Updated at: 2024-05-25 10:34:47 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vitumbua ni aina ya vitafunwa vya chai ambavyo hutengenezwa kwa kutumia unga wa mchele. Kiasili vitumbua ni chakula ambacho hupendelewa sana na watu wa pwani. Na mara nyingi wamekuwa wakipika kwa kuchanganya na nazi ili kuvifanya view na ladha nzuri zaidi
Mahitaji:
Unga wa mchele ½ kg Sukari vijiko 4 vya mezani Tui bubu la nazi Mafuta ya kupikia Unga wa hiliki ½ kijiko cha chai Hamira kijiko 1 cha chai Chuma cha vitumbua
Maandalizi:
Chukua unga wa mchele na weka kwenye bakuli au sufuria ya kilo moja Weka hamira kisha weka sukari kisha miminia tui katika mchanganyiko wako Weka hiliki koroga hadi view uji mzito Acha uji huo kwa muda wa saa moja hadi uumuke, mara nyingi kuumuka kunategemea na hali ya hewa, Baada ya hapo weka mafuta kijiko kimoja cha chakula kila kishimo acha yapate moto Kisha kaanga virumbua vyako
Mapishi ya Ugali Mchuzi Wa Samaki Nguru Wa Nazi Na Bamia Za Kukaanga
Updated at: 2024-05-25 10:37:38 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo Vya Ugali:
Unga wa mahindi/sembe - 4
Maji - 6 takriban
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Chota unga kidogo katika kibakuli uchanganye na maji kidogo . Weka maji mengineyo katika sufuria kwenye moto. Changanya na mchanganyiko mdogo ufanya kama uji. Kisha kidogo kidogo unaongeza sembe huku unakoroga na kuusonga ugali hadi uive.
Vipimo Vya Mchuzi Wa Samaki Wa Nazi
Samaki nguru - 5 vipande
Pilipili mbichi ilosagwa
Kitunguu maji kilosagwa - 1 kimoja
Nyanya ilosagwa - 2
Haldi/tumeric/bizari ya manjano - ¼ kijiko cha chai
Chumvi - kiasi
Ndimu - 2 kamua
Tui la nazi zito - 2 vikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Baada ya kumuosha samaki, weka katika sufuria. Tia chumvi, ndimu, pilipili mbichi ilosagwa. Tia vitunguu na nyanya zilosagwa Mkaushe kwa hivyo viungo, akianza kukauka tia tui la nazi. Acha kidogo tu katika moto tui liwive mchuzi ukiwa tayari.
Vipimo Vya Bamia
Bamia - ½ kilo takriban
Nyanya kopo - 1 kijiko cha chai
Methi/uwatu/fenugreek seeds ilosagwa - 1 kijiko cha chai
Dania/corriander ilosagwa - ½ kijiko cha chai
Chumvi - kiasi
Mafuta - 1 kikombe cha kahawa
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Katakata bamia kwa urefu. Weka mafuta katika karai, kisha tia bizari zote na nyanya kopo, kaanga kidogo. Tia bamia endelea kukaanga, kisha acha katika moto mdogomdogo ufunike. Kila baada ya muda funua karai ukaange bamia hadi ziwive zikiwa tayari.
Updated at: 2024-05-25 10:37:57 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Unga 300gm
Siagi 225gm
Icing Sugar 60gm
Chokoleti iliyokoza (Dark Chocolate) - 225gm
Vanilla – Vijiko 2 vya chai
Yai -1
Baking Powder ½ kijiko cha chai
Njugu za vipande ½ kikombe cha chai
Njugu zilizosagwa ¼ kikombe cha chai
JINSI YA KUTAYARISHA
Piga sukari na siagi katika mashine ya keki mpaka iwe laini Kisha mimina yai na vanilla koroga vizuri Mwisho mimina unga na baking powder polepole mpaka ichanganyike. Kata kata umbo (shape) lolote unavyopenda (kama nyota, pembetatu,duara, kopa n.k) Panga kwenye treya na choma kwa moto wa 350°C , vikibadilika rangi kidogo tu vitoe Yayusha chokoleti tia kwenye bakuli ndogo. kisha paka kwa kijiko au chovyea upande mmoja mmoja wa biskuti kisha nyunyizia njugu za kipande na njugu ya unga. Panga kwenye sahani tiyari kunywewa na chai ya maziwa au kahawa.
Jinsi ya kuishi maisha marefu (Mambo ya kuzingatia ili uishi maisha marefu)
Updated at: 2024-05-25 10:34:45 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kuishi ukiwa na afya na kuishi maisha marefu kunawezekana kwa kubadili hali ya maisha unayoishi inayoharibu afya yako mfano uvutaji wa sigara, unywaji wa pombe kupita kiasi,kutokufanya mazoezi na kutokula matunda na mbogamboga.
Mambo yanayoweza kukusaidia kuishi maisha marefu ni kama yafuatayo
Kuuandaa mwili kwa maisha marefu kwa kufanya mazoezi
Kuwa makini kutambua na kutibu matatizo ya kiafya
Kuepuka mazingira na kufanya kazi kwa namna au kazi zinazoweza kudhuru maisha yako. Mfano kuendesha gari bila kufuata utaratibu, kutokuvaa vifaa vya kujikinga wakati wa kazi
Epuka vitu vyenye sumu vinavyoweza kudhuru afya yako na kukuletea matatizo ya kiafya kama dawa za mimea na mifugo, zitumie kama inavyotakiwa
Usinywe pombe, usivute sigara wala kutumia dawa za kulevya
Updated at: 2024-05-25 10:37:47 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Dagaa (dried anchovies packet 1) Unga wa ugali (corn meal flour 1/4 kilo) (unaweza kutumia unga wa choice uipendayo) Nyanya ya kopo (tin tomato 1/2) Kitunguu maji (onion 1) Limao (lemon 1/4) Pilipili mbuzi nzima bila kukata (scotch bonnet pepper1, do not chop) Chumvi (salt 1/4 ya kijiko cha chai) Mafuta (vegetable oil) Hoho (green pepper)
Matayarisho
Chambua dagaa kwa kutoa vichwa vyao na utumbo, baada ya hapo waloeke katkika maji ya moto kwa muda wa dakika 5 na uaoshe tena katika maji ya baridi na uwakaushe uwaweke pembeni. Ukishamaliza katakata kitunguu na uandae nyanya tayari kwa upishi. Bandika sufuria ya kupikia dagaa jikoni na utie mafuta, yakishapata moto tia vitunguu pamoja na dagaa. Kaanga mpaka dagaa wawe light brown kisha tia nyanya, chumvi na pilipili. Pika nyanya mpaka ziive (ukitaka kujua kama nyanya zimeiva utaona zinatengana na mafuta) Baada ya hapo kamulia limao kidogo sana na tia pilipili hoho na zipike kama dakika mbili. kisha ipua. Ukisha maliza kupika dagaa andaa chungu cha ugali. Kwanza unatakiwa kuchemsha maji ya moto, kisha koroga pembeni unga kiasi katika maji ya baridi na utie kwenye maji yanayochemka, Fanya kama unatengeneza uji, uji wa ugali ukishachemka tia unga na uanze kuusonga mpaka ugali uive. Ukisha iva pakua na usevu na mboga tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:23:09 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Philo (thin pastry) manda nyembamba - 1 paketi
Siagi - ¼ Kikombe cha chai
Baking powder - 2 Vijiko vya chai
Pistachio/ lozi - 2 vikombe vya chai
Mafuta - ½ Kikombe
VIAMBAUPISHI VYA SHIRA
Sukari - 2 Vikombe vya chai
Maji - 2 ½ Vikombe vya chai
ndimu - ½ kijiko cha chai
JINSI YA KUANDAA
Tafuta treya iliyokuwa sawa na ukubwa wa hizo manda nyembamba (philo) au zikate hizo manda kwa ukubwa wa treya (mraba au mstatili) Kisha yeyusha siagi changanya na mafuta. Kisha panga manda moja pakaza mafuta juu yake kisha weka manda nyingine juu yake kisha pakaza mafuta tena weka manda nyingine juu yake, endelea kufanya hivyo mpaka ziwe kama sita au saba kisha nyunyizia pistachio na lozi halafu panga tena manda na mafuta manda na mafuta tena sita au saba kisha nyunyizia tena pistachio na lozi. Panga namna hivyo mpaka treya ijae inapofika manda ya mwisho kata vipande vya mraba vidogodogo humo humo kwenye treya kisha nyunyizia mafuta yaliyobaki. Washa moto wa oven 350°F kwa muda wa dakika 20 au hadi rangi ibadilike kidogo (isikauke sana) Chemsha syrup yako kama shira ya majimaji lakini isiwe nzito sana ikishakuwa tayari mwisho tia ndimu acha ipoe kidogo kisha miminia juu ya treya yote halafu malizia kunyunyizia pistachio na lozi zilizobaki. Zikishakuwa tayari zipange kwenye sahani tayari kwa kuliwa.
ANGALIZO
Ukishatoa treya kwenye oven wacha ipoe kidogo na syrup yako pia wacha ipoe kidogo kabla hujamimina, ukitia ya motomoto zitalainika. Manda nyembamba za baklawa zinauzwa tiyari madukani kwenye pakiti.
Updated at: 2024-05-25 09:52:20 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Unga wa mchele ( Vikombe 2 vikubwa) Sukari (Nusu ya kikombe kikubwa) Hamira ( Nusu ya kijiko cha chai) Hiliki (Nusu ya kijiko cha chai) Tui la nazi ( Kikombe kimoja kikubwa) Unga wa ngano (Vijiko viwili vya chakula) Mafuta ya kuchomea (Vegetable oil)
Matayarisho
Unachanga unga, sukari, hamira, hiliki, unga wa ngano na tui la nazi pamoja katika bakuli la plastiki. Kisha unaukoroga mpaka mchanganyiko unakuwa kama uji mzito. Kava bakuli lililokuwa na mchanganyiko kisha hifadhi katika sehemu yenye joto kwa muda wa masaa matatu.
Jinsi ya kupika
Weka chuma cha kuchomea vitumbua katika moto wa wastani, kisha weka mafuta kwenye chuma cha kuchomea ( Kijiko kimoja cha chai) mafuta yakisha pata moto tia uji wako (upawa mmoja) katika kila shimo la chuma cha kuchomea. Acha mpaka kitumbua kikauke kisha geuza na tia mafuta. Acha upande wa pili wa kitumbua mpaka uwe rangi ya kahawia na hapo kitumbua kitakuwa kimeiva utakitoa. Rudia hatua hizo kwa vitumbua vyote vilivyobaki.
Updated at: 2024-05-25 10:23:13 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele wa Basmati /Pishori - 4 vikombe
Kuku
Vitunguu - 3
Nyanya/Tungule - 2
Tangawizi mbichi ilosagwa - 2 vijiko vya supu
Kitunguu saumu(thomu/galic) kilosagwa - 1 kijiko cha supu
Pilipili mbichi nzima - 3
Ndimu - 2
Garama Masala/bizari mchanganyiko - 1 kijiko cha supu
Haldi/tumeric/bizari manjano - 1 kijiko cha chai
Pilipilu ya unga nyekundu - 1 kijiko cha chai
Mtindi /yoghurt - 3 vijiko vya supu
Mafuta ½ kikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha mchele, roweka. Safisha kuku vizuri, mkate vipande vya saizi ya kiasi weka katika bakuli. Katika kibakuli kidogo, changanya tangawizi mbichi, thomu, bizari zote, pilipili nyekundu ya unga, chumvi, mtindi, kamulia ndimu. Punguza mchanganyiko kidogo weka kando. Mchanganyiko uliobakia, tia katika bakuli la kuku uchanganye vizuri arowanike (marinate) kwa dakika chache hata nusu saa au zaidi. Weka kuku katika treya ya kuoka au kuchoma katika oveni kisha mchome (grill) uwe unageuzageuza hadi aive. Epua, weka kando. Katakata vitunguu, nyanya/tungule, pilipili boga weka kando. Katika sufuria ya kupikia biriani, tia mafuta, kaanga vitunguu hadi vigeuke rangi ya hudhurungi (brown). Tia nyanya na pilipili mbichi, pilipili boga na mchanganyiko uliopunguza awali. Tia kuku uchaganye vizuri. Wakati unakaanga vitunguu ili uokoe muda, huku chemsha mchele uive nusu kiini, mwaga maji, chuja. Punguza masala nusu yake weka kando. Mimina wali kiasi juu ya masala, kisha mimina masala yaliyobakia kisha juu yake tena mimina wali. Funika upike katika oveni hadi uive. Changanya unapopakua katika sahani.
Updated at: 2024-05-25 10:37:49 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viambaupishi
Mchele 2 Mugs
Mboga mchanganyiko za barafu 1 Mug
(Frozen veg)
Tuna (samaki/jodari) 2 kopo
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi 2 vijiko vya supu
Garam masala 1 kijiko cha supu
Nyanya 2
Kitungu maji 1
Mdalasini nzima 2 vijiti
Karafuu 6 chembe
Pilipili mbichi 1
Chumvi kiasi
Viazi 3
Maji 2 ½ Mugs
Mafuta 3 vijiko vya supu
Jinsi ya kuandaa na kupika
Osha mchele na uroweke kwa muda wa dakika 20 Tia mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu maji mpaka kigeuke rangi ya hudhurungi (brown). Mimina viazi, thomu na tangawizi, bizari zote na kaanga. Tia nyanya uliyokatakata ikaange mpaka iwive. Tia tuna endelea kukaanga kidogo tu. Tia maji, yatakapochemka tia mchele. Punguza moto uwe mdogo funika kwa muda wa ½ saa hadi wali ukauke na uwive. Utakuwa tayari kuliwa.