Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
AckyShine

Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Kamba Wa Nazi, Kisamvu Na Kachumbari Ya Papa Mkavu

Featured Image

Vipimo - Ugali

Maji - 4 vikombe kiasi inategemea na unga wenyewe.

Unga wa sembe - 2 vikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Tia maji kiasi katika sufuria, weka motoni, yakipata moto korogea unga wa sembe kiasi na ufanye uji mzito uache uchemke vizuri huku ukikoroga.
Chota kibakuli kimoja cha uji huo weka pembeni kisha mimina unga wote uliobaki upigepige uchanganyike vizuri kwenye uji huo mpaka ushikamane
Punguza moto anza kuusonga taratibu huku ukiongeza ule uji ulioweka pembeni kidogo kidogo mpaka uone sasa umeshikamana vizuri.
Endelea kusonga mpaka ulainike kisha mimina kwenye bakuli au sahani iliyolowanishwa na maji kisha upete pete huku ukiugeuza geuza mpaka ukae shepu nzuri ya duara.Weka tayari kwa kuliwa.

Vipimo - Mchuzi wa kamba wa nazi

Kitunguu - 1

Nyanya - 2

Kamba waliomenywa - 1 Kilo

Pilipili mbichi iliyosagwa - ½ kijiko cha chai

Kitunguu saumu na tangawizi ilivyosagwa - 1 kijiko cha supu

Nazi nzito iliyochujwa - 1 kikombe

Bizari ya mchuzi - ½ kijiko cha chai

Chumvi - Kiasi

Ndimu - Nusu

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Safisha na osha kamba vizuri kisha mtie katika sufuria. Katia kitunguu, nyanya, tia chumvi, pilipili mbichi ya kusaga, thomu na tangawizi, bizari ya mchuzi na ndimu. Tia maji kidogo kiasi acha ichemke.
Watakapoiva na karibu kukauka, mimina tui la nazi taratibu koroga kiasi
Punguza moto aacha ichemke kidogo ukiwa mchuzi tayari.

Vipimo - Kisamvu

Kisamvu - 2 vikombe

Kunde mbichi zilizochemshwa - 1 kikombe

Kitunguu - 1

Nazi nzito iliyochujwa - 1 vikombe

Chumvi - Kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Weka kisamvu katika sufuria, katia kitunguu, tia chumvi, maji kidogo acha kichemke.
Huku ikichemka mimina kunde mbichi zilizochemshwa acha zipikikie kidogo mpaka kisamvu kikaribie kukauka na kunde kuiva.
Mimina nazi nzito punguza moto acha ichemke kidogo, mimina kwenye bakuli tayari kwa kuliwa.

Vipimo - Kachumbari Ya Papa

Papa mkavu (au nguru) - kipande

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Muoshe papa vizuri atoke mchanga kisha mchome kwenye jiko la mkaa au unaweza kumtia kwenye treya kisha kwenye oven kwa moto wa 350 kwa dakika 15 mpaka 20.
Akikauka mchambue chambue weka kando.
Tengeneza kachumbari, kwa kukata kitunguu, nyanya na pilipili mbichi, tia ndimu na chumvi.
Changanya na papa mkavu uliyemchambu ikiwa tayari.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Vidokezo 10 vya Vitafunio visivyo na Karanga

Vidokezo 10 vya Vitafunio visivyo na Karanga

Vidokezo 10 vya Vitafunio visivyo na Karanga 🥜🚫

Kama unapenda kufurahia vitafunio na... Read More

Vyakula vya Kutayarishwa Mapema kwa Afya Vinavyofaa kwa Usiku wa Juma

Vyakula vya Kutayarishwa Mapema kwa Afya Vinavyofaa kwa Usiku wa Juma

Vyakula vya Kutayarishwa Mapema kwa Afya Vinavyofaa kwa Usiku wa Juma

🌙🥘

Usik... Read More

Mapishi ya Chapati za Kusukuma kitaalamu

Mapishi ya Chapati za Kusukuma kitaalamu

Mahitaji

Unga wa ngano (plain flour 1/2 of kilo)
Siagi (butter vijiko 2 vya chakula)... Read More

Madhara ya nyama nyekundu kwa mtu mwenye VVU

Madhara ya nyama nyekundu kwa mtu mwenye VVU

Kuna nyama za aina mbili, nazo ni nyama nyeupe na nyama nyekundu.

Nyama nyeupe

Hi... Read More

Jinsi ya kupika Mitai

Jinsi ya kupika Mitai

VIAMBAUPISHI

Unga wa ngano 1 1/2 Kikombe

Baking powder 1 Kijiko cha chai

Bak... Read More

Mapishi ya Ndizi na Nyama Ya Ng’ombe

Mapishi ya Ndizi na Nyama Ya Ng’ombe

Mahitaji

Ndizi mbichi - 10-12

Nyama ng’ombe - 1 kilo moja

Kitunguu maji - 2... Read More

Namna ya kutengeneza Visheti Vya Nazi Na Njugu (Sudani)

Namna ya kutengeneza Visheti Vya Nazi Na Njugu (Sudani)

VIAMBAUPISHI

Unga - 3 mug za chai

Samli - ½ mug ya chai

Maziwa - 1¼ mug ya ... Read More

Mapishi ya Maini ya ng'ombe

Mapishi ya Maini ya ng'ombe

Mahitaji

Maini (Cow liver) 1/4 kilo
Vitunguu (chopped onion) 2
Nyanya (chopped ... Read More

Mapishi ya Kabichi

Mapishi ya Kabichi

Mahitaji

Kabichi 1/2 kilo
Nyanya ya kopo 1/2
Kitunguu 1
Curry powder 1/2 k... Read More

Jinsi ya kupika Baklawa Za Pistachio Na Lozi

Jinsi ya kupika Baklawa Za Pistachio Na Lozi

VIAMBAUPISHI

Philo (thin pastry) manda nyembamba - 1 paketi

Siagi - ¼ Kikombe cha ... Read More

Mapishi ya Mihogo ya nazi na kuku

Mapishi ya Mihogo ya nazi na kuku

Mahitaji

Mihogo kilo 1
Kidali cha kuku 1 kikubwa
Nyanya 1 kubwa
Kitunguu m... Read More

JINSI YA KUANDAA VILEJA

JINSI YA KUANDAA VILEJA

MAHITAJI

Unga wa mchele - 500g

Samli - 250g

Sukari - 250g

Hiliki iliyos... Read More