Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
AckyShine

Jinsi ya kutengeneza Wali Wa Dengu Kwa Samaki Wa Kukaanga

Featured Image

Mahitaji

Mchele wa basmati - 3 Vikombe

Dengu - 2 vikombe

Viazi - 3 vikubwa

Kitunguu - 2 kubwa

Nyanya - 2

Pilipili mbichi kubwa - 3

Pilipilimanga - ½ kijiko cha chai

Garama Masala (bizari mchanganyiko) -1 kijiko cha chai

Supu ya vidonge (stock cubes) - 2 vidonge

Chumvi - kiasi

Mafuta - ¼ kikombe

Zaafarani - 1 kijiko cha chai

Samaki wa kukaanga

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Dengu kama sio za tayari kwenye kopo, roweka na zichemshe hadi ziwive

Maandalizi ya Masala Ya Dengu:

Zaafarani – iroweke katika maji ya dafu dafu (warm) ya chini ya robo kikombe weka kando.
Osha mchele, roweka.
Menya viazi na vitunguu, katakata vitunguu, na nyanya , weka kando.
Katakata viazi vipande vidogo vidogo kwa umbo la mchemraba (cubes).
Katika sufuria tia mafuta yakipata moto, tia viazi ukaange kidogo kwa moto mdogo mdogo hadi kukaribia kuwiva, toa weka kando.
Kaanga vitunguu hadi vigeuka rangi ya hudhurungi isiyokoza (light brown) kisha tia nyanya ukaange kidogo.
Tia vidonge vya supu (stock cubes) uvivuruge katika mchanganyiko, katakata pilipili mbichi kwa urefu tia, uendelee kukakaanga. Tia bizari, chumvi.
Zima moto, changanya dengu na viazi katika mchanganyiko huo.

Mapishi ya Wali:

Chemsha mchele kama kawaida ya kupika wali mweupe, kiini kiwe kimewiva nusu yake.
Chuja maji kisha changanya katika mchanganyiko wa dengu.
Nyunyizia zaafarani, uchanganye wali na mchanganyiko kidogo tu.
Funika acha uive katika mtoto mdogo mdogo au tia katika oveni hadi uive kama kawaida ya kupika wali.
Pakua katiha sahani na tolea na samaki yoyote wa kukaanga.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Tende Na Ufuta

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Tende Na Ufuta

MAHITAJI

Unga - 3 Vikombe vya chai

Baking powder - 1 ½ Vijiko vya chai

Sukar... Read More

Jinsi ya kutengeneza biskuti za Matunda Makavu Na Cornflakes

Jinsi ya kutengeneza biskuti za Matunda Makavu Na Cornflakes

VIAMBAUPISHI

Unga - 4 Vikombe

Sukari - 1 Kikombe

Baking powder 1 kijiko cha c... Read More

Mapishi ya Biriani Ya Samaki Nguru, Njegere Na Snuwbar (UAE)

Mapishi ya Biriani Ya Samaki Nguru, Njegere Na Snuwbar (UAE)

Mahitaji

Mchele wa basmati - 4 cups

Samaki nguru (king fish) - 7 vipande au zaidiRead More

Jinsi ya kupika Wali Wa Kichina wa mboga mboga Na Mayai

Jinsi ya kupika Wali Wa Kichina wa mboga mboga Na Mayai

Viambaupishi

  1. Mchele (Basmati) - 3 vikombe
  2. Mbogamboga za barafu (karot, njege... Read More
Mapishi ya Wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Samaki Na Rojo La Bilingani Na Viazi/Mbatata

Mapishi ya Wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Samaki Na Rojo La Bilingani Na Viazi/Mbatata

Wali Wa Nazi

Mpunga - 4 vikombe

Tui la nazi - 6 vikombe

Chumvi - Kiasi

Read More
Jinsi ya kuandaa Ndizi Mbichi Za Supu Ya Nyama Ng’ombe

Jinsi ya kuandaa Ndizi Mbichi Za Supu Ya Nyama Ng’ombe

Mahitaji

Ndizi mbichi - Kisia

Nyama ng’ombe - ½ kilo

Pilipili ya kusaga - ... Read More

Jinsi ya kupika Wali Wa Sosi Ya Tuna

Jinsi ya kupika Wali Wa Sosi Ya Tuna

Viambaupishi

Sosi Ya tuna

Tuna (samaki/jodari) 2 Vikopo

Vitunguu (kata kata) ... Read More

Jinsi ya kupika Cookies Za Jam Ya Peach Na Raspberry

Jinsi ya kupika Cookies Za Jam Ya Peach Na Raspberry

MAHITAJI

Unga kikombe 1 ½

Siagi ½ kikombe

Sukari ½ kikombe

Yai 1

... Read More
Mapishi ya Wali Wa Zaafarani Na Kuku Wa Kupaka

Mapishi ya Wali Wa Zaafarani Na Kuku Wa Kupaka

Vipimo

Wali:

Mchele - 3 Vikombe

Kitunguu kiichokatwa - 1

Pilipili bog... Read More

Mapishi ya Mchemsho wa ndizi na nyama

Mapishi ya Mchemsho wa ndizi na nyama

Mahitaji

Ndizi mbichi 6
Nyama ya ng'ombe (nusu kilo)
Viazi mviringo 2
Kitu... Read More

Jinsi ya kuandaa Pilau ya sosi ya soya, nyama na mboga

Jinsi ya kuandaa Pilau ya sosi ya soya, nyama na mboga

Mahitaji

Nyama isiyokuwa na mifupa - 1 ½ Lb(ratili)
Mchele wa Basmati (rowanisha) -... Read More

Jinsi ya kupika Mitai

Jinsi ya kupika Mitai

VIAMBAUPISHI

Unga wa ngano 1 1/2 Kikombe

Baking powder 1 Kijiko cha chai

Bak... Read More