Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
☰
AckyShine

Mambo ya Msingi kuyajua Ili uishi na watu vizuri

Featured Image

Nimezipenda hizi nasaha. Naamini na nyinyi wenzangu hamtakosa japo machache ya kujifunza:-
1. Epuka hasira za ovyo na kila mtu, kuwa msikivu kabla ya kukimbilia maamuzi (elewa kuwa ukiwa na hasira huwezi kupata suluhu ya jambo)
2. Usiwatendee wengine ubaya ukadhani kuwa utakuwa salama (ubaya hulipwa kwa ubaya, ipo siku ubaya wako kwa wengine utakurejea kama sio kuwarejea watu wa kizazi chako)


3. Usichukue maamuzi kabla ya kutafiti ukweli (pengine wapo wanadamu wanaopenda kuonekana wao wema kwa kuumiza wengine). Mtuhumu mtu lakini mpe muda wa kumsikiliza, usimshambulie mtu kwa maneno makali bila kuujua ukweli, ukijua ukweli nafsi inaweza kukusuta.


4. Mchukulie kila mwanadamu ni mkosaji (tambua kuwa hata wewe unawakosea sana wengine na wanakuvumilia. Hivyo usiwe mwepesi wa kuwaadhibu wenzio kwa ubaya).


5. Usipande mbegu ya chuki na ubaya katika jamii unayoishi ukadhani itakuacha salama (chuki hukua kama mti utambaao, ukiipanda ndani ya jamii yako, haitatoka kwako na inaweza kutafuna kizazi chako ukajutia.


6. Tambua kuwa yule unayeishi nae ni mwanadamu kama wewe, mpe heshima na mwonyeshee upendo hata kama huoni anafanana nawe. Maisha ni duara huenda ulikuwa kama yeye au atakuja kuwa kama wewe baadae.


6. Usiwe muongeaji ovyo ovyo na usiye na subira. Kuongea sana kunapoteza busara.


7. Jiepushe na maisha ya kusukumwa na wengine kufanya jambo usilojua manufaa yake. Jifunze kujitegemea kiakili. Sio kila unayemdhania rafiki moyoni mwake yupo pamoja nawe, na ukashirikiana nae, wengi wa marafiki zetu hututumia sana kuliko tunavyoweza kuwatumia wao.


8. Usipende sana kugombana na watu kwa njia ya maongezi yanayodumu kama vile, ujumbe wa maandishi, mawasiliano ya simu au ujumbe wa maneno (SMS). Kumbuka kuwa maneno yanaishi kuliko ugomvi au uadui, ipo siku yatakurudi na utajiona mpumbavu na kukosa pa kujificha. Jifunze kusubiri.


9.Usifumbue mdomo wako kutamka ubaya au kunyanyua kidole chako kuandika ubaya juu ya mwenzio bila kujiuliza mara mbili moyoni mwako hatima ya unachokitoa kwa mwingine.


10. Jishushe na jifunze kusikiliza wengine wakati wa mazungumzo ili uweze kujifunza kabla ya kukurupuka kujibu, usikivu ni kipimo cha busara, mtu anayekurupuka kujibu jibu kila anachosikia hawezi kuwa kiongozi, Mume au Mke mwema kwani mara nyingi atapotoka tu.


10. Usitunze hasira nyingi moyoni kwani hasira hukaa kifuani mwa mpumbavu. Jitahidi pia kuepuka kuwa na hasira mara kwa mara na zisizo na maana. Elewa kuwa hasira zisizo maana hukupunguzia maisha na kukupa maumivu wewe mwenyewe kuliko yule uliyemfanyia hasira, utakufa kwa magonjwa kabla ya wakati ufaao.


11. Thamani yako inategenezwa na watu wengine, wewe kama ni mtoto, mheshimu sana mzazi wako na kama umeoa au kuolewa, heshimu wazazi na familia ya mke au mumeo kwa kuwa bila wao, usingekuwa hivyo ulivyo leo unajivunia ndoa njema, kwa kuwa yupo mtu alimzaa huyo mwenzio. Mheshimu kwa lolote liwe jema au baya, utalipwa kwa wakati ufaao.


13. Usijibizane na mtu usiyemjua au ambaye hawezi kukupunguzia kitu katika maisha yako. Tambua kuwa unapunguza sehemu kubwa ya maisha yako kwa kutafuta magomvi na mtu wa mbali nawe.


14. Kumbuka asili yako, kumbuka upo hapo kwa kuwa kuna mahali ulitoka, maisha yanabadilika, usidharau pale ulipokuwa zamani kwa kuwa ndipo palipokufanya leo uwe hapo.


15. Subiri, sikiliza, elekeza, vumilia. Elewa sio kila mtu ana uelewa kama wako. Jitahidi kuwa mvumilivu katika kila jambo, usiinuke kuwafokea au kuwakaripia wengine kwa jambo ambalo pengine nao wanahitaji muda kueleweshwa ili walifanye vyema. Kumbuka sana, kuna wakati nawe ulikuwa huelewi kabisa lakini wapo wenzio walikuvumilia, wakakuelekeza njia njema, kufokea wengine mara kwa mara sio njia njema ya kuwafundisha bali ni kuwaweka mbali nawe.


Kumbuka: Ishi kwa kumpendeza Mungu.






Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE




Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke





Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.





[products columns="2" ids="30827"]


AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Je, kuna umuhimu wa kufanya ngono/kufanya mapenzi kwa mara kwa mara katika uhusiano?

Je, kuna umuhimu wa kufanya ngono/kufanya mapenzi kwa mara kwa mara katika uhusiano?

Je, kuna umuhimu wa kufanya ngono/kufanya mapenzi kwa mara kwa mara katika uhusiano? Hili ndilo s... Read More

Kukabiliana na Mazoea ya Kutokuelewana na Kupata Amani na Furaha katika Familia Yako

Kukabiliana na Mazoea ya Kutokuelewana na Kupata Amani na Furaha katika Familia Yako

Karibu katika makala hii ya kipekee ambayo inalenga kukupa ushauri wa kitaalamu kuhusu kukabilian... Read More

Kukabiliana na Mazoea ya Uchoyo katika Mahusiano: Kufanya Maamuzi ya Fedha kwa Pamoja

Kukabiliana na Mazoea ya Uchoyo katika Mahusiano: Kufanya Maamuzi ya Fedha kwa Pamoja

Mahusiano yanahitaji kuwa na uwazi, upendo, hisia na urafiki. Moja ya mambo ambayo yanaweza kuhar... Read More

Kusisimua Mwili na Akili: Jinsi ya Kuleta Msisimko katika Kufanya Mapenzi

Kusisimua Mwili na Akili: Jinsi ya Kuleta Msisimko katika Kufanya Mapenzi

Kusisimua Mwili na Akili: Jinsi ya Kuleta Msisimko katika Kufanya Mapenzi

Mapenzi ni moja ... Read More

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya mila na tamaduni za familia zenu

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya mila na tamaduni za familia zenu

Leo hii, nataka kuzungumzia kuhusu jinsi ya kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya mila na ... Read More

Njia za Kuboresha Uhusiano wa Kufanya Mapenzi: Ushirikiano na Mazungumzo

Njia za Kuboresha Uhusiano wa Kufanya Mapenzi: Ushirikiano na Mazungumzo

Njia za Kuboresha Uhusiano wa Kufanya Mapenzi: Ushirikiano na Mazungumzo

Kufanya mapenzi k... Read More

Vidokezo vya Kufanya Msichana Aonekuwa Muhimu katika Maisha Yako

Vidokezo vya Kufanya Msichana Aonekuwa Muhimu katika Maisha Yako

Mwanamke ni hazina kubwa katika maisha ya kila mwanaume. Ni kiumbe chenye thamani, cha thabiti na... Read More

Je, kuna umuhimu wa kuzungumzia kuhusu ngono/kufanya mapenzi ya salama na kinga dhidi ya magonjwa ya zinaa?

Je, kuna umuhimu wa kuzungumzia kuhusu ngono/kufanya mapenzi ya salama na kinga dhidi ya magonjwa ya zinaa?

Je, kuna umuhimu wa kuzungumzia kuhusu ngono/kufanya mapenzi ya salama na kinga dhidi ya magonjwa... Read More

Jinsi ya Kupunguza Shinikizo la Utendaji katika Kufanya Mapenzi: Kuwa na Mtazamo wa Kukubalika

Jinsi ya Kupunguza Shinikizo la Utendaji katika Kufanya Mapenzi: Kuwa na Mtazamo wa Kukubalika

Jinsi ya Kupunguza Shinikizo la Utendaji katika Kufanya Mapenzi: Kuwa na Mtazamo wa KukubalikaRead More

Njia za Kuimarisha Ushirikiano wa Kijamii na Kuweka Nafasi ya Shughuli za Pamoja katika Familia

Njia za Kuimarisha Ushirikiano wa Kijamii na Kuweka Nafasi ya Shughuli za Pamoja katika Familia

Habari za leo wapenzi wa ushirikiano wa kijamii, leo tutajadili njia za kuimarisha ushirikiano wa... Read More

Njia za Kuimarisha Umoja wa Kifamilia na Kuweka Maadili ya Pamoja

Njia za Kuimarisha Umoja wa Kifamilia na Kuweka Maadili ya Pamoja

Umoja wa kifamilia ni kitu muhimu katika maisha ya kila mmoja wetu. Familia ndiyo kitovu cha mais... Read More

Uhusiano wa Mbali na Kufanya Mapenzi: Njia za Kuimarisha Ushirikiano wakati wa Kutengana

Uhusiano wa Mbali na Kufanya Mapenzi: Njia za Kuimarisha Ushirikiano wakati wa Kutengana

Muda mrefu wa kutengana na mpenzi wako unaweza kuwa mgumu sana, hasa ikiwa mnatumiana kimapenzi. ... Read More