwekea jam. Panga katika treya uliyopakaza siagi. Tia nusu yake jam ya peach na nusu jam ya raspberry Bake katika oven kiasi robo saa mpaka ziwive na kugeuka rangi ya brown light. Epua vikiwa tayari