Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
☰
AckyShine

Kwa nini wasichana wakiingia utu uzima damu zinaanza kutoka kwenye uke?

Featured Image
Kutoka damu (hedhi) kwa mara ya kwanza kunaitwa kuvunja ungo na hii ni dalili ya mtoto wa kike kuingia utu uzima,0 yaani kuwa mwanamke. Wasichana wanavunja ungo kati ya umri wa miaka 8 na umri wa miaka 18. Lakini, kuvunja ungo haina maana kwamba unahitaji kuanza kujamii ana. Kwa sababu ukijamii ana kuna hatari ya kupata mimba!

Mwanzoni siku za hedhi zinaweza kuwa na mabadiliko sana. Ni baada ya muda ndipo msichana anaanza kwenda mwezini mara moja kila mwezi. Kwa wanawake wengi ni kila baada ya siku 28, hata hivyo, wengine huweza kupata hedhi chini au zaidi ya siku hizo. Idadi ya siku katika mzunguko wa hedhi ni siku 21 hadi 35.Ukitaka kuelewa kabisa maana ya kutoka damu za mwezi, lazima nieleze kuhusu mzunguko wa hedhi. Siku ya kwanza ya damu huhesabiwa kama siku ya kwanza ya mzunguko. Baada ya damu kutoka, yai moja linaanza kukua ndani ya kokwa.

Na vilevile utando ndani ya mfuko wa uzazi huanza kujengeka ili ukaribishe mimba. Kati ya siku 11 au 14 yai hupevuka ndani ya kokwa na halafu husafiri kwenye mirija ya kupitishia mayai hadi kwenye mfuko wa uzazi. Mwanamke anapata mimba kama yai likirutubishwa na mbegu ya kiume ndani ya mirija ya kupitisha mayai, i ina maana, kwamba atakuwa amejamii ana kipindi cha siku chache kabla ya yai kupevuka au siku yai linapopevuka. Kama yai halikurutubishwa, basi hufa na hutangulia kutoka kama ute, pia utando kwenye mfuko wa uzazi na kuta za uzazi hubomoka na kutoka kama damu. Hii ndiyo hedhi yenyewe.

Endapo msichana amejamiiana na mvulana na yai likarutubushwa, hataona hedhi na aelewe kwamba kuna uwezekano kwamba mimba imetungwa.

Mzunguko wa hedhi kwa baadhi ya wasichana hauna mpangilio mwanzoni, hivyo endapo hupati hedhi inayolingana kila mwezi usijali.

Katika hali ya kawaida usipopata hedhi na hukujamiiana na mvulana, basi inawezekana ni mabadiliko tu ya mwili. Hali hii ikiendelea au ukiwa na wasiwasi unashauriwa kumuona mtaalamu wa afya
AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Kwa nini inapendekezwa Kufanya Ngono na Mtu Mmoja Tu?

Kwa nini inapendekezwa Kufanya Ngono na Mtu Mmoja Tu?

Kwa nini inapendekezwa Kufanya Ngono na Mtu Mmoja Tu? 🌟

Karibu vijana wenzangu! Leo tut... Read More

Kwani Albino hawatakiwi kuishi duniani?

Kwani Albino hawatakiwi kuishi duniani?

Albino ni binadamu kama alivyo binadamu mwingine na ana haki
sawa za kuishi na kufaidi kuwep... Read More

Kwa nini jamii inatuchukia sisi Albino?

Kwa nini jamii inatuchukia sisi Albino?

Siyo watu wote katika jamii wanawachukia au kuwatenga Albino.
Wazazi, ndugu zenu, rafiki zen... Read More

Je, mtu anaweza kuzuia kupata mimba baada yakujamiiana bila kinga (kufanya ngono zembe) kwa mfano amebakwa?

Je, mtu anaweza kuzuia kupata mimba baada yakujamiiana bila kinga (kufanya ngono zembe) kwa mfano amebakwa?

Kama umebakwa au kulazimishwa kujamiiana unaweza kupata
huduma katika hospitali, kituo cha a... Read More

Magonjwa ya zinaa yanavyoenea

Magonjwa ya zinaa yanavyoenea

Magonjwa ya zinaa husababishwa na vijidudu vya magonjwa na huambukizwa kwa kukutana kimwili na mt... Read More

Je, kama wazazi watawapa dawa za kulevya watoto wao watashitakiwa kisheria?

Je, kama wazazi watawapa dawa za kulevya watoto wao watashitakiwa kisheria?

Ndiyo, watashtakiwa! Wakati mwingine wazazi huwatuma
watoto wao kuchukua au kununua pombe au... Read More

Kama wameoana mume na mke na ikatokea hawapati mtoto, je, utajuaje kuwa tatizo liko kwa mwanamke au mwanaume?

Kama wameoana mume na mke na ikatokea hawapati mtoto, je, utajuaje kuwa tatizo liko kwa mwanamke au mwanaume?

Kwa wastani i i inachukua kama muda wa mwaka mmoja kwa mwanamke kuanza kupata ujauzito, wakikutan... Read More

Je, ninaweza kuambukizwa na Virusi vya UKIMWI na UKIMWI kwa kuumwa na mbu?

Je, ninaweza kuambukizwa na Virusi vya UKIMWI na UKIMWI kwa kuumwa na mbu?

Hapana, mbu na wadudu wengine hawawezi i kukuambukiza virusi vya UKIMWI kutokana na mfumo wa mii ... Read More

Je, Ni Vipi naweza Kuepuka Shinikizo la Kufanya Ngono Katika Mahusiano?

Je, Ni Vipi naweza Kuepuka Shinikizo la Kufanya Ngono Katika Mahusiano?

Je, Ni Vipi naweza Kuepuka Shinikizo la Kufanya Ngono Katika Mahusiano? 🌼

Habari za leo... Read More

Magonjwa yatokanayo na sigara

Magonjwa yatokanayo na sigara

Kuna matatizo na magonjwa mengi na ya aina mbalimbali
unayoweza kuyapata kutokana na utuvaji... Read More

Utoaji wa zawadi kwa kubadilishana na kujamiiana

Utoaji wa zawadi kwa kubadilishana na kujamiiana

Kutoa zawadi kwa mtu kwa kubadilishana ili kujamiiana
ni unyanyasaji mbaya. Iwapo mpokeaji w... Read More

Nifanyeje Kukabiliana na Hisia za Uoga kabla ya Kufanya Ngono?

Nifanyeje Kukabiliana na Hisia za Uoga kabla ya Kufanya Ngono?

Jinsi ya Kukabiliana na Hisia za Uoga Kabla ya Kufanya Ngono 🌟

Karibu kwenye makala hii... Read More