Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
☰
AckyShine

Mambo usiyoyajua kuhusu mimba na wasichana

Featured Image

Je, mimba hupatikanaje?

Ukitaka kuelewa jinsi mimba i inavyopatikana, lazima uelewe mzunguko wa hedhi wa mwanamke. Baada ya kuvunja ungo (yaani kupata hedhi kwa mara ya kwanza) msichana hupata hedhi mara moja kila mwezi. Kwa wanawake wengi ni kila baada ya siku 28, hata hivyo wengine huweza kupata hedhi chini au zaidi ya siku hizo.
Siku ya kwanza ya hedhi huhesabiwa kama siku ya kwanza ya mzunguko. Baada ya damu kutoka, yai moja linaanza kukua ndani ya kokwa. Na vilevile utando ndani ya mfuko wa uzazi huanza kujengeka i ili ukaribishe mimba. Kati ya siku 11 au 14 yai hupevuka ndani ya kokwa na halafu husafiri kwenye mrija wa kupitisha mayai hadi mfuko wa uzazi. Mwanamke anapata mimba kama yai litaungana na mbegu ya kiume ndani ya mrija wa kupitisha mayai. Ina maana kwamba endapo atajamii ana kipindi cha siku chache kabla ya yai kupevuka au siku yai linapopevuka na kutoka kwenye kokwa, linarutubishwa wakati linaelekea kwenye mji wa mimba, na linapofika hapo kwenye mji wa mimba linatulia kwenye utando wa mji wa mimba. Mtoto anahifadhiwa na kukua ndani ya mji wa uzazi mpaka siku ya kuzaliwa. Kama yai halikurutubishwa, basi yai hufa na hutoka pamoja na utando wa mfuko wa uzazi na hutoka nje ya mwili wa mwanamke kama damu ya hedhi. Yaani, mwanamke atapata hedhi kama kawaida na atafahamu kwamba hajashika mimba.

Ni siku gani katika mzunguko wa hedhi yai linapoweza kurutubishwa?

Yai mmoja hupevuka siku 14 kabla ya hedhi i i inayofuata. Baada ya yai kukomaa ndani ya kokwa la upande wa kulia au wa kushoto, yai husafirishwa kwenye mrija wa kupitisha mayai mpaka kwenye mfuko wa uzazi.
Yai likijiunga na mbegu ya kiume ndani ya mrija wa kupitisha mayai siku zilezile, linaweza kurutubishwa. Yaani, endapo mwanamke anajamii ana kipindi cha siku chache kabla ya yai kupevuka au siku yai linapopevuka anaweza akapata mimba.
Kwa sababu wasichana wengi hawapati hedhi ya kawaida, yaani mzunguko wa siku 28 katika kila mwezi, ni vigumu sana kwao kufahamu tarehe ya hedhi i i inayofuata. Hivyo ni vigumu kujua lini litakuwepo yai linalongojea kurutubishwa.
Mzunguko wa hedhi kwa msichana unaweza kuathiriwa na mfadhaiko, huzuni, safari au mabadiliko mengine katika maisha ya msichana. Hata kama msichana ana mzunguko wa kawaida wa hedhi hali hiyo inaweza kubadilika ghafla na ukawa sio wa kawaida. Wanawake wengi na hasa wasichana hawawezi kutegemea kuhesabu siku kama njia ya kuzuia mimba, kwa sababu hawawezi kuwa na uhakika i iwapo lipo yai linalongojea kurutubishwa au la. Hakuna siku salama za kuepukana na mimba!

Ninaweza kupata mimba wakati nipo kwenye hedhi?

Ili mwanamke aweze kushika mimba, i inabidi yai lililopevuka likutane na mbegu za kiume. Yai pevu linapokosa mbegu hufa na kwa vile utando kwenye tumbo la uzazi ulishajiandaa kupokea yai lililorutubishwa hubomoka. Kwa pamoja, yai na utando hutoka kama damu kupitia ukeni na i le damu huitwa hedhi.
Hedhi ni dalili, kwamba yai halikurutubishwa na hivyo limeshakufa na kutoka. Kwa kawaida, wakati huo halitakuwepo yai jingine lililopevuka kuweza kurutubishwa na kwa hiyo uwezekano wa kupata mimba hautakuwepo. Lakini, mara chache kuna hitilafu katika mzunguko wa hedhi na yai jingine linakuwepo tayari kwa kurutubishwa, hata ukiwa kwenye hedhi. Kwa hiyo uwezekano wa kupata mimba wakati wa hedhi upo, hata kama ni mdogo.

Je, inawezekana msichana akapata mimba kabla ya kuvunja ungo?

Ndiyo, msichana anaweza kupata mimba kabla ya kuvunja ungo, yaani kabla ya kuona hedhi kwa mara ya kwanza. Kwa uhakika utajiuliza kwa nini.
Kabla ya kuona hedhi, yai ndani ya kokwa linapevuka na kusafiri kutoka kwenye kokwa mpaka tumbo la uzazi. Hedhi yenyewe ni dalili kwamba lile yai pevu halikurutubishwa na kwa hiyo linatoka pamoja na utando wa tumbo la uzazi kupitia ukeni.
Kuna maana kwamba hata kama msichana hajavunja ungo, i inawezekana kwamba ndani ya tumbo lake yai limeshaanza kupevuka. Lile yai linaweza kurutubishwa na msichana anaweza kupata mimba, hata kama hajaona hedhi yake kwa mara ya kwanza.

Je, msichana akijamiiana mara moja tu anaweza akapata mimba?

Ndiyo, msichana anaweza kupata mimba akijamii ana mara moja tu. Inategemea na mzunguko wa hedhi. Kama ndani ya tumbo la msichana lipo yai pevu ambalo ni tayari kwa kurutubishwa, na siku i ileile msichana anajamii ana na mvulana anaweza kupata mimba. Isitoshe, anaweza kupata mimba hata kama ni mara ya kwanza ya kujamii ana

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Watu wanaoishi na ulemavu wanapewa huduma za upasuaji hasa wakati wa kujifungua?

Watu wanaoishi na ulemavu wanapewa huduma za upasuaji hasa wakati wa kujifungua?

Upasuaji unafanyika kwa wanawake wote ambao wamegundulika
kuwa na tatizo la kujifungua kwa n... Read More

Jinsi ya Kujilinda na Mimba Bila Kusababisha Madhara ya Kiafya?

Jinsi ya Kujilinda na Mimba Bila Kusababisha Madhara ya Kiafya?

Jinsi ya Kujilinda na Mimba Bila Kusababisha Madhara ya Kiafya? 😊🌼

Karibu kijana! Le... Read More

Je, zipo sheria zinazolinda watu wenye ulemavu hapa Tanzania?

Je, zipo sheria zinazolinda watu wenye ulemavu hapa Tanzania?

Ndiyo, zipo sheria
hapa T a n z a n i a
z i n a z o w a l ... Read More

Kwa nini sio Sahihi Kufanya Ngono na Mtu Mmoja wa Marafiki?

Kwa nini sio Sahihi Kufanya Ngono na Mtu Mmoja wa Marafiki?

Kwa nini sio Sahihi Kufanya Ngono na Mtu Mmoja wa Marafiki? πŸŒΈπŸ’”

Jambo zuri siku zote ... Read More

Jinsi ya Kukabiliana na Hali ya Kujihisi Kukataliwa kuhusu Ngono

Jinsi ya Kukabiliana na Hali ya Kujihisi Kukataliwa kuhusu Ngono

Jinsi ya Kukabiliana na Hali ya Kujihisi Kukataliwa kuhusu Ngono 🌟

Karibu kwenye makala... Read More

Je, watu wanaamini nini katika kuongeza mchezo wa hisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, watu wanaamini nini katika kuongeza mchezo wa hisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, watu wanaamini nini katika kuongeza mchezo wa hisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi? Kufanya ... Read More

Kwa nini watu wanakunywa pombe?

Kwa nini watu wanakunywa pombe?

Unywaji wa pombe ni sehemu ya utamaduni wa Tanzania na nchi
nyinginezo duniani.

Watu h... Read More

Njia za Kujenga Mazingira ya Kuaminika katika Uhusiano wako na Msichana

Njia za Kujenga Mazingira ya Kuaminika katika Uhusiano wako na Msichana

Njia za Kujenga Mazingira ya Kuaminika katika Uhusiano wako na Msichana

Kamwe hufai kuhisi... Read More

Nifanyeje Kukabiliana na Hisia za Kuwa na Hamu ya Kufanya Ngono?

Nifanyeje Kukabiliana na Hisia za Kuwa na Hamu ya Kufanya Ngono?

Nifanyeje Kukabiliana na Hisia za Kuwa na Hamu ya Kufanya Ngono? πŸ˜ŠπŸ™Œ

Leo tutajadili j... Read More

Magonjwa yatokanayo na sigara

Magonjwa yatokanayo na sigara

Kuna matatizo na magonjwa mengi na ya aina mbalimbali
unayoweza kuyapata kutokana na utuvaji... Read More

Je, kama mwanamke na mwanaume wanapata watoto wa jinsia moja tu, ni kosa la nani?

Je, kama mwanamke na mwanaume wanapata watoto wa jinsia moja tu, ni kosa la nani?

Hakuna mwenye kosa, kwa sababu jinsia ya mtoto i inategemea na bahati na hamna uwezekano wa kupan... Read More

Njia za Kumshtua Msichana kwa Tarehe ya Kwanza

Njia za Kumshtua Msichana kwa Tarehe ya Kwanza

Hakuna kitu kizuri kama kukutana na msichana unayempenda kwa tarehe ya kwanza. Lakini, unapotaman... Read More