Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
AckyShine

Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Nyama, Mchicha, Maharage Na Chatini Ya Pilipili Mbichi

Featured Image

Vipimo Vya Mchuzi Wa Nyama

Nyama ya ng’ombe vipande vidogo - 2lb

Nyanya - 1

Kitunguu Kilichoktwa katwa - 1

Mafuta - 2 vijiko vya supu

Paprika (bizari ya masala ya rangi) - ½ kijiko cha chai

Kidonge cha supu - 1

Chumvi - Kiasi

Ndimu - Kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha nyama kwa chungio ili itoke maji. Kwenye sufuria, weka mafuta na ukaange vitunguu mpaka viwerangi ya hudhurungi.
Kisha tia nyama na kidonge cha supu uwachie moto mdogo mpaka iwive.
Halafu tia nyanya na paprika ufunike sufuria na uiwache motoni mpaka ikauke, kamulia ndimu na itakuwa tayari.

Vipimo Vya Mboga

Mchicha ulio katwa katwa 400 gm

Nyanya 1

Kitunguu kilicho katwa 1

Nazi ya unga kiasi

Pilipili mbichi 2

Mafuta ½ kijiko cha supu

Chumvi kiasi

Namna Ya Kutayarisha na Kupika

Osha mboga vizuri mpaka iwe haina mchanga.
Katika sufuria, kaanga vitungu hadi viwe laini.
Tia nyanya, mboga, pilipili na chumvi ikisha toa maji
Tia nazi na utaiwacha motoni mpaka ikauke kiasi na itakuwa
tayari kuliwa

Vipimo Vya Maharage

Maharage - 1 kopo

Kitunguu - 1

Nazi - 1 mug

Nyanya (itowe maganda) - 1 kiasi

Pilipili mbichi - 2

Mafuta - 1 kijiko cha supu

Chumvi - kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na kupika

Tia mafuta katika sufuria na ukaanga vitungu mpaka vilainike.
kisha tia nyanya na pilipili na ukaange kidogo.
Tia chumvi, maharage na nazi uwachie
moto mdogo mpaka iwe nzito kiasi na itakuwa tayari.

Vipimo Vya chatini Ya Pilipili mbichi

Pilipili mbichi - 4/5

Kotmiri - 1 Kijiko cha supu

Ndimu - kiasi

Kitunguu saumu(thomu/galic) - 1 chembe

Mafuta ya zaituni - 2 vijiko Vya supu

Chumvi - kiasi

Namna Ya Kutayarisha

Kwenye blender, tia vipimo vyote na sage isipokuwa chumvi tia mwisho kwa juu kwenye bakuli na itakuwa tayari kwa kuliwa.

Vipimo Vya ugali

Maji - 4 Vikombe kiasi inategemea na unga

Unga wa sembe - 2 vikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Tia maji kiasi katika sufuria, weka motoni, yakipata moto korogea unga wa sembe kiasi na ufanye uji mzito uache uchemke vizuri huku ukikoroga.
Chota kibakuli kimoja cha uji huo weka pembeni kisha mimina unga wote uliobaki upigepige uchanganyike vizuri kwenye uji huo mpaka ushikamane
Punguza moto anza kuusonga taratibu huku ukiongeza ule uji ulioweka pembeni kidogo kidogo mpaka uone sasa umeshikamana vizuri.
Endelea kusonga mpaka ulainike kisha mimina kwenye bakuli au sahani na itakuwa tayari kwa kuliwa na mchuzi wa nyama, maharage, mboga na chatini.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya kupika Slesi Za Chokoleti Na Karameli

Jinsi ya kupika Slesi Za Chokoleti Na Karameli

Viamba upishi

Unga 1 Magi (vikombe vya chai)

Sukari ya browni ½ Magi

Siagi i... Read More

Mapishi mazuri ya Uji wa ulezi

Mapishi mazuri ya Uji wa ulezi

Mahitaji

Unga wa ulezi (millet flour vijiko 3 vya chakula)
Maziwa fresh (milk 1/2 ki... Read More

Upishi wa Afya kwa Watoto: Milo Mzuri na Lishe Bora

Upishi wa Afya kwa Watoto: Milo Mzuri na Lishe Bora

Upishi wa Afya kwa Watoto: Milo Mzuri na Lishe Bora 🍎🥦

Habari za leo wapendwa wasoma... Read More

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Cornflakes

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Cornflakes

MAHITAJI

Unga - 1 Kikombe

Sukari ya kusaga - 3/4 Kikombe

Siagi - 125 gms

<... Read More
Mapishi ya Viazi, samaki na asparagus

Mapishi ya Viazi, samaki na asparagus

Mahitaji

Viazi (potato 1/2 kilo)
Samaki (fish 2)
Asparagus 8
Kitunguu kili... Read More

Jinsi ya kupika Mishkaki ya kuku

Jinsi ya kupika Mishkaki ya kuku

Kidali cha kuku 1 kikubwa
Swaum,tangawizi 1 kijiko cha chai
Limao 1/2
Pilipili ya ... Read More

Mapishi ya Bokoboko La Kuku

Mapishi ya Bokoboko La Kuku

Mahitaji

Ngano nzima (shayiri) - 3 Vikombe

Kuku - ½ (3 LB takriban)

Thomu na... Read More

Mawazo ya Chakula cha Usiku cha Dakika 20 kwa Familia Yote

Mawazo ya Chakula cha Usiku cha Dakika 20 kwa Familia Yote

Mawazo ya Chakula cha Usiku cha Dakika 20 kwa Familia Yote 🌮🍝🍗

Kama AckySHINE, le... Read More

Mapishi ya Chicken Satay

Mapishi ya Chicken Satay

Mahitaji

Kidali cha kuku 1 (chicken breast)
Kitunguu maji 1/2 (onion)
Kitunguu ... Read More

Mapishi ya Wali Wa Mboga Na Samaki Wa Pink Salmon

Mapishi ya Wali Wa Mboga Na Samaki Wa Pink Salmon

Vipimo

Mchele 3 vikombe

Mboga mchanganyiko 1 kikombe

Samaki wa Pink Salmon 5 ... Read More

Upishi na Protini Ndogo: Kujenga Misuli na Kukaa Fiti

Upishi na Protini Ndogo: Kujenga Misuli na Kukaa Fiti

Upishi na Protini Ndogo: Kujenga Misuli na Kukaa Fiti 💪💪

Kuna njia nyingi za kubores... Read More

Mapishi ya wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Nyama Ng’ombe Na Mchicha

Mapishi ya wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Nyama Ng’ombe Na Mchicha

Wali Wa Mpunga

Mchele wa mpunga - 4 Vikombe

Tui la nazi - 6 vikombe

Chumvi - ... Read More